Utata wa ndugu kutoka bush

Utata wa ndugu kutoka bush

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
  • Tukiwa wadogo tulitembelewa na binamu yetu kutoka kijijini. Tulimpokea vizuri na kwasababu tulikuwa rika moja tukalala pamoja. Usiku ule tulikula chips na nyama za kukaangwa. Ndugu yangu yule alishangaa tunaweka tomato sauce, akadhani damu.
Alipoionja akadatishwa na ladha yake. Akamimina kwa fujo kwenye sahani yake.
Kesho yake tukaenda Imalaseko supermarket, Zamani ndio ilikuwa mpango mzima. Baba akasema Kila mtu achukue anachotaka. Jamaa akabeba tomato sauce tatu, kufika kwenye gari kaanza kunywa Kama soda.
  • Ndugu yetu mwingine wa kike alikuja kututembelea from bush na ilikuwa ni mara yake ya Kwanza kufika mjini. Akapewa chumba chake self contained, choo Cha kuchuchumaa, akaelekezwa namna ya kukitumia.Akaelekezwa pia namna ya kutumia jiko.
Kesho yake dada kaamka mapema ili apike chai, bahati mbaya maji jikoni yakawa hayatoki. Akaenda kwenye public toilet kulikuwa na choo cha kukaa, mama akashangaa mtu anaingia chooni na sufuria na kikombe, mama akamfuata, akamuuliza vipi? Akajibu nimeona Kuna mtungi mweupe ndio nimekuja kuchota maji ya chai.
 
Siku hizi watu wa Bush sio washamba tena, teknolojia imeenea kote👌
 
Back
Top Bottom