Utata wa mpaka wa ziwa Nyasa: Google map wako sahihi kwa 100%, serikali ya Tanzania msipotoshe na kutisha watu

Mpaka uliwekwa na wakoloni, na ndio mipaka hiyo hiyo tumeirithi karibu sehemu zote hapa Afrika.
Kabla ya mkoloni hakukuwa na nchi ya Tanganyika.
Bado ningependa kujua kama kuna nchi yeyote inayomiliki ziwa ama mto kwa asilimia 100 kama sehemu ya mpaka wake. Kwa hii scenario Tanzania iko sawa kuchora mpaka wake kama tunavyotambua sasa.
 
Tufanye kama Ukraine na dubu
 
Wamalawi si wajinga kama tunalitaka hilo Ziwa tulinunue sasa..ramani ya mjerumani ambaye ndio alionganisha makabila yote akaitengeneza Tanganyika inaonyesha ziwa Nyasa halipo kwetu, kuna agenda gani nyuma ya hili ?

View attachment 3183845
Kwa hiyo na sisi tuidai Rwanda na Burundi kuwa ni sehemu ya nchi yetu?
 
Kwa hiyo maji yakizidi yakila ardhi mpaka wao nao unaongezeka?
 
Kwa hiyo na sisi tusitumie maji ya ziwa Victoria ambapo ndiyo asili ya mto Nile kwa kuwa mkoloni aliwekeana saini na Misri kwamba mwenye maamuzi ya mwisho wa mto Nile ni Misri?
 
Sisi tunachojua mpaka uko kati kati ya ziwa hizo porojo zako za Google maps wapelekee wachambawima wenzako
Nyie na nani wakati hata Tanganyika hauijui! Wewe Tanganyika unaijua Nyerere tu! Nayo ni ya upande mmoja! Eti ilikuwa koloni la uingereza! Ingekuwa hivyo tusingekuwa hivi, tungekuwa na akili.
 
Nashukuru sana kwa kujenga hoja na kunipinga kwa hoja na busara kubwa, nami nitajibu hoja zako.

1. Ukweli hauna mmiliki, ukweli upo siku zote na unasimama wenyewe. Ukweli ninaousema hapa, ni kile kinachotambulika kisheria kimataifa.
Ukiondoa hapa Tanzania ambapo tangu tukiwa watoto tumekuwa tukifundishwa (hewani hewani tu) kitu kinaitwa ziwa Nyasa, na ziwa hilo lipo Tanzania, hakuna mahali pengine popote duniani utakutana na hicho kitu kielimu. Dunia nzima wanajua kuna Ziwa Malawi, kiasili ni mali ya Malawi na kwa sehemu Msumbiji wamepata umiliki toka kwa Malawi.
Hivi unajua ni kwanini Tanzania haitaki kabisa watanzania walifahamu kama ni ziwa Malawi ambalo ndio jina lake rasmi kiulimwengu?

2. Anayeamua mpaka uwe wapi sio mtu au nchi fulani yenyewe bali mikataba ya kimataifa ya kihistoria au kisiasa inayokubalika kiulimwengu (UN). Na hiyo ndio inatambua wazi na kutamka bayana kuwa mpaka wa Ziwa Nyasa upo pwani ya ziwa upande wa Tanzania na sio katikati ya ziwa. Mipaka karibu yote hapa Africa tumerithi kutoka kwa ukoloni, sehemu chache tumeiboresha na sehemu zingine tumeitengeneza upya kwa vita na migogoro.
 
Usijali hadi zile mile kumi za sultani kutokea pwani ya kenya hadi tanganyika mnaweza kuzidai na mkazipata.

Hivi kwa nini wazanzbari mna chuki kali dhidi ya wabara
Wabara ndio nini ?
 
UN wanatambua Anglo-Germany treaty kama ndio msingi wa kuelezea mpaka wa Ziwa Malawi (Nyasa). Nimeona hiyo Anglo-Germany treaty, na inasema wazi Malawi ndio wamiliki wa ziwa lote la Nyasa. Tanzania tumekuwa tukiupinga huo mkataba wa Heligoland treaty kutumika kama msingi wa kujua mpaka wa Ziwa Nyasa kwa hoja kuwa haukutenda haki, una kasoro na umekosa uhalisia (jambo ambalo hata mimi naliunga mkono kwa 100%), lakini mpaka leo hii UN haijawahi kuukataa huo mkataba wa Heligoland kutumika katika kuelezea mpaka wa ziwa Nyasa. Na hukujawahi kuwepo tena mkataba mpya wa kutambua mpaka katika ziwa hilo baina ya Malawi na Tanzania.

Mzozo uliozuka mwaka 2012 ulitokana na Malawi kutaka kuanza kuchimba mafuta katika ziwa Nyasa upande ambao Tz tunadai ni mali yetu, na Tz kutishia kuingia vitani dhidi ya Malawi, na hiyo ikapelekea Malawi kutaka kushtaki kwa kuzuiwa kutumia rasimali inazozimiliki.
 
Sawa badi tuwape ziwa lao, haitatusaidia kuendelea kung'ang'ania mali isiyo yetu.
Labda hao walio andaa hiyo Anglo-germany traty walikosea, kwa hoja za kitanzania, naamini seriksli ya Tanganyika inalifanyia kazi hili.
 
Kwa hiyo na sisi tuidai Rwanda na Burundi kuwa ni sehemu ya nchi yetu?
Tukiweza tudai Africa nzima ni ya kwetu kwani binadamu wa kwanza aliishi Olduvai Gorge Tanzania
 
Mkuu 'Zanzibar ASP', hii historia wewe ulijifunzia wapi; kwamba kuna Ziwa Malawi? Umejifunzia nchi gani historia hiyo na lini?
Kwani nchi ya Malawi imekuwa Malawi lini, kabla yako kuzaliwa?
Ziwa Tanganyika lipo hapo, na lenyewe tulidai kuwa ni Ziwa Tanzania, mali ya Tanzania; au siy; kwa mujibu wa haya uliyo eleza hapa.
Hapana, ziwa kuitwa Nyasa au Malawi siyo sababu ya ziwa kuwa sehemu ya nchi yenye jina hilo.
Unasema Msumbiji walipewa? sehemu ya ziwa na Malawi...; kwa makubaliano gani? Tanzania haina sababu ya kuomba kugawiwa sehemu ya ziwa; kwa sababu sehemu hiyo kimaumbile; ndiyo kimaumbile mbali ya hizo sheria unazo zitanguliza hapa, ni eneo tambulika enzi na enzi kuwa ni sehemu ya wakazi waliokuwepo kwenye eneo hilo hata kabla Tanganyika haijakuwepo.
Hakuna sheria inayo izidi sheria ya kimaumbile kama hiyo.
 
Nyie na nani wakati hata Tanganyika hauijui! Wewe Tanganyika unaijua Nyerere tu! Nayo ni ya upande mmoja! Eti ilikuwa koloni la uingereza! Ingekuwa hivyo tusingekuwa hivi, tungekuwa na akili.
Mimi na mama yako ndio tunajua na wewe ndio hauna akili kuandika vizuri tuu hauwezi
 
Kuwa mzalendo; Acha ujinga. Taifa Kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…