#COVID19 Uviko-19 na chanjo zake

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
#SisiTanzania
#WeTanzania
28/Julai/2021.

UVIKO19 NA CHANJO ZAKE.

Habari yako mtanzania.
Unafahamu kuhusu UVIKO19 na chanjo zake?

UVIKO19 ni gonjwa lililoikumba Dunia nzima na kuiacha mdomo wazi mwishoni wa mwaka 2019 ikianzia mabara jirani na kuingia Afrika kwa kasi mwaka 2020.

Mpaka sasa vitovu vya tiba Duniani vinapambana kutafuta suluhu ya gonjwa la UVIKO19. Chanjo mbalimbali zimekuwa zikitengenezwa, hii yote ikiwa mikakati ya kupunguza maambukizi ya UVIKO19.

Serikali nyingi Duniani ikiwepo ya Tanzania zimekuwa na hofu ya kuanguka ki-uchumi pamoja na anguko la idadi ya wananchi wake. Hofu hii imepelekea machaguo tofauti ya namna ta kukabiliana na gonjwa hili la UVIKO19 na mitazamo juu ya chanjo zako.

Tanzania kwa imani ya Mungu tulivuka wimbi la kwanza na la pili la UVIKO19 kwa Kuchukua taadhari za kitabibu juu ya kuenenda na gonjwa hili. Tulipata madhara machache kulinganisha na makadirio yaliyotolewa na Taasisi ya Afya Duniani.

Hivi sasa ulimwengu umeingia kwenye wimbi la tatu la UVIKO19 lilonahofu zaidi kwa wengi hali tukisahau njia za kujikinga ni zilezile za wimbi la 1 na wimbi la 2.

SASA TUFANYE NINI WATANZANIA KATIKA WIMBI HILI LA TATU? NA CHANJO ZA UVIKO19?

Mosi, WaTanzania tupunguze hofu na tufate taadhari zilizowekwa na wataalamu wa afya: Tuepuke misongamano isiyo ya lazima, Tuvae barakoa kwa usalama wetu na ndugu zetu, Tunawe kwa maji safi na miminika na kadhalika.

Pili, chanjo za UVIKO19 ni hiari na sio lazima kwa mtanzania. Hii ina maana gani? Ungana nami kwenye uchambuzi huu mdogo.


Wengi mtahoji kwanini sio lazima? Na kama inatolewa kwanini serikali inawaacha huru wananchi wake juu ya chanjo hii ya Jensen & Jensen?

kila Mtanzania anapewa uhuru kikatiba. Uhuru ambao atautumia kwa kuzingatia havunji wala kuingilia uhuru wa mtu mwingine na hatochafua amani ya nchi.

Sasa tuendelee na hapa
Kila mtanzania yuko huru kikatiba kuchanja chanjo hii hizi za UVIKO19 bila kuingilia uhuru wa mtu mwingine, sambamba na kusema kuwa kila mtanzania huyo huru kutokuchanja chanjo hizi za UVIKO19 bila kuingilia uhuru wa mtu mwingine.

Tuendelee na hapa
Tanzania ni dola yenye watu wenye mitazamo mbalimbali katika nyanja za maisha. Serikali inahakikisha kumuhudumia kila mtanzania kwa haki ya kile anachopenda kuchagua ndio maana chanjo imewekwa hiari ili atakaechagua kunyoa na anyoe atakaechagua kusuka na asuke ila yote yakilenga kulinda wananchi na jamii nzima ya mtanzania bila ubaguzi ama uonevu wa maamuzi.

CHANJO NI HIARI.
USILAZIMISHWE.
USILAZIMISHE.
CHUKUA TAADHARI.


Jivunie Utanzania

Je wajua, serikali ya awamu ya sita imetoa mikopo kwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu ikiwa ni pamoja na waliokuwa wamekosa apo awali?

Je tuwashauri nini wasomi wanaohitimu vyuo na dhana ya maendeleo ya taifa?

#SisiTanzania
#WeTanzania

Jivunie Utanzania

 
Ni mimi tu ndo nimeshindwa kumaliza kusoma huu uzi? Hadi nimeshisi usingizi asubuhi hii.
 
Kuna jinsi ukianza kuandika, unafanya urefu wa andiko lako uonekane mapema aisee, hili andiko ni refu aisee.
 
Ikiwa ni lazima hakuna shida ila hiyo consent form ibadilishwe,Serikali ikubali kugharamia madhara yakitokea kwa aliyechanjwa,ikiwemo kumlipa fidia.

Maana unanilazimisha kunichanja wakati Mimi sitaki.
Nakama umeniletea chanjo kwa kunipenda na una nichanja bure,basi ubebe na zigo la madhara ya chanjo kwa upendo uleule.

Hata hivyo msihofu tuko magotini hatimaje wadudu watafubaa na kuwa mafua ya kupenga na kuendelea Kula kiazi,huku life likisonga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…