Utukutu wa Mario Balotelli, uliyajua haya kumi?

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906

1.Alitozwa Dola 400,000 (zaidi ya shilingi 700,000,000 ta kitanzania) kwa kwenda kwenye klabu ya uchi siku moja kabla ya mechi


2. Akiwa kwenye gari aina ya Bently, Januari mwaka 2012, Baloteli alisimama kwenye shule moja akiwa na marafiki zake, akatumia choo cha shule hiyo, kisha wakazunguka maeneo ya shule hiyo kwa dakika 20 na kuondoka.

3.akiwa na marafiki zake nyummbani wakirusha fataki za moto, Balotelli alitupa fataki moja bafuni na kuchoma bafu lake, askari wa zimamoto walikuja baadae na kuzima moto huo.

4. Akiwa Machester city, Kocha aliwahi kumtoa nje baada ya kukosa bao la wazi! Katika tukio hilo, Baloteli alibaki yeye na golikipa, na badala ya kufunga aligeuka na kuupiga kwa kisigino na kuutoa mpira huo. Kocha alimtoa nje dakika hiyohiyo.

5.Mtoto mdogo wa shule ya msingi alimwambia balotelli kuwa anaonewa sana shuleni, Balotelli alifunga safari na kwenda shuleni hapo ili kumpa moyo.


6.Alishawahi kumpa dola 1,000 ombaomba barabarani baada ya kushinda dola 25,000 kwenye kamali kwenye kasino moja mwaka 2011. Baada ya Kushinda fedha hizo, aliziweka kwenye kiti cha mbele cha gari yake huku akizunguka Mjini, askari walipomuuliza kwanini anaweka kiasi kikubwa cha pesa hadharani aliwajibu "Ni kwa kuwa naweza kufanya hivyo, hicho ndicho mnachotakiwa kujua"

7. Alikamatwa akiwa na ndugu yake, wakipita kwenye Gereza la wanawake nchini Italia mwaka 2010.

8.Alishawahi Kuiba Lenzi ya kamera ya Mwandishi wa Habari nchini Italia

9. Alipigwa Faini ya dola 100,0000 kwa kuwarushia wachezaji wenzake mishale ya Darts wakiwa mazoezini. alipouliza alijibu kuwa alikuwa na alikosa cha kufanya.

10. Alishawahi kushindwa kuvaa nguo ya mazoezi mpaka aliposaidiwa na Msaidizi wa klabu.

Chanzo: Blogs
 
Aliwahi kukojoa ktk glass na kuahidi kutoa dau nono kwa atakayekunywa mkojo huo,bila ajizi ndugu yake akaunywa na kuchukua mshiko huo!
 
Alisema atakaye muonyesha ubaguzi wa rangi atamshughulikia mwenyewe bila msaada wa polisi. wala chombo chochote cha dola...!
 
Alisha itwa na kocha Mourinho ofisini badala yake akaenda angalia mbio za magari.alipoulizwa baadae na kocha kwa nini hukuja akajibu,wee nakuona kila siku lakini haya mashindano ya magari ni mara moja kwa mwaka.Mourinho akabaki kucheka tu.
 
Mkuu hiyo ya dola 400,000 unaweza kunipa ushahidi kiduchu, alipigwa faini na nani?
 
Akiwa na Mourinho kuna mechi moja straika wote walikua majeruhi,hadi half time Baloteri ana kadi ya njano,wakati wa mapumziko Mourinho alitumia dakika zote 13 kati ya 15 kumuambia kua chonde chonde sina mtu mwingine kwenye benchi angalia usipate kadi nyingine.Akajibu poa kocha.Basi kuanza kipindi cha pili dakika ya 3 tu si akacheza rafu mbaya na kupewa kadi ya pili na kutolewa.Mourinho ikabidi atikise kichwa tu.
 
Nilishawahi kumpiga ngumi ya mdomo pale alipokosa kufunga goli la wazi kwani alibaki na kipa tu lkn aliupiga mpira kwa kisigino na kuutoa nje, ile ngumi ilimpasua mdomo naye akalia kwa uchungu 'bandu mweeeeeh!' huyo ndo Super Mario bana!
 
Mwaka 2010 Super Mario baada ya kupokea tuzo ya kinda bora bara la ulaya mwenye umri chini ya miaka 21 [Golden Boy trophy] alitamka haya..

On Jack Wilshere... [mpinzani wake wa mwaka huo]
"What's his name? Wil...? No, I don't know him, but next time I play against him, I will keep a close eye on him and perhaps I can show him the Golden Boy trophy and remind him that I won it"

On previous winners... [like fabregas, rooney, van der vaart and messi]
"There's only one that is a little stronger than Me: Messi. All others are behind me."
 
Ila anakoelekea sasa hv! Time will tell
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…