johnmashilatu
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 841
- 909
Mamlaka ya usimamizi wa usajili wa majini TASAC katika mkoa wa Mwanza, wameendelea kwa muda sasa kufanya jambo la hatari kwa maisha ya watu na mali zao kwa kushindwa kusimamia usafiri wa Majini katika ziwa Victoria.
Hivi karibuni zilitokea ajali mbli karibu na maeneo ya Kirumba jijini Mwanza ambapo watu walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa baada ya vyombo vya majini walivyokuwa wakisafiria kupata ajali katika Ziwa Victoria.
Kana kwamba hiyo haitoshi, mamlaka hiyo imeendelea kusuasua kuchukua hatua dhidi ya vyombo vinavyofanya safari kati ya Mwanza na Kamanga wilayani Sengerema ambapo maisha ya abiria na mali zao yamekuwa hatarni hata baada ya kufikishiwa tarifa za kuwepo kwa hali hiyo.
Imekuwa jambo la kawaida kwa siku za hivi karibuni ( jana ni mfano mwingine) kivuko cha Mkombozi kutoka Upande wa Kamanga kwenda Kirumba kilibeba abiria na mizigo ambapo magari yaliyokuwa katika kivuko hichp yalikuwa yakining'inia.
Hali ni hiyo pia katika kivuko "Geji" kinachofanya safari pia kati ya Mwanza na Kamanga ambako utaratibu wa kubeba abiria na mizigo hauzingatiwi.
Hivi karibuni zilitokea ajali mbli karibu na maeneo ya Kirumba jijini Mwanza ambapo watu walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa baada ya vyombo vya majini walivyokuwa wakisafiria kupata ajali katika Ziwa Victoria.
Kana kwamba hiyo haitoshi, mamlaka hiyo imeendelea kusuasua kuchukua hatua dhidi ya vyombo vinavyofanya safari kati ya Mwanza na Kamanga wilayani Sengerema ambapo maisha ya abiria na mali zao yamekuwa hatarni hata baada ya kufikishiwa tarifa za kuwepo kwa hali hiyo.
Imekuwa jambo la kawaida kwa siku za hivi karibuni ( jana ni mfano mwingine) kivuko cha Mkombozi kutoka Upande wa Kamanga kwenda Kirumba kilibeba abiria na mizigo ambapo magari yaliyokuwa katika kivuko hichp yalikuwa yakining'inia.
Hali ni hiyo pia katika kivuko "Geji" kinachofanya safari pia kati ya Mwanza na Kamanga ambako utaratibu wa kubeba abiria na mizigo hauzingatiwi.