Uvumilivu unanishinda jamani....

dada, ukiamua unaweza kumpeleka ustawi au mahakamani. ila kuna scenario moja nilishawahi kuiona, hii issue huwa inaleta ugomvi mkubwa sana kama mwanaume ana mke mwingine kiasi kwamba baba wa mtoto aliona kama yule mtoto ni kauzibe fulani, akafikia hatua ya kumuua yule mtoto, ili awe huru;ushirikina upo na issue kama hii nilishawahi kuiona. hivyo, kama hauna namna yeyote kabisa fuatilia, ila kama una means nyingine kumtunza uyo mtoto, achana na uyo mwanaume mpende mwanao usije kumkosa, kwasababu uyo baba yake kama anawatoto wengine na mke ujue hana uchungu sana na mtoto wako, hata mtoto wako akifa hawezi kuona uchungu zaidi ya kushukuru kama umekuwa ukimsumbua na kama mke wa ndani anamsumbua kuhusu uyo mtoto wako. ya nini umkose mwanao, uyo mtoto wako ndiye atakaye kusaidia wewe baadaye, pima halafu ukiona kuna usalama endelea, ila ukiona kuna walakini achana naye tunza mwanao mungu amekupa zawadi hiyo, la sivyo wanaume wengine huwa wanaweza kumtoa kafara ili kujikomboa na usumbufu. nimeshakutana na issue kama hizi tatu. moja walifikishana mahakamani, na mtoto alikufa kifo cha mashaka ajabu na baba hakushiriki hata msiba.
 
Jinsi ninavyowapenda wanangu, nashindwa kuielewa midume inayokataa kutunza watoto wao.

Binafsi nakushauri uanze na njia ya mazungumzo. Hapa ni muhimu kukataa sababu za kipuuzi kama kuwa na majukumu mengi. Ikishindikana hapo, jaribu kuchukua taratibu za kisheri, kwa kwenda ustawi wa jamii au mahakamani.

Siyo vizuri kuumia peke yako kwani ikitokea mtoto akafanikiwa unakuta jibaba linakenua meno na kuwatambia wengine. Bora baba naye ashiriki malezi ya mtoto kwa gharama yoyote ile!
 
Duh.... Hapo kwenye red ndipo hasa panaponitia wazimu... Yan hanisaidii kuela afu aje kumchukua!!!!!!

Usiogpe sheria zipo, fanya kuongea nae kwa utulivu umuelewe then fuata sheria uwaone ustawi coz maelewano yana umuhmu wake
 
ikifika umri wa baba kuamua kuja kumchukua mwanae,mahakama itaangalia childs welfare,pale panapomfaa mtoto,pia maoni ya mtoto yatazingatiwa,ila isikushtue kwanza,..mambo ya baadae hayo...fanya kamwa ulivyoambiwa,nenda ustawi wilaya unayoishi atoe matunzo,sio anakaa tu
 

Pole kwahilo dadaa ,na nahisi sitokuwa tofauti sana na wachangiaji wengine chanya+ ,nivizuri zaid baba nae achangie kumtunza mtoto kwani hata kama uwezo unao lakini akikupiga tafu basi hela ya ziada utafanya mambo mengine ya msingi binafs na mtoto,ila ungemwambia na kumtahadharisha kabla ya kwenda huko,kama hatowajibika wewe utafuata hatua za kisheria na kama bado atakuwa mkaidi basi mamii mbio ustawi wa jamii tatizo litakuwa solved.pole
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…