gfsonwin umenikumbusha kisa cha ndugu yangu mwaka 2010 mumewe alimletea watoto 2 amezaa na mwanamke mwingie masikini mdada alichanganyikiwa lakini mwisho wa siku akakubaliana na hali akaamua kuwalea watoto cha kushangaza mwaka huu mwanzoni mwanamke mwingine akamletea fujo nyumbani kwake huku akiwa na mtoto akidai wa mumewe......mdada amesema amevumilia sasa amechoka.........kuna mambo mengine unaweza kujifunza kuvumilia na kuna mengine yanashindakan au kufika kikomo na itakuwa sio kuvumilia tena bali kujiumiza.......
nivea soma ushuhuda wangu post #59. ndipo utakapojua nisemapo vumilia namaanisha nini.nimefika mwisho wa akili zangu nimemwachia mungu maisha na ndoa yangu ailinde mimi siwezi na anailinda kweli kweli ,things are sometimes inevitable only god can,thats why i love him
In any relationship, iwe ndoa, urafiki,familia, hata kufanya kazi pamoja uvumilivu una nafasi kubwa sana. Ndio maana hata baadhi ya familia wakigombana AMA kutofautiana ni matusi ambayo hata kwenye kamusi hayamo. Kuna coaligues hawana dog, kila kitu ni kusutana na kupaza sauti. Hata ndoa pia Kama ilivyo kwenye kazi na familia kunahitajika kiwango fulani cha uvumilivu. Ila kuna mambo yasiyohitaji kuvumilia Kama serial cheating na physical abuse. Hapo hata iweje, ni mwendo mdundo aisee.
mhh!! kwanza pole kwa jaribu hilo, hakika mie nisingestahimili.Post #59
ndugu yanu blackwoman soma post #59 ndipo utakapo jua namaanisha nini.
my dearest sister sasa huyo mama mdogo watu watasema alikuwa mjinga labda ama hana kazi ama elimu etc. mimi naomba nikupe ushuhuda kidogo tu wa kwangu binafsi na nisemapo nimepita namaanisha.
mume waliwah kununua gari zuri sana sikuwa kulipanda zaid ya kimada aitwae ANA. nakumbuka enzi hizo nikienda salun sinza anakuja na pikipiki ya mume wangu ananitukana matusi ya nguoni na kunidoboleshea wanayofanya na mr ndani ya gari. sikuwah kumjibu hata siku moja wala kulia nillisema silii.
haikuishia hapo nyumba tuliyojenga alijua atahamia yeye akaja kunipa mchambo mtakatifu nikiwa nasuka nywele saluni moja mitaa ya sinza, kurudi home mr ukimweleza anakwambia kabisa wewe kwanini ulienda kusuka huo si unamfuta mwenyewe, ngoja akuumize. hapo napo nilivumilia.
kibaya zaid nilichukulia kama changamoto sikushtaki kwa nani wala nani na niliua hisia za hasira manake natoka kabila moja hivi so sikupende watu wachukulie kama sababu, wala sikumchukulia Rb. nikiwa navumilia bado mr alisafiri aliporudi alishukia kwake na zawadi zote za ulaya nakumbuka sitasahau. na baada ya siku kama 5 ndipo wanakuja wote home usiku nikamkaribisha. waliingia wote ndani hadi kwa rum, sikufichi walilala nikalala na watoto.
asbh wanaamka wanakuta hadi chai na supu iko mezani, walihisi nimetia sumu but niliwahakikishia kwa kula pamoja nao na watoto na nikafuta meza nkawaualiza mchana watakula nini. mtoto wa mume wangu ndiye aliyeuliza baba huyu ni nani? yule mwanamke aliapotaka kujibu tu ikawa kama mume wangu kaumizwa akamwambia tena kwa ukali wewe kahaba toka ndani mwangu. Nilishtuka kama naimepigwa shoti ya umeme. Mr alikasirika sana akataka kumpiga lakini nilimtetea yule mwanamke ili asije akaumizwa. mimi na wanangu tulilia sana.
yule ANA alitolewa ndani kama mwizi kwa mateke akiwa amejifunga kitenge changu kiunoni. na hapo bado mume wangu alikuwa na mtoto wa mashtuzi ambaye nilimkuta na niko nae hadi leo.
mume wangu alishangaa sana moyo wangu jinsi ulivyo, uvumilivu na upendo wangu kwake ulimbadilisha ndio maana nimwambiapo King'asti kuwa uvumilivu humbadilisha hata shetani kuwa malaika ni kweli nimeshuhudia. leo hii nina miaka zaid ya 10 na naifurahia ndoa. naamini hakuna binti ambaye anaweza kupita hapa ila mimi nilichoangalia ni nataka nini kwenye maisha yangu? na je kwanini nitaabishe amani yangu?
haikuwa kazi rahisi kuvumilia ila ni Mungu tu alinivusha sikuwah kushtaki hata siku moja kwa mama wala ndgu wa pande zote mbili wala kwa shosti zaid ya Mungu. niliia hadi mto ukalowa machozi nilisali hadi kung'ata sura za biblia nakumbuka zab 16&17. hadi leo hii hiyo biblia inaalama za meno ambazo nilizitia miaka kama 7 hivi iliyopita.
nihitimishe kwa kumtia mama mwenzangu moyo kuwa Mungu anaweza yote usimweleze mtu sema na Mungu. halafu omba amani uone yani muujiza hutokea punde.
uvumilivu wa kweli unatokana na upendo wa kweli.uvumilivu wa kweli au wa kinafiki? kuna uvumilivu huku mtu anasema kwa chinichin au wa kutakatu kuonekana
mhh!! kwanza pole kwa jaribu hilo, hakika mie nisingestahimili.
naona kuwa upendo wako kwa mumeo ni mwingi na ukaamini ukilipa mabaya yake kwa kumtendea mema hatimaye atabadilika. nashukuru kwa hii post, ni watu wachache mno wangeweza kuchukua uamuzi wako kwenye hii situation. umeonesha love conquers all 😀. Mungu akuzidishie moyo huo
duh mpaka mchozi kwa kweli.........hata mama yangu mkubwa yaliyompata yanaelekea kufanana na yako...........mpaka alikuwa kichaa na sasa hivi anatumia dozi na kuhudhulia clinic ingawa anaendelea vizuri lakini muda mwingine anakuwa hajielewi.
Mungu ni mkubwa kwa kweli amemsaidia kwa kiasi kikubwa na sasa anaendelea vizuri na watoto wameshakuwa wakubwa wanaume wameoa na wanawake wanatarajiwa kuolewa hivi karibuni.
Daima tutayaweza yote katika yeye atutiaye nguvu.
my dearest sister sasa huyo mama mdogo watu watasema alikuwa mjinga labda ama hana kazi ama elimu etc. mimi naomba nikupe ushuhuda kidogo tu wa kwangu binafsi na nisemapo nimepita namaanisha.
mume waliwah kununua gari zuri sana sikuwa kulipanda zaid ya kimada aitwae ANA. nakumbuka enzi hizo nikienda salun sinza anakuja na pikipiki ya mume wangu ananitukana matusi ya nguoni na kunidoboleshea wanayofanya na mr ndani ya gari. sikuwah kumjibu hata siku moja wala kulia nillisema silii.
haikuishia hapo nyumba tuliyojenga alijua atahamia yeye akaja kunipa mchambo mtakatifu nikiwa nasuka nywele saluni moja mitaa ya sinza, kurudi home mr ukimweleza anakwambia kabisa wewe kwanini ulienda kusuka huo si unamfuta mwenyewe, ngoja akuumize. hapo napo nilivumilia.
kibaya zaid nilichukulia kama changamoto sikushtaki kwa nani wala nani na niliua hisia za hasira manake natoka kabila moja hivi so sikupende watu wachukulie kama sababu, wala sikumchukulia Rb. nikiwa navumilia bado mr alisafiri aliporudi alishukia kwake na zawadi zote za ulaya nakumbuka sitasahau. na baada ya siku kama 5 ndipo wanakuja wote home usiku nikamkaribisha. waliingia wote ndani hadi kwa rum, sikufichi walilala nikalala na watoto.
asbh wanaamka wanakuta hadi chai na supu iko mezani, walihisi nimetia sumu but niliwahakikishia kwa kula pamoja nao na watoto na nikafuta meza nkawaualiza mchana watakula nini. mtoto wa mume wangu ndiye aliyeuliza baba huyu ni nani? yule mwanamke aliapotaka kujibu tu ikawa kama mume wangu kaumizwa akamwambia tena kwa ukali wewe kahaba toka ndani mwangu. Nilishtuka kama naimepigwa shoti ya umeme. Mr alikasirika sana akataka kumpiga lakini nilimtetea yule mwanamke ili asije akaumizwa. mimi na wanangu tulilia sana.
yule ANA alitolewa ndani kama mwizi kwa mateke akiwa amejifunga kitenge changu kiunoni. na hapo bado mume wangu alikuwa na mtoto wa mashtuzi ambaye nilimkuta na niko nae hadi leo.
mume wangu alishangaa sana moyo wangu jinsi ulivyo, uvumilivu na upendo wangu kwake ulimbadilisha ndio maana nimwambiapo King'asti kuwa uvumilivu humbadilisha hata shetani kuwa malaika ni kweli nimeshuhudia. leo hii nina miaka zaid ya 10 na naifurahia ndoa. naamini hakuna binti ambaye anaweza kupita hapa ila mimi nilichoangalia ni nataka nini kwenye maisha yangu? na je kwanini nitaabishe amani yangu?
haikuwa kazi rahisi kuvumilia ila ni Mungu tu alinivusha sikuwah kushtaki hata siku moja kwa mama wala ndgu wa pande zote mbili wala kwa shosti zaid ya Mungu. niliia hadi mto ukalowa machozi nilisali hadi kung'ata sura za biblia nakumbuka zab 16&17. hadi leo hii hiyo biblia inaalama za meno ambazo nilizitia miaka kama 7 hivi iliyopita.
nihitimishe kwa kumtia mama mwenzangu moyo kuwa Mungu anaweza yote usimweleze mtu sema na Mungu. halafu omba amani uone yani muujiza hutokea punde.
nimesoma ndugu yangu nampa hongera mwanamke huyo.......... uvumilivu kwa macho/mawazo ya kibinadamu utabaki kuwa msamiati nithubutu kusema ni kwa nguvu za muumba wetu.
habari za ijumaa wana MMU.
Leo nimekuja na hii mada hapa iitwayo uvumilivu hasa katika maisha ya ndoa. Mara nyingi sana nimekuwa nikisema ndoa yahitaj uvumilivu lakin sidhani kama naeleweka ipasavyo juu ya hili neno.
wataalamu wa lugha watanisaidia kuidefine vizuri bali mimi naomba nieleze nguvu ya uvumilivu panapo mapenzi ya kweli.
Jamani kwanza naomba mnielewe kwamba kwenye mapenzi ya dhati uvumilivu hutangulia, na hii hutokana na ukweli kwamba upendo huvumilia. Panapo upendo ule usiosukumwa na mambo ya nje bali ule wenye msukumo wa ndani tu uvumilivu hutangulia na hii ni kwasababu kuu mbili nazo ni:-
1) uvumilivu huona mapungufu ya mwenza wako kama changamoto wala si kama chuki.
2)uvumilivu hauhesabu gharama za kazi,upendo,kujitolea ama hela.
kwasababu hizi mbili siku zote mimi huwa naishi kwa kuvumilia mbele upendo ukafuata nyuma. na hii ni kwasababu ninapenda kwa dhati na wala si kwababu ya msukumo wa vitu ama kitu.
naona niifupishie hapa nisiwachoshe kwa maneno mengi mkashindwa kudadavua. nakaribisha maswali na maelezo ya nyongeza.
Amen to that. ukiandika kitabu cha maisha yako utapata wateja, watu wengi hupata moyo wakifahamu mahasibu wanayoyapata yamepitiwa na watu wengine ambao wameyashinda. inatupatia ujasiri wa ziada wa kukabiliana na maisha yetu 😀ni
ma bro baine n kurt nimejikuta nalia sijui kwanini nimeyasema haya hapa yamenikumbusha mbali sana mimi na wanangu lakini pia nafurahi sana yamebaki historia sasa.
nashukuru sana sister binafsi nimejikumbusha those days nikaishia kulia palikuwa pagumu sana ndio maana huwaga nasema humu jamvini mara kwa mara makosa ya mume wewe jipe raha tu muda wote watu wanaona natania ni ukweli kabisa. ninaamini hata mama yako mkubwa kama angekuwa anajipa raha kwa kutoka na friends, asingepata msongo mkali kama huo.
nilijifunza kuvumilia kwa kukaa kimya na kushtaki kwa Mungu lakini sikujifungia ndani, nilikuwa natoka naenda kuburudika na marafiki pasi kuwaambia langu la ndani hadi Mungu aliponijibu.
kweli msongo wa mawazo ndo ulimpelekea uko...........hata mimi nilishasema daima ntatabasamu hata nikiudhiwa vipi ...............mana wewe unajipa presha wakati mwenzako anakula raha..........
hakimu sahihi wa hii kesi za ndoa ni Mungu pekee ila kuwajulisha mashost ni mwiko..............yakwangu moyoni atayajua Mungu.
umenikumbusha zaburi pale juu kiukweli uwa zinafariji na kueleza kila kitu........... zaburi ya 138 ni ya shukrani uwa napenda kuitumia hii kama sala yangu ya kushukuru kila siku.