Jumapili usiku wa sa mbili hivi nilikwenda Stand Kuu ya mabasi yaendayo na yatokayo mikoani na nje ya nchi pale Ubungo ili kumpokea mjomba wangu aliyekua anatokea Tabora. Nilipofika pale nikampigia simu akanambia wapo Kibamba
Kwakua nilikua nahisi uchovu na usingizi kwa mbaali, nikaamua kushuka garini nikatafute japo chai au kahawa nichangamke kidogo. Nilifika kwenye mgahawa mmoja uliokua unaendeshwa na wanawake watupu nikakaa kwenye meza moja na jamaa aliyekua amebeba begi lake mgongoni huku anakunywa maji
Muhudumu alinifata na baada ya kumuagiza aniletee chai akataka kuongea pia na yule jamaa tuliekaa nae meza moja. Hawakuelewana. Jamaa anaongea kiingereza tu tena kwa lafudhi niliyohisi ni ya ki Nigeria na dada yule pamoja na wenzake wote pale hawakumuelewa
Nikajaribu kutoa kamsaada kangu ka kiingereza cha chini ya mwembe kwa Ras Simba na yule bwana akaletewa chakula alichokua anakihitaji, na baada ya hapo tukawa tunapiga stori za hapa na pale. Aliniambia yeye ni raia wa Ghana na sio Nigeria kama nilivyokua nimedhania awali
Nilichogundua ni kwamba jamaa alikua ana mahesabu makali mno nadhani kutokana na budget na pia safari yake ilikua bado ndefu mana alikua anaenda Uganda kisha aelekee DRC. Kwa ukarimu wa Kitanzania nikaamua nimlipie bill ya chakula na kinywaji alichokunywa, na jamaa kwanza akashangaa na kisha alipoona namaanisha alinishukuru sana sana!
Baada ya dakika chache mjomba akanipigia kunambia kua ndio wanaingia Ubungo stand na mie ikabidi niagane na huyo rafiki yangu Mghana ili nisogee kwenye basi
Basi wakati tunapeana mikono kuagana jamaa akanishukuru tena na halafu akanambia ukarimu niliomfanyia utaukumbuka sana. Kisha kwa sauti ya chini akaniuliza wewe ni dini fulani?(akiitaja jina). Nilidhani lile swali halikua na maana nikalipotezea, lakini akaniuliza tena!
Nikamwambia I am a human being. Kwamba mimi ni binadamu na chochote nilichofanya kwake kama ni kizuri na kitafanya anithamini basi nimekifanya kutokana na ubinadamu wangu kwanza
Na kama nimefanya chochote chenye kasoro na yeye akanidharau kwa kosa hilo basi ajue nimefanya hivyo kwa kasoro zangu kama binaadamu na wala sikutumwa na imani yangu ya dini!
Nikamwambia wazungu wanatucheka sana watu weusi tunavyoumizana na hata kuuana kwa jina la dini huku tukiwa hatufati values zinazohubiriwa na hizo dini kama vile kusema ukweli na kuacha uongo, kuacha wizi na ufisadi na kutendeana haki
Jamaa aliona aibu sana kwa maneno yangu yale na tukawa tumeagana bila hata ya kupeana contacts.
Nadhani kuna shida sana kwenye hili la dini hasa kwetu sisi waafrika. Kwa jina la dini watu wanauana, wanadhulumiana na kutendena ukatiliwa kila aina
Kaka mkubwa umeshawahi kutambua umuhimu wa dini ?
Je ushawahi kujiuliza kielimu ni yapi malengo ya dini ?
Kaka unaposema wazungu wanawacheka,huu ni ujinga uliopea kabisa,inaonekana kwako wewe wazungu ndio kipimo cha ustaarabu na kuelimika,hali ya kuwa ukweli wa mambo ni kinyume ?
Na unaposema wazungu wana kucheka una maanisha wazungu gani na wanakucheka kwanini ?
Je unafikiri kila mwafrika ana yafanya hayo unayohisi kwayo wazungu wanawacheka ?
Hapa nakupa malengo ya dini japokuwa swali hili nimekuuliza hapo juu,na ninajua usingeweza kulijibu.
Malengo ya dini :
1. Dini imekuja kuilinda akili ya mtu
Hili ni miongoni mwa malengo ya dini,kuja kwake ni kuilinda akili ya binadamu isifisidike,yaani isiingiwe na uchafu na kuyakemea yote yapelekayo akili kuharibika,kama vile matumizi ya pombe,madawa ya kulevya na mfano wake.
2. Dini imekuja kulinda mali za mtu
Hili pia ni lengo la dini. Kuwepo kwa dini watu watajua kuchunga amana za watu,kuepuka dhuluma,kutafuta machumo ya halali,kuacha kula mali za mayatima na mfano wake.
3. Dini imekuja kulinda vizazi vys watu.
Hapa ndio maana unakuta dini inakemea sana uzinzi na mfano wake.
4. Dini imekuja kulinda na kichunga heshima ya mtu
Hapa dini imekuja kutufunza jinsi ya kuishi na wenzi wako,wapendwa wako na maadui zako na mfano wake.
5. Dini imekuja kututoa kutoka katika hali duni kiutendaji kwenda katika hali ya juu kiutendaji
Dini imekuja kurekebisha zile ada na desturi za kihayawani,ushirikina na ujings mwengine.
Narudi..........