Uvaaji wa barakoa usigeuzwe kuwa fasheni

Uvaaji wa barakoa usigeuzwe kuwa fasheni

Peter Agostino

Senior Member
Joined
Sep 23, 2016
Posts
105
Reaction score
229
Mengi yamesemwa kuhusiana na hizi barakoa na hadi sasa hivi kuna baadhi ya watu hawajazielewa vizuri.

Kuna wanaodai zile za kutengenezwa mtaani hazifai kabisa lakini kuna kundi la watu wengine wanadai hata hivyo zinasaidia kuliko kuacha kabisa kuvaa.

Nilichokishuhudia leo kwa jirani yangu mmoja kwa kweli kimenisikitisha, Katoka na barakoa yake huko akatupita nje hata salamu akawa anatoa kwa shida alivyojifunga usoni na kuingia zake ndani.

Haukupita muda mrefu nikashangaa kumuona mwanawe mdogo wa miaka 4 akitoka na ile barakoa nje huku akiichezea. Si kama babake alijisahau hapana bali alimwambia mwenyewe, "Chukua mwanangu na wewe uchezee"

Vituko vingine ni pale utakapowaona watu wakijali zaidi uvaaji wa barakoa na kusahau njia zingine za kujikinga kama kunawa mikono na kukaa umbali wa mita moja.

Kwa mitindo kama hii ugojwa huu hatuwezi kuushinda, tujitahidi kuchanganya mbinu zote bila ya kudharau hata moja pale barakoa inaposaidia itumike lakini pale kukaa mbali kunaposaidia pia kutumike kikamilifu, kunawa mikono nk.
 
Wabongo tulivyo wabishi labda mpaka watu wachapwe bakora watakuwa serious.
 
Barakoa zinauzwa na machinga barabarani Kama njugu..barakoa zenyewe ukiangalia kitambaa kilichotumika unaweza lia
 
Peter acha uongo, kaingia ndani ulijuaje kama alimwambia mtoto akachezee? Riwaya yako ni nzuri ila iboreshe
 
Nimewaona vijana kadhaa wamevaa kisha wanazishusha kwa mikono zinashuka mpaka kidevuni kisha anazirudisha tena.

Mwingine anaoshusha chini anaendelea na shughuli zingine akijisikia anaivaa kwa kuipandisha tu. wengine tena wengi wameshona za vitambaa ambazo kwa kweli ni wanapoteza muda tu.

Labda kwa wanawake wanaovaa za kitambaa naweza sema zinawasaidia kuficha lips, wamesevu hela ya lips sababu hawajapaka lips.
 
Barakoa zinauzwa na machinga barabarani Kama njugu..barakoa zenyewe ukiangalia kitambaa kilichotumika unaweza lia
Nimeona barakoa zinauzwa sh mia nne.. zimetengenezwa na mifuko mbadala ile.. raia wanazivaa halafu tudogoo
 
Back
Top Bottom