Uungwana: Rejesha gharama za kufanikisha mkopo uliopatiwa na rafiki, ndugu au jamaa

Uungwana: Rejesha gharama za kufanikisha mkopo uliopatiwa na rafiki, ndugu au jamaa

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Salaam Wakuu,

Nataka nizungumzie tu chembe ya uungwana ambayo inaweza kuwa na manufaa makubwa maishani mwetu.

Ni vema kuonesha uungwana unapopatiwa mkopo wa fedha na ndugu, jamaa au rafiki. Uungwana wa kwanza ni kuhakikisha una dhamira ya kulipa pindi unapokopa, kisha kupambana juu chini kuhakikisha unalipa.

Uungwana wa pili ingawa ni muhimu sana ni kuzingatia gharama (kama zipo) zilizotumika wakati wa kukopeshwa. Si vema kujisahaulisha kwenye hili.

Mfano: Wewe Taini umemuomba Juma kiasi cha Tsh 50,000 kisha akakutumia kwa njia ya benki au mtandao wa simu. Juma ametozwa Tsh 2,000 kukutumia hicho kiasi, halafu wewe Taini unamrudishia Juma Tsh 50,000 kamili bila kujali kuwa alitumia gharama fulani kukusaidia ulipokuwa na shida.

Amini, huenda aliyekutendea wema asikuulize jambo lolote ila huwa ni kipimo cha uungwana. Wakati mwingine anaweza kupata uzito kukusaidia kwakuwa huwa unabaki na buku buku zake mara kibao.

Haya makato ni sehemu ya mkopo. Usijisahaulishe. Unless mna makubaliano ya namna fulani kwamba kufanya hivyo hakuathiri mahusiano, uaminifu na zaidi, heshima iliyopo kati yenu.

Je, wewe ni muungwana wakati wa kurejesha deni? Je, umewahi kumshushia heshima mtu aliyekosa uungwana wa namna hiyo?
 
Watu hawana ustaarabu siku hizi tujifunze kutokusaidia watu maana malipo yake ni wewe uliyetoa msaada kubaki na mawazo tu kwamba umemsaidia mtu muda wa kurudisha hafikirii kuwa kuna gharama za ziada zimetumika kumtumia pesa.

Mara nyingi huwa wao wanarudisha pesa bila hata ya kutolea sasa hiyo ni hasara kwa mtu aliyetoa msaada.
 
Kuna mtu juzi nikamtumia 50,000 aliyohitaji, nikaongeza na 3,000 niki-assume anaweza asiwe na hela ya kutoa na tozo ya Samia kwa wakati ule. Asirudishe 50 kamili!
 
Binafsi kukopesha nakaribia kuacha, wamebaki watu wachache tu nnaowamudu kuwakopesha. Mimi nimejiwekea kwamba ntakopesha mtu kiwango cha pesa ambacho hata kikipotea sitaathirika.

Sema mleta mada kitu unachosema watu wangekizingatia ni bonge la uungwana
 
Kuna mtu juzi nikamtumia 50,000 aliyohitaji, nikaongeza na 3,000 niki-assume anaweza asiwe na hela ya kutoa na tozo ya Samia kwa wakati ule. Asirudishe 50 kamili!
Imagine hasara unayopata ukiwakopesha watu watatu wa namna hiyo.
 
Binafsi kukopesha nakaribia kuacha, wamebaki watu wachache tu nnaowamudu kuwakopesha. Mimi nimejiwekea kwamba ntakopesha mtu kiwango cha pesa ambacho hata kikipotea sitaathirika.

Sema mleta mada kitu unachosema watu wangekizingatia ni bonge la uungwana
Kabisa, kabisa!
 
Watu hawana ustaarabu siku hizi tujifunze kutokusaidia watu maana malipo yake ni wewe uliyetoa msaada kubaki na mawazo tu kwamba umemsaidia mtu muda wa kurudisha hafikirii kuwa kuna gharama za ziada zimetumika kumtumia pesa.

Mara nyingi huwa wao wanarudisha pesa bila hata ya kutolea sasa hiyo ni hasara kwa mtu aliyetoa msaada.
Si jambo jema kabisa yani.
 
Bora hata akumbuke kurudisha hicho ulichomtumia. Wengine wanajisahaulisha kabisa...
Watu hawana ustaarabu siku hizi tujifunze kutokusaidia watu maana malipo yake ni wewe uliyetoa msaada kubaki na mawazo tu kwamba umemsaidia mtu muda wa kurudisha hafikirii kuwa kuna gharama za ziada zimetumika kumtumia pesa.

Mara nyingi huwa wao wanarudisha pesa bila hata ya kutolea sasa hiyo ni hasara kwa mtu aliyetoa msaada.
 
Kuna mtu juzi nikamtumia 50,000 aliyohitaji, nikaongeza na 3,000 niki-assume anaweza asiwe na hela ya kutoa na tozo ya Samia kwa wakati ule. Asirudishe 50 kamili!
Nakuhakikishia kabisa, atakutumia 50k cash 😂
 
Mtakuwa mmefanya vizuri sana, Lakini hakikisheni mmepokea malalamiko kwa watu zaidi ya watano tofauti.
 
Nilikuwa nalaumu wanaorusha watu pesa mpaka kipindi flani nikakopa laki na 50 halafu mambo yakayumba, nilimzungusha jamaa mpaka akatishia kwenda kwa mganga. kulipa deni sio kazi rahisi hasa kama umeshatataua shida.
 
Dhamira ya kulipa ina kuwepo lakini hali halisi ni matokeo ya kutolipa. Let say unaomba mkopo wa laki tatu, kama umeshindwa kupata laki tatu mpaka uombe mkopo kuurudisha ni changamoto. Inawezekana unawekeza kwenye biashara nayo inabuma, una korosho shambani ambazo Magufuli anazinunua kwa mkopo na hakulipi.
 
Back
Top Bottom