Zwangedaba
Member
- Feb 1, 2009
- 99
- 25
Kipindi cha miaka 1800 wakati wa ushindi wa Napoleon huko Misri ulifungua historia ya Misri kwa Wazungu. Wakati huo, mumian hawakupewa heshima waliyostahili kutoka kwa wasomi wa Ulaya na kwa kweli, mumiani waliweza kununuliwa kutoka kwa wachuuzi wa mitaani - WAMACHINGA (kama inavyoonekana kwenye picha) an kutumiwa kama tukio kuu la hafla na mikusanyiko ya kijamii iliyofanyika katika karne ya 18. Wasomi wa zama hiyo mara nyingi walishikilia "Hafla za kuwavua mumiani", ambavyo, kama jina linavyoelezea, lilikuwa na mada kuu ambayo Mumiani angevuliwa mbele watazamaji wenye majivuno, wakshangilia na kupiga kelele kwa wakati mmoja.
Mmachinga akiuza mumiani mtaani (Misri 1865)
Katika kipindi hicho, mabaki yaliyohifadhiwa vizuri ya Wamisri wa kale yalikuwa yakisagwa kama unga na kutumiwa kama dawa. Kutokana na umaarufu wa jambo hili, ilipelekea kuwapo kwa udanganyifu katika biashara hii ili kukidhi mahitaji, ambapo miili ya waombaji ilitengenezwa kama ile ya Wamisri wa kale waliotumbuliwa na kutunzwa.
Kutokana na Mapinduzi ya Viwanda, mumiani wengi wa Wamisri walitumiwa kwa madhumuni zaidi ya kibinadamu: idadi kubwa ya mumiani wa binadamu na wanyama walisagwa na kutumwa Uingereza na Ujerumani kwa ajili ya matumizi kama mbolea. Wengine walitumiwa kama kikolezo (pigment) cha rangi ya kahawia au waliondolewa nguo zao, ambazo baadaye zilipelekwa Marekani kwa ajili ya matumizi ya kutengeneza karatasi viwandani. Mwandishi Mark Twain aliripoti kwamba mumiani walikuwa wakitumika pia kama nishati ya kuendeshea treni huko Misri.
Mwishoni mwa karne ya kumi na tisa, mumiani waligeuka kuwa vitu vyenye thamani kayika maonyesho, na mumiani walinunuliwa kwa wing na matajiri wa Ulaya na Amerika kama alama ya utalii. Kwa wale ambao hawakuweza kumudu mumiani mzima, mabaki yaliyogawanyika - kama vile kichwa, mikono au miguu - yaliweza kununuliwa kwa kificha (black market) na kusafirishwa nyumbani kisiri.
Kwa hiyo, tamaa ya biashara ya mumiani kwa Ulaya ilikuwa kubwa, kwamba hata baada ya kuyapitia, kuyafukua na kuiba kwenye makaburi yote hakukuwa na mumiani wamisri wa kale wa kutosha kukidhi mahitaji. Na hivyo mumiani bandia walitenegenezwa kutoka maiti za wahalifu waliouawa, wazee, maskini na wale ambao walikufa kutokana na magonjwa ya ajabu, kwa kuwazika katika mchanga au kuwajaza miili yao na lami na kuwakausha juani.
rarehistoricalphotos.com
Mmachinga akiuza mumiani mtaani (Misri 1865)
Katika kipindi hicho, mabaki yaliyohifadhiwa vizuri ya Wamisri wa kale yalikuwa yakisagwa kama unga na kutumiwa kama dawa. Kutokana na umaarufu wa jambo hili, ilipelekea kuwapo kwa udanganyifu katika biashara hii ili kukidhi mahitaji, ambapo miili ya waombaji ilitengenezwa kama ile ya Wamisri wa kale waliotumbuliwa na kutunzwa.
Kutokana na Mapinduzi ya Viwanda, mumiani wengi wa Wamisri walitumiwa kwa madhumuni zaidi ya kibinadamu: idadi kubwa ya mumiani wa binadamu na wanyama walisagwa na kutumwa Uingereza na Ujerumani kwa ajili ya matumizi kama mbolea. Wengine walitumiwa kama kikolezo (pigment) cha rangi ya kahawia au waliondolewa nguo zao, ambazo baadaye zilipelekwa Marekani kwa ajili ya matumizi ya kutengeneza karatasi viwandani. Mwandishi Mark Twain aliripoti kwamba mumiani walikuwa wakitumika pia kama nishati ya kuendeshea treni huko Misri.
Mwishoni mwa karne ya kumi na tisa, mumiani waligeuka kuwa vitu vyenye thamani kayika maonyesho, na mumiani walinunuliwa kwa wing na matajiri wa Ulaya na Amerika kama alama ya utalii. Kwa wale ambao hawakuweza kumudu mumiani mzima, mabaki yaliyogawanyika - kama vile kichwa, mikono au miguu - yaliweza kununuliwa kwa kificha (black market) na kusafirishwa nyumbani kisiri.
Kwa hiyo, tamaa ya biashara ya mumiani kwa Ulaya ilikuwa kubwa, kwamba hata baada ya kuyapitia, kuyafukua na kuiba kwenye makaburi yote hakukuwa na mumiani wamisri wa kale wa kutosha kukidhi mahitaji. Na hivyo mumiani bandia walitenegenezwa kutoka maiti za wahalifu waliouawa, wazee, maskini na wale ambao walikufa kutokana na magonjwa ya ajabu, kwa kuwazika katika mchanga au kuwajaza miili yao na lami na kuwakausha juani.
Street vendor selling mummies in Egypt, 1865
So brisk was the trade in mummies to Europe that even after ransacking tombs there just were not enough ancient Egyptian bodies to meet the demand.