Utitiri wa nafasi za kuteuliwa umefanya watu wengi kuwa wana CCM

Riskytaker

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2024
Posts
568
Reaction score
2,522
Kuna Watanzania ndani ya CCM wanaamini kwamba ipo siku watakula teuzi, au kwamba watoto na ndugu zao watapata nafasi hizo na hivyo kufaidika kwa kodi za wananchi.

Hali hii inaonyesha ujinga mwingi katika chama, ambapo vijana wengi wa UVCCM wamerundikana na hawana hamu ya mabadiliko.

Watu wanajipendekeza tu, lakini ukitazama kwa makini, hakuna kinachofanyika chenye maana. Tunahitaji vijana wenye mawazo mbadala na ujasiri wa kuleta mabadiliko halisi kwa ajili ya jamii.
 
Watu wengi wapo CCM sio kwasababu wanakipenda chama bali kwakuwa kuna fursa za ajira na pia hutosumbuliwa na mamlaka endapo utakuwa ni mfanyabiashara.
 
Me sisiemu naipenda toka moyoni
Samia kipenzi cha watanzania
Tunampenda bure kabisa
Tumejitoa si KWA kutaka kitu

+255762567111
Jina Lukazi mshamba
 
Ni kwel jaamaa yangu kala ajira juz tu hapa tulikua tunamuona kama chizi kutembea na manguo ya ccm.
 


Uteuzi ni adui wa Taifa hili.
Uteuzi unatuletea upendeleo
Uteuzi unatuletea Chawa.
Uteuzi unatuletea ufisadi kama ule wa sukari.
Uteuzi unatuletea watu wasio na sifa wala uadilifu.
Uteuzi unztuletea udini.
Uteuzi unatuletea Ukabila na ukanda.
Uteuzi unaua uzalendo kwa kujenga uchama.
Uteuzi unatuletea mauaji na utekaji .
Uteuzi unatujengea unafiki .
Uteuzi unajenga mtandao wa rushwa ya fedha na ngono.
Uteuzi unaua ndoa za watu.
Uteuzi unaimarisha ushoga na usagaji.
Uteuzi unaua ubunifu.
Uteuzi unaua Demokrasia.
Uteuzi qoumounyokou
 
Yaani wengi wana matumaini kuliko hata wachimba madini, cha kushangaza sasa WASALITI wa CHADEMA ndio wanapeta

Kuondoa hizi SARAKASI, ni KATIBA MPYA ifute nafasi ya uDC, Mkurugenzi ambaye ataomba kazi kwenye Halmashauri chini yq Usaili ulio wazi na wa haki, asimamie..Wakuu wa Mikoa wachaguliwe na Wananchi, nafac nyingi za CEO wa Makampuni/ mashirika ya Serikali zigombaniwe na kupitishwa na Bodi ya Wakurugenzi..period
 
wengi ni ccm fake ili wapate vyeo au wasibughudhiwe biashara zao
 
Akina Pasco mayala wako kwenye waiting list

Hii imezalisha uchawa

Tulishuhudia upuuzi wakati wa kura za maoni eti wagombea ,walifika zaidi ya 150

Yaani wagombea wanazidi wajumbe

Alafu mamlaka za nchi zinaona sawa tu.

Tangu ndugu yetu Pasco aangukie pua anaoshi kama Digi Digi hajiamini na haaminiki , tasluma yake yote tupa kule
 
Ilisemwa adui wa taifa hili ni ujinga, maradhi na umasikini lakini kwa sasa adui wa Taifa hili ni CCM
 
Petro Magoti DC wa Kisarawe, 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hata Askari au Mwanasheria akitaka kumshughulilia Mharifu anaangalia kwanza nature ya chama cha mharifu.

Baada ya hapo anajiulize je nikifanya hiki nitapata uteuzi?
 
Inasikitisha sana Siku hizi vijana waliomaliza form six wazisaka kadi za ccm ili wapate mikopo kirahisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…