Utetezi wa Sabaya: Ametanua uwanja, ana mengi ya kuyathibitisha. Porojo hazitatosha kumnasua!

Yeye alimtaja Magufuli kama mamlaka yake ya uteuzi

..nadhani amelenga kupata MSAMAHA WA RAISI baada ya kutumikia kifungo kwa muda mfupi.

..inawezekana operesheni anazozungumzia Sabaya zilikuwepo kweli, na yeye alishiriki, sasa vijana waliotumika namna hiyo huwa wanalindwa.

..ikiwa Sabaya atapatikana na hatia nadhani kuna watu ndani ya system ambao watampigania apate huruma ya msamaha wa Raisi.
 
Marehemu hawezi kujitetea, wajitetee waliokuwa wasaidizi wake amabao wapo hai na wapo madarakani.
 
Sabaya hajamtaja Philipo Mpango na Luoga kama wanafahamu operation ya Arusha! Aliwataja kuthibitisha kama operation za namna ile ambazo anafanya nje ya eneo lake lakiutawala sio ya kwanza kwani aliifanya pia Dar eneo la Chanika huku watu tajwa hapo juu wakiwa wanafahamu kuwa Sabaya kuna kazi anaifanya Chanika.

Kwaiyo yamkini Operation ya Arusha Luoga assijue ila Luoga hawezi kushangaa kuwa kuna operation nyingine Sabaya anaifanya eneo la Arusha cos alishafanyanae Dar.
 
Wewe ni Parody la Lumumba.
Sabaya hasafishiki.
 
Unaposema mamlaka yake ya uteuzi haipo una maanisha nini?

1. Sabaya aliteuliwa na Rais wa Selikari ya awamu ya tano ambayo iliingia madarakani kwa uchaguzi wa October 2020. Hakuna uchaguzi uliofanyika baada ya huo hivyo bado uteuzi wake ni halali.

2. Hata baada ya Rais Magufuli kufa uteuzi wa Sabaya haukutenguliwa na aliendelea kuwa mkuu wa wilaya na hawajawahi kufukuzwa/ kuachishwa kazi hivyo yuko sahii anaposema yeye bado ni mtumishi wa Selikari.

3. Rais aliyepo madarakani aliwahi kukiri hadharani kuwa yeye na mtangulizi wake ni kitu kimoja hivyo wanamuunganiko katika kila kitu ikiwemo na maamuzi yaliyowahi kufanyika huko nyuma.

4. Kikatiba Selikari Selikari ni taasisi na maamuzi yote hufanyika kwa mlengo wa Collective responsibility hivyo kwa mantiki hiyo kama Sabaya ana hatia maana yake Selikari yote inakuwa na hatia mpaka watakapo thibitisha pasipo shaka kwamba Sabaya hakutumwa na mamlaka ya uteuzi.

Nashauri DPP afute kesi ya Sabaya sababu ina public interest na inaweza kuhatarisha amani ya nchi na kuteteresha ofisi namba moja.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu unatia aibu na huruma. Umejifunza wapi kuwa utetezi hauhitaji ushahidi? Bure kabisa!
Kwahiyo Mahakama itamkuta na hatia kwakuwa ameshindwa kuthibitisha hoja zake, ha ha ha ha ha UDSM, kweli uchawi upo nimeamini!
 
Mr. Petro E. Mselewa hapa umeandika kama Mwanasheria kweli uliye huru.....

Asante sana, umeliweka jambo very clear kisheria. Hata hivyo mimi nina swali moja kwako...

Kwamba, suppose akaweza kuthibitisha maelezo yake kwa ushahidi utakaokubalika mahakamani....

Je, kuna sheria inayomlinda mtu baki kama Sabaya a mere District Commissioner asiye na kinga yoyote ya kisheria au kikatiba aliyetumwa na "mamlaka yake ya juu yenye kinga ya kisheria/kikatiba" kutenda uhalifu wa kijinai yeye mwenyewe personally...?
 
Wewe ndiyo huna akili, Sabaya hawezi kutumia defence ya Magufuli bila ushahidi wa maandishi. Mpango kujuwa uwapo wa operesheni siyo ruksa kwa Sabaya kufanya jinai. Amekiri kuwapo kwenye duka lililotajwa na amekiri kumkuta mtu anayedaiwa kupigwa na kunyang'anywa fedha.

HACHOMOKI
 
kwani kazi za kiintelijesia tena ukiwa umetumwa na mamlaka yako ya uteuzi tena taasisi ya urais zinahitaji kibali kutoka eneo linalopelelezwa? mwenye wajibu wa kutoa kibali si mh.rais mwenyewe? nani mwingine mwenye mamlaka ya kupinga agizo la mh.rais
 
Unazidi kunishangaza Kama kweli wewe ni mwanasheria aise tena upo UDSM.
nijibu hili swali, kwenye hii kesi Sabaya anatakiwa kuthibitisha Nini!?
Kwamba alichokisema mahakamani ni kweli na kweli tupu, siyo uongo.
 
Hakuna mkuu. Kikubwa ni yeye kuthibitisha aliagizwa na alitekeleza alivyoagizwa bila kutenda jinai
 
Hakuna mkuu. Kikubwa ni yeye kuthibitisha aliagizwa na alitekeleza alivyoagizwa bila kutenda jinai
Kama ndivyo ilivyo, wanasheria wake wanaomtetea wamefikiri nini hata kumwongoza mteja wao kujitetea katika namna hii..?

Je, ni kughafilika na kuona basi liwalo na liwe?

By the way, kuna hili pia;

Kwamba, inawezekana ni kweli alikuwa na agizo la kutenda "jukumu fulani maalumu" kama anavyodai, lakini ktk utekelezaji akatumia njia zake mbaya kutekeleza bila kujua kuwa hapo badae inaweza kugeuka kuwa jinai kwake...

Ni wazi kuwa huyu bwana hana akili wala maarifa ya uongozi...!!
 
Hapa ndio utaona logic ya ndg Kibatala kuhusu kuistaki taasisi maana kwa kesi Kama ya sabaya hiyo taasisi itaweza kuingilia mahakama
Madai ya Sabaya naweza kuyafananisha na tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu. Hivi wale waliompiga risasi TL wakifahamika na kufikishwa mahakamani, je wakijitetea kuwa walipata maagizo kutoka juu utetezi huo utawasaidia? Hapana hauwezi kuwasaidia.
 

 
Thanks Mkuu, I was about to ask the same question [emoji780]
Urais sio mtu Urais ni Taasisi

Sent from my TECNO KD7h using JamiiForums mobile app
Do you think kuna mtu aliyeko kwenye taasisi ya urais atakubali kwenda kukubali kuwa NI KWELI TAASISI HIYO ILIMTUMA SABAYA AKAFANYE ALIYO YAFANYA TENA MENGINE MBELE YA KAMERA? AKITOKEA MTU WA AINA HIYO BASI MAANA YAKE THEY DO NO DESERVE TO BE THERE.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…