Hongera kwa mawazo mazuri iko hivi gharama sio kubwa inategemea unaanza na production ya ukuwa gani nakushauri anza kidogo kutegemea na soko lako na pia kwakuwa unaanza kutengeneza itakusaidia kwenye improvement mana utakuta ulikosea kitu au ulizidisha materials simply unaweza anza na 50,000.
Materials ni:
Mafuta dumu la 20litre linauzwa 38,000, caustic utachukua ya kupimiwa interm of kg, blue kwa ajili ya kuipa sabuni rangi zile tunaweka kwenye mashati kipindi hicho wahenga hahhahhah zipo feki na og Ila utadadisi, perfume kwa ajili ya harufu kuna za aina tof. Mfano ya lemon ni we we tu hapo harufu isiyokera muhimu, then hydrometer vifaa unatakiwa uandae vifuatavyo jaba au beseni kubwa ya kukorogea na ubao wa kumwagia mkorogo I mean ujiuji hapa inabidi umtafute fundi seremala akudizainie kibao chenye vyumba vya bars kwa idadi yako unayotaka simple 80 to 100 bars inatosha kishkaji.
Udambwiudambi usisahau kachapa kako
Changamoto zipo sana sana soko sasa hivi watengenezaji ni wengi wakubwa kwa wadogo sabuni ni nyingi pia wapo wanaoagiza kigoma direct sababu kule materials ndo nyumbani hivyo bei imedrop na itadrop sana halo mbeleni wako wanaozalisha mzigo wa kujaza canter wengi tu sasa hivi bei maeneo mengi kwa dar ni Tsh. 25,000 kwa katon ya sabuni 20 wewe huko mnapouza 30 elfu ni wapi au kwa mangi dukani na tatizo LA soko ni pale unapozalisha mzigo mkubwa mfano wa kujaza canter so itakulazimu uuze jumla kwa watu wa jumla bei itakuwa chini so itaminya kafaida.
Halafu ujue sabuni za magadi hazitumiki kivile kama za kawaida kina white wash na ndugu yake jamaa matumizi yake ni local limited.
Changamoto nyingine wapo wanaoproduce feki wanaharibu soko hawa watu.
Muhimu ingia YouTube jifunze zaidi then ingia mzigoni tengeneza kwa ajili yako kwanza hata bar moja then angalia ubora na uimprove kabla hujaanza kuuzia watu maana kwenye mix unaweza zidisha au kupunguza vitu sabuni ikatoka zaidi ya jiwe,laini sana,iwe inaisha haraka na mwisho iwe inamuwasha mtu pindi atumiapo.
Mwisho, ujitahidi kwenye kutafuta masoko endelevu maana kuna watu walisarender kwenye hii ishu. Asante