UTEUZI: Rais Magufuli ateua Mkuu mpya wa Wilaya ya Nzega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hanang

UTEUZI: Rais Magufuli ateua Mkuu mpya wa Wilaya ya Nzega na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hanang

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
LEO Julai 9, 2020 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amemteua Kamanda wa Kikosi cha Polisi TAZARA, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advera John Bulimba kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nzega mkoani Tabora kuchukua nafasi ya Godfrey William Ngupula.

Mbali na uteuzi wa ACP Bulimba, Rais Magufuli pia amemteua Solomon Isack Shati kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang mkoani Manayara, ambapo kabla ya uteuzi huo Bw. Shati alikuwa Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe mkoani Katavi.

Wakati huo huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kept. George Mkuchika kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya uteuzi wa makatibu tawala wa wilaya mbili.

IMG-20200710-WA0000.jpg

Maendeleo hayana vyama!

Soma pia: Yupo wapi mwanamama Advera Senso/Bulimba?
 
Back
Top Bottom