Utata wa vyeti vya O-level na A-level vya Mosses Kusiluka wa Mwalimu Nyerere Academy

Utata wa vyeti vya O-level na A-level vya Mosses Kusiluka wa Mwalimu Nyerere Academy

Uzalendi

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2013
Posts
221
Reaction score
15
Kuna utata katika majina ya Mosses Kusiluka wa Mwalimu Nyerere na Dr.Mosses Kusiluka wa Ardhi University. Hili suala linafaa kuchunguzwa kwani Dr.Magoti wa Mwalimu Nyerere Academy ameoa nyumba moja na Prof.Kusiluka aliyekuwa DVC Academy wa OUT na ndio maana alimuajiri Mosses Kusiluka ambaye vyeti vyake vina utata/walakini.

Dr.Magoti pia alimuajiri Erasto Muhagama aliyetumia vyeti vya kugushi na alipofichuliwa baada ya kumsomesha degrii ya pili alimshauri aache kazi baada ya TAKUKURU kuanza kufatilia.

Kwa kuwa Serikali inahakiki vyeti ni vema kuanzia na hili na kuwawajibisha viongozi wa Mwalimu Nyerere ambao wanapeana kazi kindugu na kufumbia macho kughushi vyeti na ufisadi mbalimbali kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa. Nawasilisha kwa hatua za haraka.
 
Kuna utata katika majina ya Mosses Kusiluka wa Mwalimu Nyerere na Dr.Mosses Kusiluka wa Ardhi University. Hili suala linafaa kuchunguzwa kwani Dr.Magoti wa Mwalimu Nyerere Academy ameoa nyumba moja na Prof.Kusiluka aliyekuwa DVC Academy wa OUT na ndio maana alimuajiri Mosses Kusiluka ambaye vyeti vyake vina utata/walakini.

Dr.Magoti pia alimuajiri Erasto Muhagama aliyetumia vyeti vya kugushi na alipofichuliwa baada ya kumsomesha degrii ya pili alimshauri aache kazi baada ya TAKUKURU kuanza kufatilia.

Kwa kuwa Serikali inahakiki vyeti ni vema kuanzia na hili na kuwawajibisha viongozi wa Mwalimu Nyerere ambao wanapeana kazi kindugu na kufumbia macho kughushi vyeti na ufisadi mbalimbali kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa. Nawasilisha kwa hatua za haraka.

Mwl.Nyerere Academy hiyo ya Mbezi ama ipi....?...nijibu kwanza then ntachangia kitu hapa
 
Mwalimu Nyerere Academy?????????????????????? Nimetoka kapa
 
Kama Walimu wanaofundisha hapo ndio hao elimu ya Chuo hiki ina kitu kweli, Serikali ichukue hatua kunusuru hili haraka iwezekanavyo maana wazazi watapoteza ada yao bila watoto wao kupata wanachotaka.
Mwalimu Nyerere Academy?????????????????????? Nimetoka kapa
 
Tunalidhalilisha mno jina la baba wa Taifa, vitu kibao viko sub~standard au viko kifisadifisadi halafu tunavipa jina la Nyerere .ni upumbavu hiyo sio njia sahihi ya kumuenzi
 
Hata Dr,Salim M/Kiti wa Bodi ya Chuo anaharibiwa jina lake bila yeye kujua kwa kufichwa ukweli wa maamuzi mengi yanayofanywa na watu wawili tuu katika Chuo hicho.
Tunalidhalilisha mno jina la baba wa Taifa, vitu kibao viko sub~standard au viko kifisadifisadi halafu tunavipa jina la Nyerere .ni upumbavu hiyo sio njia sahihi ya kumuenzi
 
Acha tu wapige kazi maana hata wanaoenda pale nadhani hawalendi future ya maisha yao binafsi pale napachukulia kama mgahawa wa askari wanaofanya kazi pale kambi ya Navy kigamboni. Hakuna elimu pale.
 
Mwalimu Nyerere Memprial Academy-Kigamboni.

Taratibu jamaa yangu maana una hasira za longtime na hawa jamaa maana kuna kitu walikukwaza nini?
Maisha ni popote atapiga mzigo tu kwanimm kuna watu niliwaacha STD VII, wapo mbali hata wale wa F-IV na F-VI
HUU MPANGO WA SERIKALI WA KUWAFICHUA HAWA waliogushi utagota tu kwani kuna jamaa aliwataja kina Kamara, Lukuvi, Nagu kiko wapi na akadai wamkamate wote wakanywea na watu wanachovya bata
Memprial Memorial
 
Suala si kukwazwa ila uozo huu wa kughushi vyeti na udanganyifu katika elimu, kama wewe unakubaliana na hali ni wewe kwa kutokuwa na huruma kwa kizazi za baadaye kutokana na udanganyifu katika elimu sijui itakuwaje kwa maendeleo ya jamii.
Taratibu jamaa yangu maana una hasira za longtime na hawa jamaa maana kuna kitu walikukwaza nini?
Maisha ni popote atapiga mzigo tu kwanimm kuna watu niliwaacha STD VII, wapo mbali hata wale wa F-IV na F-VI
HUU MPANGO WA SERIKALI WA KUWAFICHUA HAWA waliogushi utagota tu kwani kuna jamaa aliwataja kina Kamara, Lukuvi, Nagu kiko wapi na akadai wamkamate wote wakanywea na watu wanachovya bata
Memprial Memorial
 
[h=2]Dk. John Magoti na mr. Lwambano mchunguzwe,mmekiua chuo cha kumbukumbu ya mwalimu Nyerere[/h]
WANAJANVI SALAM?

Namasikitiko makubwa juu ya chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere cha Kigamboni ambacho kwa ukweli mimi kama mtu wajirani na chuo hiki yanayotokea yananipa mashaka endapo katika serikali ya rais Kikwete kuna watu makini katika kusimamia elimu yetu.

Huyu mkuu wa chuo alishawahi kufungiwa mlango na watumishi miaka kazaa nyuma na akanusuriwa na mzee kingunge Ngiombare Mwiru.

Alistaafu akapewa miaka mitano akamaliza akapewa tena miaka miwili hadi feb 2014, sasa kunataarifa kuwa kaomba kujiuzuru haraka oct 2013 pamoja na Mkt wa bodi DK SALI A SALIM baada ya kuona moto unawake kila kona.

Moja; Magoti anatuhumiwa yeye na MR Lwambano kula zaidi ya Tsh milioni 300 za fedha ya gharama ya wanafunzi ya matibabu

Yani walichangisha pesa kinyume na agizo la serikali LA MWAKA 2008

Serikali iliagiza tangu mwaka 2008 kuwa mwanachuo au sekondari aliejiunga na bima ya afya Hatotozwa tena gharama ya matibabu na taasisi za umma na taasisi hizo zijiunge na bima ya matibabu

DK MAGOTI kwa njia za panya akaanzisha mchango wa matibabu wa shilingi laki moja kila mwaka kwa kila mwanazfunzi na kwa mwaka alichangisha zaidi ya milioni 150 kwa wanachuo waliokuwa takribani 1500,mchango huo ulidumu kwa muda waamiaka 3 hadi 2013 kutokana na kitumbua kuingia mchanga mara baada ya mwanachuo aliekuwa akisoma chuoni hapo kwa wakati huo ABUBAKAR ASENGA .D kuwasha moto wa kukataa kulipa gharama hizo na hatimae aliondolewa chuoni kwa kusimamishwa miezi 3 na kesi hadi sasa inaendelea ambapo chuo kimeshatumia zaidi ya milioni 10 kumlipa wakili wakuhakikisha mwanachuo huyo arudi chuoni hapo.

Magoti akaweka tangazo kuwa atarejesha pesa zote za wanachuo ambazo amezichangisha weye bima za matibabu ,jambo ambalo hajafanya hadi sasa, na wanachuo wengi wameshamaliza chuo na wako tangu miaka 3 nyuma, atarudishaje pesa hizi na hizi pesa zimetumikaje mana nasikia imebaki laki 6 tu?

Nani anazikagua? Wakati zahanati hapa chuoni inapewa ruzuku ya dawa na tabibu analipwa na serikali.
Hadi sasa wanachuo ambao hawana bima (na chuo hakitaki kuanzisha huduma hiyo chuoni) wanatakiwa kulipa shilingi laki moja kila mwaka, mwanachuo aumwe au asiumwe lazima aliepe na gharama hizo ni kwa zahanati ya chuo tu inayofungwa saa 10 jioni na tabibu ni huyo mmoja tu.

Mwanachuo akipewa rufaa ni kwa gharama zake,baaada ya malalamiko sasa Magoti kaamua eti mwakachuo akizidiwa zaidi atapelekwa Burhani hosp ambapo ameingia nao mkataba wa kifisadi pia.

Kila kitu huyu mzee anaamua mara baada ya kushauriwa na huyu bwana Lwambano ambae ndie anaonekana kumiliki utajiri wa Dk Magoti.

Kumbukeni huyu Lwambano ameajiriwa chuo cha Nyrere mara baada ya kufilisi kiwanda cha kahawa Moshi, na ameajiriwa akiwa na miaka 40 kinyume na taratibu za serikali.

Anafanya kazi zaidi ya tatu hapa chuoni,msajili,mhadhiri,msimam izi wa zabuni,msimamizi wa rasilimali watu na kadhalika.

Mara zote huyu bwana Magoti, alikpokuwa akiandikwa hapa mtandaoni na ufisadi wake alikuwa akitetewa na bwana mmoja anaejulikana kwa jina la Mabuba ambae ni memba wa sikunyingi humu ,na ni mfanyakazi hapa chuoni.
SASA MABUBA NAE YAMEMKUTA NA KAMA YUMO HUMU ASEME KWELI HAPA

Alikuwa afisa wa mitihani, akaamuriwa aweke somo la mtihani kwenye ratiba kinyuime cha taratibu kwa kuwa somo lilikuwa jipya na halikuwa kwenye mpangio wa mwaka, alikataa na siku ya mwisho, Magoti aliingia ofisini kwa Mabuba na kutunga mtihani,kuchukua karatasi za majibu na akaenda kwenye chumba cha wanachuo wanaotakiwa kufanya mtihani na kuwasimamia yeye mwenyewe kwa kuwa alitangaza somo hilo kuanza kufundishwa pasi na marekebisho ya kanuni wakati bwana Mabua alisema endapo somo hilo litafanyika basi atajiuzulu nafasi yake

Mabuba sasa AMEACHIA OFISI,ameelewa ukweli na uzalendo umemshinda akaamua kuachia nafasi na akaondolewa na kuteuliwa mtu mwingine ambae kwa kweli nikichekesho mana wanachuo imebidi wapate matokeo yao kwa njia ya kusoma kwenye matangazo kwenye ubao,,kwa kuwa hakuijua ofisi wala hakupewa semika ni kama kawaida ya Magoti ya kuhamka asubuhi na kusema wewe ndiwe utakuwa afisa mitihani na unakuwa.
NI DIKTETA MKUBWA.

Pole Mabuba, ukweli haupendi kupuuzwa puuzwa maana lazima udhihiri.

Tatu; WATUMISHI HAPA CHUONI SASA hawapati allowance yeyote ile ikidaiwa hakuna pesa na pesa zilienda kujenga nyumba ya kukaa wanafunzi katika tawi la chuo cha zanzibar kinyume cha taratibu.

Chuo hakina fedha chuo ambacho kilikuwa kinakaribia idadi ya wanachuo 2000 miaka miwili iliyopita sasa walioomba kujiunga na chuo hawafiki 200 na kunahati hata wasiwasili wote, sasa chuo hakifikishi jumla ya wanachuo 1000
WAZIRI MKUU PINDA NJOO KWA ZIARA YA GAFLA HAPA CHUONI AMURU UZUNGUMZE NA WAFANYA KAZI BILA MAGOTI NA MR LWAMBANO KUWAPO,,,,,TUKWAMBIE MAMBO ZAIDI YA YALE YA MWAKA JUZI ULIPOKUJA NA KUKUTA UFISADI ULIOKITHIRI CHUONI.

HAPA CHUONI kulikuwa na mkuu wa idara ya maktaba huyu bwana ni Mmasai hakutaka mchezo aliletewa orodha ya vitabu 5 vilivyonunuliwa kila kimoja shilingi laki saba wakati vinauzwa shilingi elfu arobaini kariakoo, akapandisha mori na kwenda kwa Magoti,alipofika akaambiwa alaa kumbe unakiherehere na wakubwa WA NCHI HII…..
basi utaisoma namba, huyu bwana Mmasai ana first class degree katika mambo ya maktaba na aliajiriwa akiwa na diploma mpaka sasa ajatambuliwa wala kupandishwa cheo, wenzake wanapanda tu yeye kila mwaka anaambiwa bajeti si ya Wamasai

Mkt wa bodi ya chuo hiki ni DK SALIM AHAMED SALIM, DK HUYU ANAMAJUKUMU MAZITO YANAYOMPA NAFASI MAGOTI KUFANYA ATAKACHO kwakuwa hakuna mtu wakaribu kumfatilia.

ALICHUKUA MAGARI YA SERIKALI KWENDA KUTOLEA POSA YA mwanae Musoma na kushiriki kwenye harusi Arusha KAFANYWA NINI?

Lwambano kila kukicha anachukua magari ya serikali chuoni na kwenda nayo Rufiji kwenye shamba lake,
LWA MBANO SASA ANAMILIKI MAFUSO ZAIDI YA 7,EXTRIAL GARI YA KUTEMBELEA NA JUZI AMENUNUA PRADO NEW MODEL AMEIPAKI CHUMBANI NYUMBANI ANAPOISHI NA AMEIJENGEA UKUTA akifanya mpango wakubadili hati kuandika jila la nduguye.

Kila mara anawalingishia wafanyakazi wenzake kuwa yeye amejijenga vya kutosha na yupo tayari kwa chochote.
Mambo ya Magoti yalimkuta pia aliekuwa makam mkuu wa chuo Mr Mushi na kukataa kuongezewa mkataba na badala yake kuwa mwalimu wa kawaida,siku ambayo Mushi alisema hivyo haraka bwana Magoti akamteua mtu wake ambae yeye hajui kusema hapana bali NDIYO TUU anaitwa Mr Lunyelele kuchukua nafasi kabla ya bodi kuamua.

Sasa Lwamabano anapesa kuliko chuo, Juzi ameikopesha SACCOS YA wafanyakazi wachuo na yeye ndie anatembea na makabrasha ya saccos.

BWANA MAGOTI SIKU AKIKUTANA NA WANACHUO KUZUNGUMZA NAO,HOTUBA ZAKE NI MAARUFU KWA KUANZA HIVI, “NDUGU WANACHUO KAMA KAWAIDA HAKUNA MASWALI H APA”,ANAHUTUBIA ANAONDOKA
NAULIZA HIVI DK MAGOTI AMEKINUNUA CHUO CHA MWALIMU NYERERE?
MAANA CHUO SASA KINAITWA CHUO CHA KUMSAHAU NYERERE

Alimuajiri shemejie amabe alisomea vyeti vya mtu akiwa na diploma na kumsomesha hadi Phd bwana MHAGAMA,kilipo waka likawekwa tangazo eti ameamua kuacha kazi kwa hiari.

Sasa hapa chuoni bwana Magoti amemuajiri ndugu yake anaeitwa Mr KIOI,huyu bwan pia ameajiriwa chuo cha DIT suala ambalo nikinyume cha taratibu za serikali kwa mtu kuwa na ajira mbili rasmi ndani ya taasisi za serikali,utashangaa wakati Magoti ni mkubwa ktk nchi hii anatishia kila mtu,

Tunalidhalilisha mno jina la baba wa Taifa, vitu kibao viko sub~standard au viko kifisadifisadi halafu tunavipa jina la Nyerere .ni upumbavu hiyo sio njia sahihi ya kumuenzi
 
[h=2]Uthibitisho wa tuhuma zilizopo chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere[/h]
Wana JF kumekuwa watu hususan Mkuu Uzalendi, Mpalamtoko na wengine juu ya tuhuma za chuo hicho, hapa naweka barua iliyoandikwa na bwana Mabuba kwenda kwa mkuu wa chuo. Kumbukeni ndugu huyu naye ni mtuhumiwa, amekuwa akituhumiwa kutoa vyeti feki. Nitajitahidi kuwaletea kila doc nitakayoipata.


Tuhuma hizi kama ni kweli, basi vyuo kazi ipo.​
paperclip.png
Attached Files
 
Back
Top Bottom