Uvimbe tumboni

EMMYGUY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
11,099
Reaction score
25,347
Habari Wakuu!

Nina ndugu yangu amekuwa akisumbuliwa na tatizo la uvimbe tumboni upande wa kushoto, ni mda mrefu sasa.

Tangu mwezi Novemba 2015 amekuwa akiumwa sana, na kuna siku alitapita damu mfululizo na kupelekea kwenda kuongezewa damu hospitalini.

Kwa sasa hali yake inaendelea na unafuu kidogo maana amekuwa akilalama tumbo kumuuma pamoja na kujaa kama gesi, pamoja na nguvu kumuishia japo dawa anatumia mpaka sasa.

Nahitaji ushauri wenu ili nimsaidie ndugu yangu.

Zangu shukrani natanguliza.
MziziMkavu pia karibu kwa mawazo yako.
 
Last edited by a moderator:
Habari yako ndugu?Pole kwa kuuguliwa na ndugu yako hujatuambia ana Uvimbe wa aina gani tumboni kwa jina la kitaalamu unaitwaje huo uvimbe? hujatuambia huyo ndugu yako ni Mwanamke au mwanamme? Ukihitaji Matibabu yangu unaweza kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 
Poleni sana. Mpeleke hospitali huenda akahitaji upasuaji ama kubadilishiwa dawa.
 
Aliambiwa Ini limepata hitilafu linavuja maji na kusababisha gesi pamoja na Bandama, ndiyo maelezo aliyonipa. Vile vile anakuwa anajisikia kichefu chefu na anaishia kutema mate.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…