Uteuzi: Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma

Uteuzi: Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma

Aramun

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2023
Posts
461
Reaction score
2,213
20240604_195040.jpg
Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Prof. Abel Makubi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma

Prof. Makubi anachukua nafasi ya Dkt. Alphonce B. Chandika ambaye amemaliza muda wake

Kabla ya Uteuzi, Makubi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa na Ubongo, Muhimbili (MOI) Awali, amewahi kuwa Mganga Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu Wizara ya Afya

PIA SOMA
- Prof. Makubi afanya kikao cha kimkakati na Madaktari Bingwa/bobezi ndani ya MOI
 
1000025987.jpg

Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Prof. Abel Makubi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma

Prof. Makubi anachukua nafasi ya Dkt. Alphonce B. Chandika ambaye amemaliza muda wake

Kabla ya Uteuzi, Makubi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa na Ubongo, Muhimbili (MOI) Awali, amewahi kuwa Mganga Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu Wizara ya Afya

Pia Soma:
- Prof. Makubi afanya kikao cha kimkakati na Madaktari Bingwa/bobezi ndani ya MOI
 
Wasukuma wanaendelea kuula tu.

Hata hivyo ni wachapakazi sana
 
Huyu Jamaa nafikiri ndio Mkurugenzi pekee kufanya kazi zaidi ya Taasisi mbili za Afya alianza kuwa Mkurugenzi Bugando, akaja Kuwa Mganga Mkuu wa Serikali akaja kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya akaja kuwa Mkurugenzi MOI sasa anaenda kuwa Mkurugenzi BMH

Binafsi ni mtu mchapakazi sana sana aliibadili kwa kiasi kikubwa Bugando!!
 
Huyu Chandika kwanini asiendelee kama alifanya vizuri mbona yule wa Takwimu anaendelea hata kama amemaliza muda wake! Huwa inakuaje?
 
Huyu Jamaa nafikiri ndio Mkurugenzi pekee kufanya kazi zaidi ya Taasisi mbili za Afya alianza kuwa Mkurugenzi Bugando, akaja Kuwa Mganga Mkuu wa Serikali akaja kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya akaja kuwa Mkurugenzi MOI sasa anaenda kuwa Mkurugenzi BMH

Binafsi ni mtu mchapakazi sana sana aliibadili kwa kiasi kikubwa Bugando!!
Ila kama alikuwa MOI mmmh ajifunze kwa wenzake JKCI jinsi wanavyoendesha vizuri taasisi yao with very good services...but MOI mmmh
 
M
Ila kama alikuwa MOI mmmh ajifunze kwa wenzake JKCI jinsi wanavyoendesha vizuri taasisi yao with very good services...but MOI mmmh
MOI kakaa muda mfupi hajafikisha hata Mwaka nahisi, Japo alijitahidi somehow
 
Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Prof. Abel Makubi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma

Prof. Makubi anachukua nafasi ya Dkt. Alphonce B. Chandika ambaye amemaliza muda wake

Kabla ya Uteuzi, Makubi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa na Ubongo, Muhimbili (MOI) Awali, amewahi kuwa Mganga Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu Wizara ya Afya

PIA SOMA
- Prof. Makubi afanya kikao cha kimkakati na Madaktari Bingwa/bobezi ndani ya MOI
LEO WAFANYAKAZI MOI WAMLILIA NA KUMPONGEZA PROF. MAKUBI

Simanzi na pongezi zilitawala ndivyo unavyoweza kusema wakati wa hafla fupi ya Menejimeti na wafanyakazi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) walipoagana na aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wake Prof. Abel Makubi ambaye ameteuliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa ya Makao Makuu ya Nchi jijini Dodoma.

Katika hafla hiyo iliyofanyika leo Juni, 7, 2024 katika ukumbi wa MOI Mpya wajumbe wa Menejimenti kwa niaba ya wafanyakazi walishindwa kuzuia hisia zao za huzuni kwa uhamisho wa kiongozi wao ambaye ndani ya miezi 11 ya uongozi wake ameleta mabadiliko makubwa katika taasisi hiyo, hata hivyo hawakusita kumpongeza.

Mkurugenzi wa Upasuaji wa Mifupa Dkt. Antony Assey kwa niaba ya wafanyakazi amemshukuru Prof. Makubi kwa uongozi wake mahiri na kufanikisha mageuzi makubwa ndani ya kipindi cha miezi 11.

Kwa upande mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi TUGHE tawi la MOI, Privatus Masula amempongeza Prof. Makubi kwa kuboresha maslahi ya watumishi na kuongeza ari ya uwajibikaji na kutoa huduma bora kwa wateja.

Prof. Makubi ametumia fursa hiyo kuwashukuru wafanyakazi wa MOI kwa kuonesha ushirikiano na kufanikisha kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kwamba ni jukumu lao kuendeleza Ari hiyo.

“Binafsi naomba niwashukuru kwa kunipokea na kunikubali, Muendeleze mazuri hasahasa ubora wa huduma hilo ndiyo kipaumbele cha wizara na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan...ni jukumu lenu kuendeleza miradi tuliyoianzisha” amesema Prof. Makubi
 

Attachments

  • FB_IMG_1717780121788.jpg
    FB_IMG_1717780121788.jpg
    75.4 KB · Views: 14
Hivi inakuaje rais anateua kila kitu mpaka professionals kama mkurugenzi wa hospital.....
Katiba bovu.......fisiemu ni mzigo mzito sana kwa watanzania

Watu wanatakiwa waombe hizo nafasi utashanga kuona vichwa vya hatari vyenye uwezo

Sasa haya mambo ya kuteuana gizani kisisiemu sisiemu ndio maana taifa letu lipo nyuma sana

Kuna vijana wadogo wana ma-exposure ya hatari
 
Back
Top Bottom