Utawala wa Majimbo ni kuipasua nchi vipande vipande

Utawala wa Majimbo ni kuipasua nchi vipande vipande

Desprospero

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2023
Posts
1,015
Reaction score
2,493
Chadema inahubiri kuwa endapo watashika dola (ndoto ya kawaida) basi wataanzisha utawala wa kimajimbo Ili kurahisisha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo. Ukiitazama mfumo huu na jinsi wanavyouelezea kwa haraka unaweza kudhani ni kweli.

Kama kuna jambo ambalo ukitaka ugomvi na Watanzania na uachwe kwenye mataa na uchukiwe kama ukoma au saratani basi njoo na sera yoyote ya kibaguzi iwe ni udini, rangi, ukabila, ukanda, jinsia nakadhalika.

Moja ya tunu adhimu wanayoienzi Watanzania ni Umoja wao, udugu wao, ushirikiano wao, ushirika wao. Hakuna zuri ndani utawala wa Majimbo zaidi ya kutugawa watu wa nchi moja. Utawala wa majimbo utafanya kuwepo na tofauti kubwa sana ya ulaji wa keki Taifa ndani ya kapu moja.

Sera hii inataka kila Jimbo lijikusanyie mapato yake binafsi na kutumia itakavyo na Salio (kiduchu) kupelekwa Serikali Kuu. Hii maana yake ni kwamba baadhi ya maeneo watakufa masikini na ushahidi tunaona katika ukusanyaji mapato Katiba baadhi ya H/Mashauri. Bila fedha kushushwa Toka kapu la Taifa hawawezi kujiendesha.

Vita na migogoro isiyoisha DRC ni matokeo ya mfumo huu. Ndani ya nchi moja lakini kutoka Jimbo moja kwenda linguine unakutana na "Beria" na unalipia Dola mia mfano utoke Arusha kwenda Tanga. Hii ndio sababu Tshekedi hawezi kuitawala Kongo maana hakuna Jeshi la nchi Bali majeshi ya majimbo. Huo ni mfano mmoja.

Watetezi wa hoja hii utolea mfano Marekani na Ujerumani lakini wanasahau umri wa nchi hizi katika utawala na demokrasia. Nchi changa kama hizi za Afrika zenye kujitawala chini ya miaka 60 bado zinatakiwa kukaa pamoja si kutengana.

Jambo la maana ni kuweka mfumo mzuri wa kuwafikia kila raia katika kupata huduma za lazima: kula, kuvaa na kulala.

Ni kutokomeza rushwa, ufisadi, upigaji, uhuni wa kimkakati nakadhalika. Raia kutendewa haki sawa kwa kila jambo. Lakini hakuna ushahidi wa kisayansi kuthibitisha kuwa utawala wa Majimbo ndio suluhisho la matatizo yetu. Tuwapinge, tuwakatae wanaotaka kututumbukiza kwenye vita ya kugombania rasilimali zetu. Tuwanunie.
#BringBackOurMoneyCAG
 
Chadema inahubiri kuwa endapo watashika dola (ndoto ya kawaida) basi wataanzisha utawala wa kimajimbo Ili kurahisisha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo. Ukiitazama mfumo huu na jinsi wanavyouelezea kwa haraka unaweza kudhani ni kweli.
Ni hawajaelewashwa tu maana ya federal government, watu wanatumua ukabila mgawanyiko kutishia wananchi wasio elewa, lakini ukweli federal government ndo suluhisho ya maendeleo tz na kupunguza ufisadi na upendeleo.
 
Chadema inahubiri kuwa endapo watashika dola (ndoto ya kawaida) basi wataanzisha utawala wa kimajimbo Ili kurahisisha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo. Ukiitazama mfumo huu na jinsi wanavyouelezea kwa haraka unaweza kudhani ni kweli.

Kama kuna jambo ambalo ukitaka ugomvi na Watanzania na uachwe kwenye mataa na uchukiwe kama ukoma au saratani basi njoo na sera yoyote ya kibaguzi iwe ni udini, rangi, ukabila, ukanda, jinsia nakadhalika.

Moja ya tunu adhimu wanayoienzi Watanzania ni Umoja wao, udugu wao, ushirikiano wao, ushirika wao. Hakuna zuri ndani utawala wa Majimbo zaidi ya kutugawa watu wa nchi moja. Utawala wa majimbo utafanya kuwepo na tofauti kubwa sana ya ulaji wa keki Taifa ndani ya kapu moja.

Sera hii inataka kila Jimbo lijikusanyie mapato yake binafsi na kutumia itakavyo na Salio (kiduchu) kupelekwa Serikali Kuu. Hii maana yake ni kwamba baadhi ya maeneo watakufa masikini na ushahidi tunaona katika ukusanyaji mapato Katiba baadhi ya H/Mashauri. Bila fedha kushushwa Toka kapu la Taifa hawawezi kujiendesha.

Vita na migogoro isiyoisha DRC ni matokeo ya mfumo huu. Ndani ya nchi moja lakini kutoka Jimbo moja kwenda linguine unakutana na "Beria" na unalipia Dola mia mfano utoke Arusha kwenda Tanga. Hii ndio sababu Tshekedi hawezi kuitawala Kongo maana hakuna Jeshi la nchi Bali majeshi ya majimbo. Huo ni mfano mmoja.

Watetezi wa hoja hii utolea mfano Marekani na Ujerumani lakini wanasahau umri wa nchi hizi katika utawala na demokrasia. Nchi changa kama hizi za Afrika zenye kujitawala chini ya miaka 60 bado zinatakiwa kukaa pamoja si kutengana.

Jambo la maana ni kuweka mfumo mzuri wa kuwafikia kila raia katika kupata huduma za lazima: kula, kuvaa na kulala.

Ni kutokomeza rushwa, ufisadi, upigaji, uhuni wa kimkakati nakadhalika. Raia kutendewa haki sawa kwa kila jambo. Lakini hakuna ushahidi wa kisayansi kuthibitisha kuwa utawala wa Majimbo ndio suluhisho la matatizo yetu. Tuwapinge, tuwakatae wanaotaka kututumbukiza kwenye vita ya kugombania rasilimali zetu. Tuwanunie.
#BringBackOurMoneyCAG
mm ningefurahi sana kama mifano yako yote ungeitolea kwa majirani zetu kenya lkn huko marekani hao siyo saizi yetu.tufafanulie ukioainisha na nchi ya kenya.je huko nako jeshi linamilikiwa na nani?
 
mm ningefurahi sana kama mifano yako yote ungeitolea kwa majirani zetu kenya lkn huko marekani hao siyo saizi yetu.tufafanulie ukioainisha na nchi ya kenya.je huko nako jeshi linamilikiwa na nani?
Tofautisha utawala wa Majimbo na ugatuzi wa kiuongozi. Kenya wamefanya ugatuzi lakini pamoja na yote ndipo bado maisha ya Wakenya yameendelea kuwa magumu na Pengo kati ya malofa na mabwenyenye limezidi kupanuka.
 
Ni hawajaelewashwa tu maana ya federal government, watu wanatumua ukabila mgawanyiko kutishia wananchi wasio elewa, lakini ukweli federal government ndo suluhisho ya maendeleo tz na kupunguza ufisadi na upendeleo.
Kwa TZ federal Government haifai. Hakuna hoja ya msingi wala nini.
 
mm ningefurahi sana kama mifano yako yote ungeitolea kwa majirani zetu kenya lkn huko marekani hao siyo saizi yetu.tufafanulie ukioainisha na nchi ya kenya.je huko nako jeshi linamilikiwa na nani?
Kenya hapo Ugatuzi/devolution imewashinda
 
Tofautisha utawala wa Majimbo na ugatuzi wa kiuongozi. Kenya wamefanya ugatuzi lakini pamoja na yote ndipo bado maisha ya Wakenya yameendelea kuwa magumu na Pengo kati ya malofa na mabwenyenye limezidi kupanuka.

..Tanganyika mpaka mwaka 1962 ilikuwa na majimbo na hakukuwa na tatizo la ukabila.

..pia wakati wa majimbo hakukuwa na tatizo au sheria inayozuia mwananchi kuhama toka eneo moja kwenda eneo lingine.

..kuhusu UKABILA mikoa tuliyonayo sasa hivi pamoja na wilaya imegawa nchi kikabila. Ni nadra sana kukuta wilaya ina jamii ya kabila zaidi ya moja.

..ukirudi kwa Chadema wao wanapendekeza Tanganyika iwe na majimbo / kanda 8 na Zanzibar iwe na majimbo 2.

.Katika majimbo au kanda zinazopendekezwa na Chadema hakuna utengano wa kikabila. Hakuna jimbo au kanda isiyokuwa na rasilimali ardhi, watu, au maliasili, kiasi kwamba jimbo lishindwe kujiendesha.

..Kuhusu ukusanyaji wa KODI au mapato ktk mfumo wa majimbo kuna kodi za jimbo, na kodi za serikali kuu. Serikali kuu itakuwa na vyombo vyake ktk kila jimbo kukusanya kilicho chake. Kila jimbo nalo litakuwa na chombo chake kukusanya mapato yake.

..Hivi tunavyozungumza Zanzibar tayari ina chombo chake cha kukusanya kodi mahsusi kwa ajili ya Zanzibar, vilevile TRA chombo cha muungano inakusanya mapato ya serikali ya muungano Zanzibar.

..Mwisho, hoja ya ugatuzi wa madaraka ilikuwepo hata wakati wa Mwalimu NYERERE. Baba wa taifa alikuja na sera inaitwa MADARAKA MIKOANI na lengo lake lilikuwa ni kuipunguzia serikali kuu madaraka na kuyapeleka chini zaidi kwa wananchi.
 
Naunga mkono hoja, na matatizo yote iliyonayo TZ lakini kuna Aina ya Umoja flani hivi tulionao ambao ni very unic, ni ngumu sana kuukuta nchi nyingi kubwa kubwa.
 
Back
Top Bottom