UVCCM endesheni Harambee ya kuwachangia wafanyabiashara wa Karume waliopata hasara ya moto

UVCCM endesheni Harambee ya kuwachangia wafanyabiashara wa Karume waliopata hasara ya moto

Lady Mwali

Senior Member
Joined
Nov 15, 2018
Posts
147
Reaction score
333
Kutokana na hasara kubwa waliopata wafanyabiashara wa soko la Karume baada ya ajali ya moto ni busara na ubinadamu wa hali ya juu Umoja wa Vijana wa CCM ufanya harambee ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kuwapunguzia machungu wahanga hawa wa moto.

Najua UVCCM wanna ushawishi mkubwa kwa viongozi na matajiri wa nchi hii, hilo linawezekana madiwani, wabunge, wakuu wa mikoa na viongozi wengine waoneshe utu wa kuchangia wahanga hawa wa ajali ya moto.

Hata mama Samia aoneshe utu wake kwa kuchangia pesa akionesha njia kwa viongozi wengine hakuna ubishi wafanyabiashara wa soko hili wamepoteza mitaji yao yote ukizingatia walio wengi wana mikopo benki, wataishi vipi na familia zao?

Napenda kampeni hii ianze mara moja hii itaonesha jinsi gani CCM inajali wananchi na ni kipimo tosha cha kuonesha utu na ubinadamu.
 
Kutokana na hasara kubwa waliopata wafanyabiashara wa soko la Karume baada ya ajali ya moto ni busara na ubinadamu wa hali ya juu Umoja wa Vijana wa CCM ufanya harambee ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kuwapunguzia machungu wahanga hawa wa moto...
Hivi mlipomvunjia mbowe bilicanas na kuharibu miundo mbinu ya shamba lake kule moshi mlitegemea ataishi vipi na familia yake?
 
Kutokana na hasara kubwa waliopata wafanyabiashara wa soko la Karume baada ya ajali ya moto ni busara na ubinadamu wa hali ya juu Umoja wa Vijana wa CCM ufanya harambee ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kuwapunguzia machungu wahanga hawa wa moto...
Hawana ushawishi zaidi ya kutumia nguvu
 
Kutokana na hasara kubwa waliopata wafanyabiashara wa soko la Karume baada ya ajali ya moto ni busara na ubinadamu wa hali ya juu Umoja wa Vijana wa CCM ufanya harambee ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kuwapunguzia machungu wahanga hawa wa moto...
Ni unafiki wa kisiasa huu.

Wanatakiwa waainishe sera za kuwasaidia Watanzania wote wa kipato cha chini.
 
Hivi mlipomvunjia mbowe bilicanas na kuharibu miundo mbinu ya shamba lake kule moshi nlitegemea ataishi vipi na familia yake?
CCM ni mashetani aiseeee, hawakuangalia vijana walioajiriwa na Mbowe
 
Uvccm wako bize na kuwaza uteuzi ndiyo maana wamekuwa CHAWA Hadi Wanakela
 
Yaani waliochoma Soko waendeshe harambee ya kusaidia waliochomewa soko?!🐒🐒🐒

Natamani nikutukane ila kwa sababu wewe ni mwanamke inabidi nifunge tu mdomo wangu.
 
Uzuri ni kuwa machinga wanajua aliyewasababishia moto ni nani. Ndio maana wameomba wajenge vibanda vyao wenyewe.

Uwezi wapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa ya mirinda lazima washituke
Jana walianza kujenga ila vimebomolewa leo! Asbh waliemda kwa RC kumuuliza kulikon ila inaonesha Seeikali haitaki wajenge wenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio vijana wa ccm tu hata wa chadema act cuf nk kila atakae guswa.
 
Back
Top Bottom