Utitiri wa wanamuziki wa hovyo unawabania wenye vipaji vya kweli

Utitiri wa wanamuziki wa hovyo unawabania wenye vipaji vya kweli

Nsimbi

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2014
Posts
1,091
Reaction score
1,203
Wanajiita wanamuziki lakini mimi nasema ni wahuni na wababaishaji ambao wameivamia fani kwa mtindo wa zima moto.

Baadhi ya wanamuziki wanaojiita ni wa kizazi kipya ni janga kwa taifa kwa kuwa wanaiharibu jamii kwa nyimbo zao za ovyoovyo.

Wengi ni wachafuzi wakubwa wa lugha na ni tishio kwa malezi ya watoto wadogo. Ni rahisi kwa mtoto kuiga kuvaa mavazi ya ajabu kwa vile amemuona mwanamziki maarufu kwa luninga.

Mtoto wa kiume akimuona mwanamziki wa kiume kavaa gauni au kusuka nywele ni rahisi kudhani kuwa hiyo ni sawa.

Wengi ni mfano mbaya kabisa kwa watoto. Mambo yao mengi ya hovyo yanaigwa na watoto na ni vigumu kuwakataza.
Wengi hawana nyimbo zozote za maana zaidi ya bahati tu na waganga ndio inayowabeba.

Zile tetesi za ndumbanangai labda si uongo kwani nyimbo zao hazina viwango. Fate huwabeba hata wajinga kama domo!!!

Vijana siku hizi wamemudu kuwarubuni baadhi ya watu kupenda nyimbo zao zilizojaa utumbo wa taulo!!!?
Hawa vijana sasa fedha zinawalevya wameanza nyodo.

Mashabiki wanawavimbisha tu vichwa vijana hawa ni hovyo kuwafanya wadhani wanaimba nyimbo nzuri kumbe sivyo.

Watu kama Hamorapa ndio wanamuziki wa ovyo ninaoongelea. Sijui hata anaimba nini. Baadhi ya wananchi wanapenda nyimbo mbaya. Dogojanja anajitahidi kiasi ingawa hana jipya. Sister P anajiita mkongwe lakini nahisi analazimisha tu. Hana kipaji.

Kibonge mwepesi anaweza kuwa na kipaji sema bongofleva imekorogwa sana siku hizi. Sasa wanamuziki wenye vipaji wamezingirwa na wapuuzi kama mbegu nzuri zinavyozingirwa na miiba.

Yule Snura naye analazimisha tu. Hana kipaji cha muziki kabisa. Chura atachuja sana kwani nyimbo zake hazina ujumbe wala vina.
Barnaba ni mbabaishaji mkubwa. Analazimisha kazi asiyoiweza. Sioni nyimbo zozote za maana zaidi ya kuvaa kike na hivyo kupotosha watoto wetu.
Shishibabe anabananga sema ana bahati ya kupendwa. Yeye anadhani watu wanapenda nyimbo zake kumbe wanamuonea huruma!
Maua Sama naye kituko jumlisha rafiki yake Gigimoney. Hawa wanafinyanga maadili ya taifa na kuwa sumu kwa makuzi ya watoto. Basata imekuwa kama jibwa lisilo na meno!

Vanessa anaupenda musiki lakini musiki haumpendi yeye. Ulaghai tu unambeba lakini nyimbo zake hazina mashiko.

Mwasiti anajikongoja sema amezongwa na msitu wa wanamuziki vimeo.
Utitiri wa wanamuziki ganga njaa unafanya wenye vipaji kubaniwa.

Wengi wamevamia fani ya musiki kwa kukwepa kazi ngumu lakini za staha kama kilimo, useremala, uvuvi, uchimbaji madini nk. Wengine walikwepa ugumu wa shule.

Mtu yeyote anaweza kuimba lakini si kila mtu anaweza kuwa mwanamziki. Lazima uwe na kipaji. Huwezi kufoji kipaji.
Jamii iache kuwashobokea wana bongofleva wahuni.
 
Wanajiita wanamuziki lakini mimi nasema ni wahuni na wababaishaji ambao wameivamia fani kwa mtindo wa zima moto.

Baadhi ya wanamuziki wanaojiita ni wa kizazi kipya ni janga kwa taifa kwa kuwa wanaiharibu jamii kwa nyimbo zao za ovyoovyo.

Wengi ni wachafuzi wakubwa wa lugha na ni tishio kwa malezi ya watoto wadogo. Ni rahisi kwa mtoto kuiga kuvaa mavazi ya ajabu kwa vile amemuona mwanamziki maarufu kwa luninga.

Mtoto wa kiume akimuona mwanamziki wa kiume kavaa gauni au kusuka nywele ni rahisi kudhani kuwa hiyo ni sawa.

Mtu kama Diamond Platinum ni mfano mbaya kabisa kwa watoto. Mambo yake mengi ya ovyo yanaigwa na watoto na ni vigumu kuwakataza.
Hana nyimbo zozote za maana zaidi ya bahati tu inayombeba.

Zile tetesi za ndumbanangai labda si uongo kwani hana nyimbo zenye viwango. Fate huwabeba hata wajinga kama domo.

Amewapumbaza watu kupenda nyimbo zake zilizojaa utumbo wa taulo?
Huyu kijana sasa fedha zinamlevya ameanza nyodo.

Hata Ali Kiba hana la maana. Mashabiki wanawavimbisha tu vichwa vijana hawa ni hivyo kuwafanya wadhani wanaimba nyimbo nzuri kumbe sivyo.

Watu kama Hamorapa ndio wanamuziki wa ovyo ninaoongelea. Sijui hata anaimba nini. Baadhi ya wananchi wanapenda nyimbo mbaya. Dogojanja anajitahidi kiasi ingawa hana jipya. Sister P anajiita mkongwe lakini nahisi analazimisha tu. Hana kipaji.

Kibonge mwepesi anaweza kuwa na kipaji sema bongofleva imekorogwa sana siku hizi. Sasa wanamuziki wenye vipaji wamezingirwa na wapuuzi kama mbegu nzuri zinavyozingirwa na miiba.

Yule Snura naye analazimisha tu. Hana kipaji cha muziki kabisa. Chura atachuja sana kwani nyimbo zake hazina ujumbe wala vina.
Barnaba ni mbabaishaji mkubwa. Analazimisha kazi asiyoiweza. Sioni nyimbo zozote za maana zaidi ya kuvaa kike na hivyo kupotosha watoto wetu.
Shishibabe anabananga sema ana bahati ya kupendwa. Yeye anadhani watu wanapenda nyimbo zake kumbe wanamuonea huruma!
Maua Sama naye kituko jumlisha rafiki yake Gigimoney. Hawa wanafinyanga maadili ya taifa na kuwa sumu kwa makuzi ya watoto. Basata imekuwa kama jibwa lisilo na meno!

Vanessa anaupenda musiki lakini musiki haumpendi yeye. Ulaghai tu unambeba lakini nyimbo zake hazina mashiko.

Mwasiti anajikongoja sema amezongwa na msitu wa wanamuziki vimeo.
Utitiri wa wanamuziki ganga njaa unafanya wenye vipaji kubaniwa.

Wengi wamevamia fani ya musiki kwa kukwepa kazi ngumu lakini za staha kama kilimo, useremala, uvuvi, uchimbaji madini nk. Wengine walikwepa ugumu wa shule.

Mtu yeyote anaweza kuimba lakini si kila mtu anaweza kuwa mwanamziki. Lazima uwe na kipaji. Huwezi kufoji kipaji.
Jamii iache kuwashobokea wana bongofleva wahuni.
Hapa umeongea ukweli mtupu ingawa kuna viazi hawatokuelewA
 
We mzee vipi? Nakushauri endelea kusingiliza nyimbo za Msondo Ngoma ya ukae ndio zinaendana na umri wako, huku kwingine tuachie wajukuu zako
 
kabla ya yote naomba ujue haohao wasanii wa ovyo wamewasahdia vijana weng kupata ajira ,we unadhihilisha chuki zako dhid yao,
je wasanii gan unaowajua wew ni wasanii wa kweli wamebaniwa ,
imekuwaje awa wahovyo wanahit kuliko hao wako wa kweli, toa thread kwa akil sio unakurupuka afu kusemea mafanikio ya jasho la wenzako sio poa
 
Wataje hao wa hovyo kama kweli unafanya hip hop
 
Secular music(wa kidunia) ni muziki wa kishetani..sasa wewe unataka waimbe nini zaidi ya kumsifia Lucifer mwanzilishi wa hiyo tasnia..Hello Hello Tanzania ya Linah Sanga ndio hit ya mwisho yenye akili
 
Kipindi anataka kukua kwanini hakupalilia shamba ili asiote kwenye miba!? Maana hata mbinguni si wote watakao ingia sembuse kwenye muziki!! Waambie tu wajipange kipindi wanataka kutoka wapalilie shamba ili wastawi vizuri..
 
Ulivyomtaja Maua sama ndio nikajua una stress ,kalale mziki hujui.
 
Back
Top Bottom