SoC04 Uvuvi ni hazina ya ajira kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na Tanzania yote

SoC04 Uvuvi ni hazina ya ajira kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na Tanzania yote

Tanzania Tuitakayo competition threads

hauleibrahim

Senior Member
Joined
May 17, 2024
Posts
183
Reaction score
125
Uvuvi ni chanzo cha ajira pia ni chanzo Bora cha kitoweo kama ilivyo ufugaji hasa kwa hapa Tanzania.

Ili uvuvi ulete Tija na mtokeo ya kueleweka sana ndani ya taifa ni vizuri kama taifa likaanza kuingiza mikakati Bora kama ifuatavyo hasa Kwa wakazi wa Kanda ya ziwa hasa vijana wa maeneo hayo wasio na ajira.

1. Ziwepo semina za mara Kwa mara za mbinu za uvuvi wa kisasa na faida zake kiujumla.

2. Vipatikane vifaa vya kisasa iwe Kwa vijana wanao taka uvuvi kwa kukopeshwa ili waanze uvuvi huo wakiwa na utaalam huku pia wakiwa na vifaa vyenye tija katika uvuvi wao hapo baharini.

3. Iwepo mikopo itakayo wasaidia vijana waweze kupata pesa za kuanzia kununua vifaa Kwa wale ambao bado watakuwa hawaja ingia kwenye uvuvi na wanataka kuingia nap wafanye uvuvi mikopo iwe ya riba ya kuweza kuhimilika au kama ikishindika vitolewe vifaa vya mikopo.

4. Tuwe na makongamano ya mara Kwa mara mfano Kwa mwezi mara moja yawe ni makongamano ya wataalam wa uvuvi na wavuvi wenyewe kuboresha mbinu Bora za uvuvi na utunzaji mazingira ya uvuvi ili samaki waendelee kuwepo wengi miaka na miaka pia itasaidia kupata mbinu mbada na kuachana na mbinu za uvuvi wa kizamani usio na tija Kwa mvuvi.

5. Vitolewe vipeperushi vya kugawa mashule ya sec na vyuoni: Vipeperushi vihusu mbinu za uvuvi wa kisasa pamoja na utunzaji mazingira yaa bahari ili kuwatunza samaki Kwa wingi na wawepo Kwa miaka mingi baharini mbinu hii itasaidia kumuandaa mtu anae kukaa kuvua akiwa na utaaalama tayri wa awali tofauti na Sasa kila mtu anatumia ule uzoefu wa uvuvi wa miakaka ya mababu usio endana na teknolojia yetu.

6. Wawepo wataalam wa kutumia teknolojia wnao wapa utaalam wavuvi kujua samaki wnapatikana wapi Kwa muda nyakati ya kama kiangazi ama masika hii itaondoa Ile hali ya kuvua kimazoeaa bila kujua ulipo tega nyavu zako ni eneo sahihi au unabahtisha tu kuwapata hao samaki.

Serikali wakiboresha hayo itasaidia vijana kuvutiwa na kujikita katika uvivu na kupeleka kitoeo kama samaki kupatikana Kwa wingi na kuongeza Pato la taifa Kwa nchi

Mbinu za kisasa zinavutia vijana kujiajili kwenye usasa wenye matokeo Bora ya kupata ajira kwenye maziwa na bahari hasa Kwa ufanyaji uvuvi
 
Upvote 0
Serikali wakiboresha hayo itasaidia vijana kuvutiwa na kujikita katika uvivu na kupeleka kitoeo kama samaki kupatikana Kwa wingi na kuongeza Pato la taifa Kwa nchi
Sijui kwa nini neno uvuvi linaendana na neno uvivu 😆😆😆✔🏃

makongamano ya wataalam wa uvuvi na wavuvi wenyewe kuboresha mbinu Bora za uvuvi na utunzaji mazingira ya uvuvi ili samaki waendelee kuwepo wengi miaka na miaka pia itasaidia kupata mbinu mbada na kuachana na mbinu za uvuvi wa kizamani usio na tija Kwa mvuvi
Sawa mkuu
 
Back
Top Bottom