Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, walioteuliwa ni kama ifuatavyo:
(1) Prof. Faustin Rweshabura Kamuzora ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTTAMIS. Prof. Kamuzora ni Katibu Tawala wa Mkoa Mstaafu, anachukua nafasi ya Bw. Casmir Kyuki ambaye amemaliza muda wake;
(ii) Prof. Joseph Andrew Kuzilwa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP). Prof. Kuzilwa ni Profesa Mstaafu, Chuo Kikuu cha Mzumbe; na
(iii) Prof. Ahmed Mohamed Ame ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) kwa kipindi cha pili.
Uteuzi huu umeanza tarehe 04 Agosti, 2024.
PIA SOMA
- Uteuzi Julai 31, 2024: Rais Samia aunda Tume ya Kutathmini na Kushauri kuhusu Masuala ya Kodi (Presidential Commission on Tax Reforms)
(1) Prof. Faustin Rweshabura Kamuzora ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Uwekezaji ya UTTAMIS. Prof. Kamuzora ni Katibu Tawala wa Mkoa Mstaafu, anachukua nafasi ya Bw. Casmir Kyuki ambaye amemaliza muda wake;
(ii) Prof. Joseph Andrew Kuzilwa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP). Prof. Kuzilwa ni Profesa Mstaafu, Chuo Kikuu cha Mzumbe; na
(iii) Prof. Ahmed Mohamed Ame ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) kwa kipindi cha pili.
Uteuzi huu umeanza tarehe 04 Agosti, 2024.
- Uteuzi Julai 31, 2024: Rais Samia aunda Tume ya Kutathmini na Kushauri kuhusu Masuala ya Kodi (Presidential Commission on Tax Reforms)