Utekelezaji Diplomasia ya Uchumi kwa maslahi ya Taifa: Balozi Liberata Mulamula akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe

Utekelezaji Diplomasia ya Uchumi kwa maslahi ya Taifa: Balozi Liberata Mulamula akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe

Wazo Kuu

Senior Member
Joined
Oct 21, 2018
Posts
114
Reaction score
295
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Mauritius Balozi Prof. Emmanuel Mbennah na kusisitiza juu ya utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa maslahi ya Taifa

Mazungumzo ya viongozi hao yamelenga kusisitiza utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi pamoja na kuboresha mazingira ya utendaji kazi baina ya Wizara na Balozi za Tanzania ili kuweza kutumia fursa zilipo katika mataifa mbalimbali kunufaisha Taifa.

Vilevile, Waziri Mulamula amesisitiza uwajibikaji kwa balozi zote za Tanzania ili kuweza kufikia malengo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ukuzaji na utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Mauritius Balozi Prof. Emmanuel Mbennah katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Mauritius Balozi Prof. Emmanuel Mbennah yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ambaye pia anaiwakilisha Tanzania nchini Mauritius Balozi Prof. Emmanuel Mbennah

 
Back
Top Bottom