Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Hamna kitu kinaitwa Makabila ya Mipakani. Ila Kuna makabila yaliyopo pande zote katika nchi mbili zinazopakana. Mfano Wamaasai wapo kuanzia MASAI Mara hadi Mvomero na Kilosa. Tambarare lote la bonde la ufa kuanzia Kenya, Ngorongoro, Longido, Monduli, Simanjiro, Kiteto hadi Mvomero na Kilosa ni Umasaaini.

Utasemaje Wamaasai ninkabila la Moakani.

Upande wa Mwambao Wadigo wanaanzia Mombasa hadi Tanga.

Hivyo, mipaka halisi kama tunahitaji kuwa na mipaka kufuata alama muhimu kama mito, milima, maziwa n.k
 
Ukienda mahakaani na hii attitude utashindwa na kutupwa ndani kwa kudharau mahakama.
Hamna mahakama inayofanya kesi za migogoro ya mipakankama vile inaamua kesi kupigana.

Ndo maana hata migogoro yetu ya mipaka ya vijiji vinashughulikiwa na mabaraza yake ya ardhi na pale inapobidhi inaoelekwa mahakama ya ardhi. Siyo mahakama za kawaida.

Migogoro ikigoma kutatulika huwa shahidi wa mwisho ni ridhaa ya wananchi kwamba wanataka kuwa sehemu ya mamlaka ipi.

Kwa migogoro wa Ziwa Nyasa hakuna maamuzi mengine yoyote yatakayokubakika zaidi ya mpakankuwa katika kina kina kirefi Cha Ziwa.

Hapo msihangaike na ushabiki. Na katika kesi ya Mwaka 2012 iliamuliwa hivo Kwa hukumu ya upande Moja baada ya Malawi kuingia mtini baada ya kuona wanashindwa hoja zao.

Mikataba ya Kikolini mengi imeputwa na wakati. Ndo maana hata Ethiopia imejenga Bwawa kubwa kuliko yote Afrika pamoja na Misri kudai kuwa mwenye haki ya maji yote ya Moto Nile.
Hata Tanzania tayari tumetoa maji Ziwa Victoria kwenda hadi Tabora na Nzega na tunayaleta Dodoma Kwa ajili ya Kilimo na matumizi ya majumbani
 
Kwani hilo ziwa hata tukilipqta linaleta ugali? Tuna mambo mangapi ya thamani kubwa kuliko hilo ziwa na hayajaleta tija yoyote?.

Waacheni Walawi wchukue kilicho chao.
 
Kwa hiyo ziwa Nyasa likifurika hadi mji wa Kyela, mpaka unahama? Wazungu walikuwa na akili nyingi walipoamua mipaka ya maji kupita katikati ya water bodies. Mpaka wa Kimataifa haitakiwi kuwa flexible. Ni fixed.
 
Well
 
Kama hutaki kuabudu mipaka ya wakoloni basi nami nasema mkoa wa Tanga ni sehemu ya Kenya na pia mkoa wa Kigoma ni sehemu ya Burundi. Ili nisiabudu mipaka ya wakoloni.

Unaweza tuonyesha ramani ya Tanganyika yenye mipaka isiyo ya wakoloni?
 
Kama hutaki kuabudu mipaka ya wakoloni basi nami nasema mkoa wa Tanga ni sehemu ya Kenya na pia mkoa wa Kigoma ni sehemu ya Burundi. Ili nisiabudu mipaka ya wakoloni.

Unaweza tuonyesha ramani ya Tanganyika yenye mipaka isiyo ya wakoloni?
Swali muhimu sana
 
Kama hutaki kuabudu mipaka ya wakoloni basi nami nasema mkoa wa Tanga ni sehemu ya Kenya na pia mkoa wa Kigoma ni sehemu ya Burundi. Ili nisiabudu mipaka ya wakoloni.

Unaweza tuonyesha ramani ya Tanganyika yenye mipaka isiyo ya wakoloni?
Katika Mipaka ya Wakoloni Burundi haijawahi kuwa nchi. Ni sehemu ya Tanganyika. Sasa tuambie huo Mkataba ulioipa Bundi hadi la Koloni rasmi na nchi.

Kama unaabudu mipaka ya Mkoloni Tanganyika turudishiwe Rwanda, Burundi na Kyonga Triangle (Cabo Delgado).
 
Yule mwanamke aliye ruka makachu akiwa uchi mmeshamalizana nae?
 
Tusipotoshe, haitatusaidia kitu. Kesi ya Ziwa Nyasa sisi ndiyo tuliojitoa baada ya kuona tutashindwa. Nafikiri haikuendelea baada ya msuluhishi kutushauri tukae mezani. Na hakuna sheria ya kimataifa inayoongoza mipaka kwenye inland water bodies. Zipo sheria za mipaka baharini tu.

Tupambane tupate ushahidi wa kutusaidia kwenye kesi, tusipotoshe na kujifariji.
 
Ungemtaja kwa kimatumbi hatakuwelewa Lunatic kama huyo yaani ni K. Viumbe vya ziwani vinahudumiwa na nchi kavu . So nchi yetu ifanye kuhudumia ziwa linalomilikiwa na malawi. Haya ma pimbi ndo yalipaswa kukimbizana na wasiojulikana manina
 
Ni sawa na kusema eti Zanzibar ni nchi huki mtu akivunia kuwa kuna Tanzania. Kuna wakati visiwa vile tutavihesabu kama mikoa yetu, kama wanajivunia waarabu tunajua hizo dila hazina uwezo wa kusimamia jambo ukitaka kujua nenda Mashariki ya kati.
Nije kwenye mada.
Kabla ya google ramani ilikuwaje
Kuna mipaka ya Wajerumani, na kuna mipaka ya Waingerreza lkn kanla ya hao kulikuwa na watu walishije?
Kwamba Qanyakyusa walio upande wa pili wa ziwa watakuwa hawana uhalali wa kutumia ziwa eti lote liko Malawi, mtu atumie hata kichwa kile kidogo basi kwa mamba madogo kama haya.
Aliyedanganya wata loose hadi Pusi maana kuna wanyakyusa huko.
 
Kabla ya
 
Katika Mipaka ya Wakoloni Burundi haijawahi kuwa nchi. Ni sehemu ya Tanganyika. Sasa tuambie huo Mkataba ulioipa Bundi hadi la Koloni rasmi na nchi.
Kabla ya Wajerumani kuja kikuwepo na territory inaitwa Tanganyika? Hakuna.

Wakati wakoloni wanakuja waliikuta Kingdom of Burundi ikiongozwa na Mwami kina Ntare, na kabla ya hiyo kulikuwepo na Kitala empire ambayo iliunganisha baadhi ya jamii za Waganda na Wahaya. Wewe Mfalme wa Tanganyika uliwahi msikia?

Burundi ilikuwa nchi hata kabla ya Tanganyika iliyobumbwa na wakoloni.

Hizo nyingine ni developments za baadae. League of Nations mwaka 1922 inaitaja Luanda-Urundi. Baadae zinajitenga kwenye uhuru na kuwa nchi mbili Rwanda na Burundi sababu hata kabla ya wakoloni kuja zilikuwa zinajua mipaka yake na tawala ni tofauti.
Kama unaabudu mipaka ya Mkoloni Tanganyika turudishiwe Rwanda, Burundi na Kyonga Triangle (Cabo Delgado).
Turudishiwe na nani? Nani alizichukua Rwanda, Burundi na Cabo Delgado?
Kwanini Tanganyika isiwe ndio irudishwe kwa Burundi kama ndio hivyo.
Sababu Burundi wana falme tangu miaka ya 1500s, Tanganyika imebumbwa mwishoni mwa 1800s kwa kuunganisha makabila ambayo hata hayakuwa yanajua kama yapo. Mndendeule akaambiwa na Mjerumani eti yeye na Mzanaki ni nchi moja.

Bado hujanipa ramani ya Tanganyika isiyo ya wakoloni mkuu.
 
Huyo pimbi muache ajifiche kwenye keyboard ya simu ,aende awaambie wajinga wenzie wajaribu ajue huo mkoa anaoutetea unadanganywa na hao waliowaongopea kutumia google. Huyu ni msaliti tu kama wasaliti wengine
 
Sijasoma maelezo,ila Nipo tayari kwenda vitani Tanganyika ikimegea aridhi yake hata hatua ya Kidole kimoja.We fight so as to live peacefully.
 
Kabla ya wakoloni hawajaigawa sehemu hiyo Kwa utashi wao wenyeji walikuwa wanatumia Hilo ziwa Kwa matumizi Yao ya kila siku na kiasili wanahaki nalo! Huwezi kupora haki ya ziwa lao kwa sababu wazungu wameamua wanavyotaka wako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…