SoC02 Uwajibikaji wa sekta ya kilimo katika mfumuko wa bei na uchumi
Stories of Change - 2022 Competition

Daniel Levert

Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
16
Reaction score
7
UTANGULIZI

Kilimo ni dhana pana inayojumuisha uzalishaji wa mazao, ufugaji na uvuvi. Katika andiko hili nitaangazia kilimo kwa upande wa uzalishaji mazao.

Sekta ya kilimo ni sekta mama ya uchumi wa Tanzania. Huchochea maendeleo ya sekta zingine kama usafiri, viwanda na masoko. Mfumuko wa bei nchini unasababishwa na kuongezeka kwa uhitaji zaidi ya kiwango cha uzalishaji pamoja na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji mashambani. Tanzania ina idadi kubwa ya wakulima wadogo wadogo ambapo wengi wanashindwa kumudu ongezeko la gharama za mbolea, viwatilifu na usafiri. Ongezeko la gharama za uzalishaji, umbali wa masoko na ubovu wa miundombinu imepelekea wakulima kupunguza uzalishaji, wengi wanazalisha mazao kwa mahitaji ya chakula cha familia tu. Kiwango kidogo kinachopatikana huleta ushindani mkubwa katika masoko na kupelekea mfumuko wa bei.

Sekta ya kilimo huathiri sekta zingine hivyo mfumuko wa bei katika uzalishaji wa mazao hupelekea mfumuko wa bei katika sekta zingine na kupanda kwa gharama za maisha kwa ujumla.

UHALISIA MTAANI

Nilitembelea masoko mawili ya Singida mjini maarufu kwa uuzaji wa mazao ya nafaka ikiwemo mahindi, mchele, mihogo, mtama na viazi vitamu. Soko moja linaitwa soko mjinga na jingine soko la mahembe, nilifuatilia zao la mahindi kama mfano. Maelezo ya wafanyabiashara wanaonunua mazao toka kwa wakulima yalifanana. Mei 2021 wafanyabiashara hawa walinunua debe la mahindi kwa wakulima kwa 8,000/= Tshs ,septemba 2021 debe lilipanda hadi Tshs 10000. Mei 2022, wafanyabiashara hawa walinunua debe moja la mahindi kwa 10,000/= Tshs , hadi 1 Septemba 2022 walinunua debe kwa 16000-17000/=Tshs kutoka kwa wakulima kukiwa na makadirio ya ongezeko la bei kwa asilimia 40 ikifananishwa na mfumuko wa bei ya mwaka 2021. Bei hutegemewa kupanda zaidi kipindi cha masika ikikadiriwa kufika 150,000/=Tshs kwa gunia moja la mahindi 2022.

picha halisi sokoni
20220902_135756.jpg
20220915_122214.jpg

Hadi April 2022 serikali kupitia wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) ilifanikiwa kuhifadhi takribani tani 198,496.165 za chakula katika ghala za taifa (Nukuu kutoka bajeti ya kilimo mwaka wa fedha 2022/2023).

Bajeti inaonesha utoshelevu na usalama wa chakula na lishe nchini ilihali watanzania wengi wanashindwa kumudu kupata lishe bora kutokana na gharama za vyakula kupanda sana, mavuno duni na hali zao zinazidi kua duni.

MAPENDEKEZO

Serikali kupitia wizara ya kilimo izingatie na iimarishe uhusiano mzuri na kampuni binafsi ambazo zimepiga hatua kubwa katika kilimo binafsi mfano MeTL. Pia kuzingatia mchango wa asasi za kiraia zisizo za kiserikali zinazofikiwa na watanzania wengi mfano Jamii Forums na Twaweza katika kusambaza taarifa za dira na sayansi ya maendeleo ya kilimo . Hii itasaidia kuongeza njia za kutatua changamoto zinazokumba kilimo cha Tanzania na uchumi kwa ujumla.

Iundwe tume huru nje ya jukwaa la siasa. Tume huru nje ya mifumo ya siasa itasaidia katika kutekeleza majukumu ya nchi kwa ajili ya watanzania wote bila kujali msimamo wa kiongozi fulani wala itikadi ya chama fulani. Tume ipewe uhuru wa kuratibu majukwaa mbalimbali na majadiliano ya matumizi ya fedha ili kutoa mapendekezo serikalini kabla ya fedha kuelekezwa katika miradi mbalimbali. Tume iwe na wataalamu wa uchumi ili kusimamia bei elekezi ya mazao na bidhaa zake maana thamani halisi ya ukuaji wa fedha yetu katika soko la dunia haiendani na thamani halisi ya mfumuko wa bei

Serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi na teknolojia iyape kipaumbele masomo ya kutumia utashi wa binadamu kuanzia taaluma ya elimu msingi. Somo la kilimo lingewekwa katika mtaala ili kuongeza ushindani na ujuzi katika kilimo.

Kutoa elimu kwa wakulima katika njia rafiki zaidi kuhusu kilimo cha kisasa na mazingira kitakachowawezesha kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa inayoathiri ikolojia za asili na uzalishaji wa mazao. Serikali, makampuni na wadau mbalimbali wa kilimo wawatembelee wakulima mashambani na si katika majarida tu. Pia katika kukabiliana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji, serikali iongeze ruzuku kwa wakulima mashambani wenye uwezo mdogo wa kumudu gharama za viwatilifu, mbolea na mahitaji mengineyo.

Ni ngumu kufikia nchi ya maendeleo ya viwanda na masoko bila kufikia nchi ya maendeleo ya kilimo kwanza, mfano halisi ni mataifa mengi yanayoongoza kwa maendeleo ya viwanda duniani ndio yanaongoza kwa kilimo pia na uuzaji wa chakula duniani mfano China na Marekani. Miundombinu ya mashambani nchini Tanzania ni ya kiwango cha chini swala linaloendeleza ugumu wa uzalishaji na mfumuko wa gharama za uzalishaji. Miundombinu bora ingesogezwa karibu na maeneo ya uzalishaji malighafi.

Kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za kilimo. Seikali iwaamini vijana na kuwapa nafasi kuwasilisha programu zao za maendeleo na kuchangia maamuzi. Ikumbukwe vijana ni kundi linaloathiriwa na mabadiliko ya sasa lakini litaendelea kuathiriwa maana vijana ndio viongozi wa kesho hivyo wapewe nafasi.

Tanzania ina takribani hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo, kati ya hekta zote ni takribani hekta milioni 10.8 tu sawa na asilimia 24 ndizo zinazolimwa kwa mwaka(wizara ya kilimo,2017).

Serikali ingeongeza hekta zingine kwa ajili ya kuwapa vijana fursa maana imekua ni kilio kikubwa kwa vijana kukosa ajira huku wakiitwa wavivu kua mali ipo shambani hivyo wakajiajiri, mashamba ambayo wengi hawajui wanaanzia wapi kuyapata. Serikali ingefungua milango kwa kuwekeza katika kufungua mashamba mapya ili kuongeza wigo wa soko la ajira na uzalishaji kwa vijana. VIJANA TUKIWEZESHWA TUNAWEZA, TUFUNGULIENI MASHAMBA TUCHAPE KAZI.

images (12).jpeg

images (11).jpeg
picha kutoka mtandaoni

HITIMISHO
Kutokana na takwimu za shirika la chakula na kilimo duaniani(FAO) mwaka 2018 inaonyesha kufikia mwaka 2030 biashara ya chakula itakua juu zaidi kufikia dola za kimarekani trilioni 1. Kwa upande mmoja ni taarifa nzuri sana , kwa upande mwingine ni onyo, taarifa hii inaweza kua nzuri ama onyo kwa taifa husika kutokana na hatua itakazoamua kuchukua katika uzalishaji na usimamizi wa mazao kuelekea 2030.

Kilimo pekee hakiwezi kutokomeza umaskini na kukabiliana na mfumuko wa bei ila kinaweza kutumika kama nyenzo kuu ya kuunganisha sekta zingine ili kuleta uchumi thabiti. Natoa wito kwa wataalamu na wadau wote kutoka idara za sera na mipango, wizara ya kilimo, viongozi wa serikali kuu na watunga sheria wa nchi kufumbua macho kutizama mbali zaidi ili kufanya uaamuzi bora leo na kutoa mwongozo mzuri kwa ajili ya kesho ili ifikapo 2030 tuwe na utoshelevu unaoonekana wa mazao kwa chakula pamoja na biashara.
 
Upvote 10
kuna hilo swala la kuulizwa experience kila tunapoenda , inaumiza sana mtu ndo umetoka chuo lakini kila kampuni inataka experience mm naitoa wapi[emoji852]
ilo swala la kuongezwa hekta kwa ajili ya vijana lizingatiwe
 
kuna hilo swala la kuulizwa experience kila tunapoenda , inaumiza sana mtu ndo umetoka chuo lakini kila kampuni inataka experience mm naitoa wapi[emoji852]
ilo swala la kuongezwa hekta kwa ajili ya vijana lizingatiwe
ni kweli kaka, tuipe mipango ya awamu ya muda mrefu muda
 
Mm ninaona hali hii ya mifumuko ya bei za nafaka nchini inachangiwa pia na ulimaji wa mazoea na uhaba wa taarifa sahh kwa wakulima, Mwisho wa siku wakipata loss njia za kufidia loss n kuuza kwa bei ya juu. Taarifa za kitaalamu za ulimaji ,uvunaji na uhifadhi wa zao husika na hali ya kimasoko ni muhimu wakulima wawenazo.

Naona serikali kwa sasa swala la pembejeo za kilimo inalitazma kwa jicho la tatu kumekuwa na ushukaji wa bei za pembejeo hii n hatua nzuri , lakn swala la taarifa sahihi za utumiaji wa pembejeo hizi ndiko jidihada zinapaswa zipelekwe kwa sasa.


By the way ... nmekubali jitihada zako za kuandaa Nakala kama hii, kaz nzuri kjna
 
Mm ninaona hali hii ya mifumuko ya bei za nafaka nchini inachangiwa pia na ulimaji wa mazoea na uhaba wa taarifa sahh kwa wakulima, Mwisho wa siku wakipata loss njia za kufidia loss n kuuza kwa bei ya juu. Taarifa za kitaalamu za ulimaji ,uvunaji na uhifadhi wa zao husika na hali ya kimasoko ni muhimu wakulima wawenazo.

Naona serikali kwa sasa swala la pembejeo za kilimo inalitazma kwa jicho la tatu kumekuwa na ushukaji wa bei za pembejeo hii n hatua nzuri , lakn swala la taarifa sahihi za utumiaji wa pembejeo hizi ndiko jidihada zinapaswa zipelekwe kwa sasa.


By the way ... nmekubali jitihada zako za kuandaa Nakala kama hii, kaz nzuri kjna
shukrani mkuu
pia ulichosema ni kweli mkuu ndio maana inabidi iundwe tume huru, ambayo inaweza kusimamia mipango mikakati hata kama ni katika awamu ya muda mrefu katika kutoa elimu bora kwa wakulima ..usahihi wa taarfa za mabadiliko ya tabia nchi na namna ya kukabili ili kuleta kesho imara
hii itasaidia kupunguza kilimo cha mazoea kua sasa ni msimu wa mvua bhasi tuingie mashambani
 
kuna hilo swala la kuulizwa experience kila tunapoenda , inaumiza sana mtu ndo umetoka chuo lakini kila kampuni inataka experience mm naitoa wapi[emoji852]
ilo swala la kuongezwa hekta kwa ajili ya vijana lizingatiwe
pamoja kaka🙏
hongera kwa makala nzuri yenye kuleta maendeleo katika jamii yetu.hakika kura umepata
 
UTANGULIZI

Kilimo ni dhana pana inayojumuisha uzalishaji wa mazao, ufugaji wa wanyama na uvuvi wa samaki. Katika andiko hili nitaangazia kilimo kwa upande wa uzalishaji mazao.

Sekta ya kilimo ni sekta mama ya uchumi wa Tanzania. Huchochea maendeleo ya sekta zingine kama usafiri, viwanda na masoko. Mfumuko wa bei nchini unasababishwa na kuongezeka kwa uhitaji zaidi ya kiwango cha uzalishaji pamoja na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji mashambani. Tanzania ina idadi kubwa ya wakulima wadogo wadogo ambapo wengi wanashindwa kumudu ongezeko la gharama za mbolea, viwatilifu na usafiri. Ongezeko la gharama za uzalishaji, umbali wa masoko na ubovu wa miundombinu imepelekea wakulima kupunguza uzalishaji, wengi wanazalisha mazao kwa mahitaji ya chakula cha familia tu. Kiwango kidogo kinachopatikana huleta ushindani mkubwa katika masoko na kupelekea mfumuko wa bei.

Sekta ya kilimo huathiri sekta zingine hivyo mfumuko wa bei katika uzalishaji wa mazao hupelekea mfumuko wa bei katika sekta zingine na kupanda kwa gharama za maisha kwa ujumla.

UHALISIA MTAANI

Nilitembelea masoko mawili ya Singida mjini maarufu kwa uuzaji wa mazao ya nafaka ikiwemo mahindi, mchele, mihogo, mtama na viazi vitamu. Soko moja linaitwa soko mjinga na jingine soko la mahembe, nilifuatilia zao la mahindi kama mfano. Maelezo ya wafanyabiashara wanaonunua mazao toka kwa wakulima yalifanana. Mei 2021 wafanyabiashara hawa walinunua debe la mahindi kutoka kwa wakulima kwa 8,000/= Tshs , septemba 2021 debe lilipanda hadi Tshs 10000. Mei 2022, wafanyabiashara hawa walinunua debe moja la mahindi kwa 10,000/= Tshs , Septemba 2022 walinunua debe hilo kwa 16000-17000/=Tshs kutoka kwa wakulima kukiwa na makadirio ya ongezeko la bei kwa asilimia 40 ikifananishwa na mfumuko wa bei ya mwaka 2021. Bei hutegemewa kupanda zaidi kipindi cha masika ikikadiriwa kufika 150,000/=Tshs kwa gunia moja la mahindi 2022.

Hadi April 2022 serikali kupitia wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) ilifanikiwa kuhifadhi takribani tani 198,496.165 za chakula katika ghala za taifa (Nukuu kutoka bajeti ya kilimo mwaka wa fedha 2022/2023).

Bajeti inaonesha utoshelevu na usalama wa chakula na lishe nchini ilihali watanzania wengi wanashindwa kumudu kupata lishe bora kutokana na gharama za vyakula kupanda sana na hali zao zinazidi kua duni.

MAPENDEKEZO

Serikali kupitia wizara ya kilimo izingatie na iimarishe uhusiano mzuri na kampuni binafsi ambazo zimepiga hatua kubwa katika kilimo binafsi mfano MeTL. Pia kuzingatia mchango wa asasi za kiraia zisizo za kiserikali zinazofikiwa na watanzania wengi mfano Jamii Forums na Twaweza katika kusambaza taarifa za dira na sayansi ya maendeleo ya kilimo . Hii itasaidia kuongeza njia za kutatua changamoto zinazokumba kilimo cha Tanzania na uchumi kwa ujumla.

Iundwe tume huru nje ya jukwaa la siasa. Tume huru nje ya mifumo ya siasa itasaidia katika kutekeleza majukumu ya nchi kwa ajili ya watanzania wote bila kujali msimamo wa kiongozi fulani wala itikadi ya chama fulani. Tume ipewe uhuru wa kuratibu majukwaa mbalimbali na majadiliano ya matumizi ya fedha ili kutoa mapendekezo serikalini kabla ya fedha kuelekezwa katika miradi mbalimbali. Tume iwe na wataalamu wa uchumi ili kusimamia bei elekezi ya mazao na bidhaa zake maana thamani halisi ya ukuaji wa fedha yetu katika soko la dunia haiendani na thamani halisi ya mfumuko wa bei

Serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi na teknolojia iyape kipaumbele masomo ya kutumia utashi wa binadamu kuanzia taaluma ya elimu msingi. Somo la kilimo lingewekwa katika mtaala maana masomo haya huhitajika zaidi mtaani kuliko ujuzi wa masomo mengine ya kawaida.

Kutoa elimu kwa wakulima katika njia rafiki zaidi kuhusu kilimo cha kisasa na mazingira kitakachoweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa inayoathiri ikolojia za asili na uzalishaji wa mazao. Serikali, makampuni na wadau mbalimbali wa kilimo wawatembelee wakulima mashambani na si katika majarida tu. Pia katika kukabiliana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji, serikali iongeze ruzuku kwa wakulima mashambani wenye uwezo mdogo wa kumudu gharama za viwatilifu, mbolea na mahitaji mengineyo.

Ni ngumu kufikia nchi ya maendeleo ya viwanda na masoko bila kufikia nchi ya maendeleo ya kilimo kwanza, mfano halisi ni mataifa mengi yanayoongoza kwa maendeleo ya viwanda duniani ndio yanaongoza kwa kilimo pia na uuzaji wa chakula duniani mfano China na Marekani. Miundombinu ya mashambani nchini Tanzania ni ya kiwango cha chini swala linaloendeleza ugumu wa uzalishaji na mfumuko wa gharama za uzalishaji. Miundombinu bora ingesogezwa karibu na maeneo ya uzalishaji malighafi.

Kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za kilimo. Seikali iwaamini vijana na kuwapa nafasi kuwasilisha programu zao za maendeleo na kuchangia maamuzi. Ikumbukwe vijana ni kundi linaloathiriwa na mabadiliko ya sasa lakini litaendelea kuathiriwa maana vijana ndio viongozi wa kesho hivyo wapewe nafasi.

Tanzania ina takribani hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo, kati ya hekta zote ni takribani hekta milioni 10.8 tu sawa na asilimia 24 ndizo zinazolimwa kwa mwaka(wizara ya kilimo,2017).

Serikali ingeongeza hekta zingine kwa ajili ya kuwapa vijana fursa maana imekua ni kilio kikubwa kwa vijana kukosa ajira huku wakiitwa wavivu kua mali ipo shambani hivyo wakajiajiri, mashamba ambayo wengi hawajui wanaanzia wapi kuyapata. Serikali ingefungua milango kwa kuwekeza katika kufungua mashamba mapya ili kuongeza wigo wa soko la ajira na uzalishaji kwa vijana. VIJANA TUKIWEZESHWA TUNAWEZA, TUFUNGULIENI MASHAMBA TUCHAPE KAZI.

View attachment 2346488 View attachment 2346489 picha na mtandao

HITIMISHO
Kutokana na takwimu za shirika la chakula na kilimo duaniani(FAO) mwaka 2018 inaonyesha kufikia mwaka 2030 biashara ya chakula itakua juu zaidi kufikia dola za kimarekani trilioni 1. Kwa upande mmoja ni taarifa nzuri sana , kwa upande mwingine ni onyo, taarifa hii inaweza kua nzuri ama onyo kwa taifa husika kutokana na hatua itakazoamua kuchukua katika uzalishaji na usimamizi wa mazao kuelekea 2030.

Kilimo pekee hakiwezi kupunguza umaskini na kukabiliana na mfumuko wa bei ila kinaweza kutumika kama nyenzo kuu ya kuunganisha sekta zingine ili kuleta uchumi thabiti. Natoa wito kwa wataalamu na wadau wote kutoka idara za sera na mipango, wizara ya kilimo, viongozi wa serikali kuu na watunga sheria wa nchi kufumbua macho kutizama mbali zaidi ili kufanya uaamuzi bora leo na kutoa mwongozo mzuri kwa ajili ya kesho ili ifikapo 2030 tuwe wauzaji wakubwa wa chakula nje na si wanunuzi tu.
Sekta ya kilimo ni sekta mama nchini inayotegemewa kulisha wananchi wake na kukuza uchumi wa nchi,mjadala wa uwajibikaji wa sekta ya kilimo katika mfumuko wa bei za bidhaa masokoni na uchumi wa nchi unahitaji umakini na serenading yet na kwa watu wote. Nakupa hongera kaka kwa kupa mjadala huu nafasi ya kupewa mtazamo wa makini,na kutamani nakala hii kupewa zaidi ya kura.
 
Sekta ya kilimo ni sekta mama nchini inayotegemewa kulisha wananchi wake na kukuza uchumi wa nchi,mjadala wa uwajibikaji wa sekta ya kilimo katika mfumuko wa bei za bidhaa masokoni na uchumi wa nchi unahitaji umakini na serenading yet na kwa watu wote. Nakupa hongera kaka kwa kupa mjadala huu nafasi ya kupewa mtazamo wa makini,na kutamani nakala hii kupewa zaidi ya kura.
nashukuru mtaalamu wa kilimo mwenyewe🙏
 
Secta ya kilimo ni muhimuu sana kwa maisha ya kila siku ,licha ya kwamba inasaidia kutuzalishia chakula pia huchangia pato la serikali katika bajeti mbali mbali piah maendeleo ya sect nyingine Kama miundo mbinu , barabara na n.k ........... Ni muhimuu sana serikali kutoa elimu angalau kwa kila kaya wakawa na kashamba Cha kujizalishia chakula piah na kusaport wakulima wakubwa na wadogo wadg.....
Umenenaa mtu wangu one love kwa pamojaa tunaweza kufikisha ujumbe huu kwa wahusika iliwaone njia gan nzur ambazo zinaweza kutumika ili kufanikisha yote haya✊
 
Secta ya kilimo ni muhimuu sana kwa maisha ya kila siku ,licha ya kwamba inasaidia kutuzalishia chakula pia huchangia pato la serikali katika bajeti mbali mbali piah maendeleo ya sect nyingine Kama miundo mbinu , barabara na n.k ........... Ni muhimuu sana serikali kutoa elimu angalau kwa kila kaya wakawa na kashamba Cha kujizalishia chakula piah na kusaport wakulima wakubwa na wadogo wadg.....
Umenenaa mtu wangu one love kwa pamojaa tunaweza kufikisha ujumbe huu kwa wahusika iliwaone njia gan nzur ambazo zinaweza kutumika ili kufanikisha yote haya✊
asante kaka kwa mchango wako
pamoja sana🙏
 
UTANGULIZI

Kilimo ni dhana pana inayojumuisha uzalishaji wa mazao, ufugaji wa wanyama na uvuvi wa samaki. Katika andiko hili nitaangazia kilimo kwa upande wa uzalishaji mazao.

Sekta ya kilimo ni sekta mama ya uchumi wa Tanzania. Huchochea maendeleo ya sekta zingine kama usafiri, viwanda na masoko. Mfumuko wa bei nchini unasababishwa na kuongezeka kwa uhitaji zaidi ya kiwango cha uzalishaji pamoja na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji mashambani. Tanzania ina idadi kubwa ya wakulima wadogo wadogo ambapo wengi wanashindwa kumudu ongezeko la gharama za mbolea, viwatilifu na usafiri. Ongezeko la gharama za uzalishaji, umbali wa masoko na ubovu wa miundombinu imepelekea wakulima kupunguza uzalishaji, wengi wanazalisha mazao kwa mahitaji ya chakula cha familia tu. Kiwango kidogo kinachopatikana huleta ushindani mkubwa katika masoko na kupelekea mfumuko wa bei.

Sekta ya kilimo huathiri sekta zingine hivyo mfumuko wa bei katika uzalishaji wa mazao hupelekea mfumuko wa bei katika sekta zingine na kupanda kwa gharama za maisha kwa ujumla.

UHALISIA MTAANI

Nilitembelea masoko mawili ya Singida mjini maarufu kwa uuzaji wa mazao ya nafaka ikiwemo mahindi, mchele, mihogo, mtama na viazi vitamu. Soko moja linaitwa soko mjinga na jingine soko la mahembe, nilifuatilia zao la mahindi kama mfano. Maelezo ya wafanyabiashara wanaonunua mazao toka kwa wakulima yalifanana. Mei 2021 wafanyabiashara hawa walinunua debe la mahindi kutoka kwa wakulima kwa 8,000/= Tshs , septemba 2021 debe lilipanda hadi Tshs 10000. Mei 2022, wafanyabiashara hawa walinunua debe moja la mahindi kwa 10,000/= Tshs , Septemba 2022 walinunua debe hilo kwa 16000-17000/=Tshs kutoka kwa wakulima kukiwa na makadirio ya ongezeko la bei kwa asilimia 40 ikifananishwa na mfumuko wa bei ya mwaka 2021. Bei hutegemewa kupanda zaidi kipindi cha masika ikikadiriwa kufika 150,000/=Tshs kwa gunia moja la mahindi 2022.

picha halisi sokoni
View attachment 2348262
Hadi April 2022 serikali kupitia wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) ilifanikiwa kuhifadhi takribani tani 198,496.165 za chakula katika ghala za taifa (Nukuu kutoka bajeti ya kilimo mwaka wa fedha 2022/2023).

Bajeti inaonesha utoshelevu na usalama wa chakula na lishe nchini ilihali watanzania wengi wanashindwa kumudu kupata lishe bora kutokana na gharama za vyakula kupanda sana, mavuno na hali zao zinazidi kua duni.

MAPENDEKEZO

Serikali kupitia wizara ya kilimo izingatie na iimarishe uhusiano mzuri na kampuni binafsi ambazo zimepiga hatua kubwa katika kilimo binafsi mfano MeTL. Pia kuzingatia mchango wa asasi za kiraia zisizo za kiserikali zinazofikiwa na watanzania wengi mfano Jamii Forums na Twaweza katika kusambaza taarifa za dira na sayansi ya maendeleo ya kilimo . Hii itasaidia kuongeza njia za kutatua changamoto zinazokumba kilimo cha Tanzania na uchumi kwa ujumla.

Iundwe tume huru nje ya jukwaa la siasa. Tume huru nje ya mifumo ya siasa itasaidia katika kutekeleza majukumu ya nchi kwa ajili ya watanzania wote bila kujali msimamo wa kiongozi fulani wala itikadi ya chama fulani. Tume ipewe uhuru wa kuratibu majukwaa mbalimbali na majadiliano ya matumizi ya fedha ili kutoa mapendekezo serikalini kabla ya fedha kuelekezwa katika miradi mbalimbali. Tume iwe na wataalamu wa uchumi ili kusimamia bei elekezi ya mazao na bidhaa zake maana thamani halisi ya ukuaji wa fedha yetu katika soko la dunia haiendani na thamani halisi ya mfumuko wa bei

Serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi na teknolojia iyape kipaumbele masomo ya kutumia utashi wa binadamu kuanzia taaluma ya elimu msingi. Somo la kilimo lingewekwa katika mtaala maana masomo haya huhitajika zaidi mtaani kuliko ujuzi wa masomo mengine ya kawaida.

Kutoa elimu kwa wakulima katika njia rafiki zaidi kuhusu kilimo cha kisasa na mazingira kitakachoweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa inayoathiri ikolojia za asili na uzalishaji wa mazao. Serikali, makampuni na wadau mbalimbali wa kilimo wawatembelee wakulima mashambani na si katika majarida tu. Pia katika kukabiliana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji, serikali iongeze ruzuku kwa wakulima mashambani wenye uwezo mdogo wa kumudu gharama za viwatilifu, mbolea na mahitaji mengineyo.

Ni ngumu kufikia nchi ya maendeleo ya viwanda na masoko bila kufikia nchi ya maendeleo ya kilimo kwanza, mfano halisi ni mataifa mengi yanayoongoza kwa maendeleo ya viwanda duniani ndio yanaongoza kwa kilimo pia na uuzaji wa chakula duniani mfano China na Marekani. Miundombinu ya mashambani nchini Tanzania ni ya kiwango cha chini swala linaloendeleza ugumu wa uzalishaji na mfumuko wa gharama za uzalishaji. Miundombinu bora ingesogezwa karibu na maeneo ya uzalishaji malighafi.

Kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za kilimo. Seikali iwaamini vijana na kuwapa nafasi kuwasilisha programu zao za maendeleo na kuchangia maamuzi. Ikumbukwe vijana ni kundi linaloathiriwa na mabadiliko ya sasa lakini litaendelea kuathiriwa maana vijana ndio viongozi wa kesho hivyo wapewe nafasi.

Tanzania ina takribani hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo, kati ya hekta zote ni takribani hekta milioni 10.8 tu sawa na asilimia 24 ndizo zinazolimwa kwa mwaka(wizara ya kilimo,2017).

Serikali ingeongeza hekta zingine kwa ajili ya kuwapa vijana fursa maana imekua ni kilio kikubwa kwa vijana kukosa ajira huku wakiitwa wavivu kua mali ipo shambani hivyo wakajiajiri, mashamba ambayo wengi hawajui wanaanzia wapi kuyapata. Serikali ingefungua milango kwa kuwekeza katika kufungua mashamba mapya ili kuongeza wigo wa soko la ajira na uzalishaji kwa vijana. VIJANA TUKIWEZESHWA TUNAWEZA, TUFUNGULIENI MASHAMBA TUCHAPE KAZI.

View attachment 2346488
View attachment 2346489 picha za mtandao

HITIMISHO
Kutokana na takwimu za shirika la chakula na kilimo duaniani(FAO) mwaka 2018 inaonyesha kufikia mwaka 2030 biashara ya chakula itakua juu zaidi kufikia dola za kimarekani trilioni 1. Kwa upande mmoja ni taarifa nzuri sana , kwa upande mwingine ni onyo, taarifa hii inaweza kua nzuri ama onyo kwa taifa husika kutokana na hatua itakazoamua kuchukua katika uzalishaji na usimamizi wa mazao kuelekea 2030.

Kilimo pekee hakiwezi kupunguza umaskini na kukabiliana na mfumuko wa bei ila kinaweza kutumika kama nyenzo kuu ya kuunganisha sekta zingine ili kuleta uchumi thabiti. Natoa wito kwa wataalamu na wadau wote kutoka idara za sera na mipango, wizara ya kilimo, viongozi wa serikali kuu na watunga sheria wa nchi kufumbua macho kutizama mbali zaidi ili kufanya uaamuzi bora leo na kutoa mwongozo mzuri kwa ajili ya kesho ili ifikapo 2030 tuwe wauzaji wakubwa wa chakula nje na si wanunuzi tu.
hongera kwa andiko zuri mtaalamu wa kilimo
ila huoni pia mfumuko wa bei katika sekta zingine nyingi?
unahisi kilimo ndio kitaleta ahueni kwa wananchi?
 
hongera kwa andiko zuri mtaalamu wa kilimo
ila huoni pia mfumuko wa bei katika sekta zingine nyingi?
unahisi kilimo ndio kitaleta ahueni kwa wananchi?
nashukuru kwa mawazo na mchango wako chanya
tajibu kama ifuatavyo
rejea hitimisho katika andiko langu aya ya pili ' nimesema kua kilimo pekee hakiwezi kututoa katika umaskini lakini kinaweza kutumika kama nyenzo kuu ya kuunganisha sekta zingine zote katika vita dhidi ya umaskini na mfumuko wa bei, ukitembea sehemu nyingi utagundua kua vilio ya kupanda gharama za vitu ni kubwa lakini hakuna kilio kikubwa kama kupanda kwa gharama za chakula maana hili ni hitaji kuu kuliko mengine yote, kila mtu lazima apeleke mkono kinywani kila siku , hili ni la watanzania wote,
mfano, baadhi ya picha (screenshot) hapo chini inaonesha baadhi ya mchango wa wananchi katika makala yajamii forums kuhusu kushuka kwa bei za mafuta na kupanda kwa gharama za vyakula, serikali imetoa ruzuku ili kushusha gharama za mafuta, wananchi wanashukuru lakini bado tu swala la chakula wanaligusia kwa sababu mwananchi huyu akishindwa kutumia usafiri wake binafs kwa sababu ya bei ya mafuta basi atatumia usafiri wa umma, lakini je akishindwa kumudu gharama za lishe mbadala ni nini?, utagundua kua hili halina mbadala tofauti na kupatikana kwa chakula, mbadala wa chakula ni chakula tu hivyo sekta hii inahitaji uangalizi wa tofauti sana na wa lazima kwa kipindi hiki
asante
 

Attachments

  • 20220907_161035.jpg
    20220907_161035.jpg
    31.4 KB · Views: 5
  • 20220907_161058.jpg
    20220907_161058.jpg
    40.7 KB · Views: 6
  • 20220907_160951.jpg
    20220907_160951.jpg
    79.2 KB · Views: 7
  • 20220907_161018.jpg
    20220907_161018.jpg
    71.9 KB · Views: 6
UTANGULIZI

Kilimo ni dhana pana inayojumuisha uzalishaji wa mazao, ufugaji wa wanyama na uvuvi wa samaki. Katika andiko hili nitaangazia kilimo kwa upande wa uzalishaji mazao.

Sekta ya kilimo ni sekta mama ya uchumi wa Tanzania. Huchochea maendeleo ya sekta zingine kama usafiri, viwanda na masoko. Mfumuko wa bei nchini unasababishwa na kuongezeka kwa uhitaji zaidi ya kiwango cha uzalishaji pamoja na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji mashambani. Tanzania ina idadi kubwa ya wakulima wadogo wadogo ambapo wengi wanashindwa kumudu ongezeko la gharama za mbolea, viwatilifu na usafiri. Ongezeko la gharama za uzalishaji, umbali wa masoko na ubovu wa miundombinu imepelekea wakulima kupunguza uzalishaji, wengi wanazalisha mazao kwa mahitaji ya chakula cha familia tu. Kiwango kidogo kinachopatikana huleta ushindani mkubwa katika masoko na kupelekea mfumuko wa bei.

Sekta ya kilimo huathiri sekta zingine hivyo mfumuko wa bei katika uzalishaji wa mazao hupelekea mfumuko wa bei katika sekta zingine na kupanda kwa gharama za maisha kwa ujumla.

UHALISIA MTAANI

Nilitembelea masoko mawili ya Singida mjini maarufu kwa uuzaji wa mazao ya nafaka ikiwemo mahindi, mchele, mihogo, mtama na viazi vitamu. Soko moja linaitwa soko mjinga na jingine soko la mahembe, nilifuatilia zao la mahindi kama mfano. Maelezo ya wafanyabiashara wanaonunua mazao toka kwa wakulima yalifanana. Mei 2021 wafanyabiashara hawa walinunua debe la mahindi kutoka kwa wakulima kwa 8,000/= Tshs , septemba 2021 debe lilipanda hadi Tshs 10000. Mei 2022, wafanyabiashara hawa walinunua debe moja la mahindi kwa 10,000/= Tshs , Septemba 2022 walinunua debe hilo kwa 16000-17000/=Tshs kutoka kwa wakulima kukiwa na makadirio ya ongezeko la bei kwa asilimia 40 ikifananishwa na mfumuko wa bei ya mwaka 2021. Bei hutegemewa kupanda zaidi kipindi cha masika ikikadiriwa kufika 150,000/=Tshs kwa gunia moja la mahindi 2022.

picha halisi sokoni
View attachment 2348262
Hadi April 2022 serikali kupitia wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) ilifanikiwa kuhifadhi takribani tani 198,496.165 za chakula katika ghala za taifa (Nukuu kutoka bajeti ya kilimo mwaka wa fedha 2022/2023).

Bajeti inaonesha utoshelevu na usalama wa chakula na lishe nchini ilihali watanzania wengi wanashindwa kumudu kupata lishe bora kutokana na gharama za vyakula kupanda sana, mavuno na hali zao zinazidi kua duni.

MAPENDEKEZO

Serikali kupitia wizara ya kilimo izingatie na iimarishe uhusiano mzuri na kampuni binafsi ambazo zimepiga hatua kubwa katika kilimo binafsi mfano MeTL. Pia kuzingatia mchango wa asasi za kiraia zisizo za kiserikali zinazofikiwa na watanzania wengi mfano Jamii Forums na Twaweza katika kusambaza taarifa za dira na sayansi ya maendeleo ya kilimo . Hii itasaidia kuongeza njia za kutatua changamoto zinazokumba kilimo cha Tanzania na uchumi kwa ujumla.

Iundwe tume huru nje ya jukwaa la siasa. Tume huru nje ya mifumo ya siasa itasaidia katika kutekeleza majukumu ya nchi kwa ajili ya watanzania wote bila kujali msimamo wa kiongozi fulani wala itikadi ya chama fulani. Tume ipewe uhuru wa kuratibu majukwaa mbalimbali na majadiliano ya matumizi ya fedha ili kutoa mapendekezo serikalini kabla ya fedha kuelekezwa katika miradi mbalimbali. Tume iwe na wataalamu wa uchumi ili kusimamia bei elekezi ya mazao na bidhaa zake maana thamani halisi ya ukuaji wa fedha yetu katika soko la dunia haiendani na thamani halisi ya mfumuko wa bei

Serikali kupitia wizara ya elimu, sayansi na teknolojia iyape kipaumbele masomo ya kutumia utashi wa binadamu kuanzia taaluma ya elimu msingi. Somo la kilimo lingewekwa katika mtaala maana masomo haya huhitajika zaidi mtaani kuliko ujuzi wa masomo mengine ya kawaida.

Kutoa elimu kwa wakulima katika njia rafiki zaidi kuhusu kilimo cha kisasa na mazingira kitakachoweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na hali ya hewa inayoathiri ikolojia za asili na uzalishaji wa mazao. Serikali, makampuni na wadau mbalimbali wa kilimo wawatembelee wakulima mashambani na si katika majarida tu. Pia katika kukabiliana na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji, serikali iongeze ruzuku kwa wakulima mashambani wenye uwezo mdogo wa kumudu gharama za viwatilifu, mbolea na mahitaji mengineyo.

Ni ngumu kufikia nchi ya maendeleo ya viwanda na masoko bila kufikia nchi ya maendeleo ya kilimo kwanza, mfano halisi ni mataifa mengi yanayoongoza kwa maendeleo ya viwanda duniani ndio yanaongoza kwa kilimo pia na uuzaji wa chakula duniani mfano China na Marekani. Miundombinu ya mashambani nchini Tanzania ni ya kiwango cha chini swala linaloendeleza ugumu wa uzalishaji na mfumuko wa gharama za uzalishaji. Miundombinu bora ingesogezwa karibu na maeneo ya uzalishaji malighafi.

Kuongeza ushiriki wa vijana katika shughuli za kilimo. Seikali iwaamini vijana na kuwapa nafasi kuwasilisha programu zao za maendeleo na kuchangia maamuzi. Ikumbukwe vijana ni kundi linaloathiriwa na mabadiliko ya sasa lakini litaendelea kuathiriwa maana vijana ndio viongozi wa kesho hivyo wapewe nafasi.

Tanzania ina takribani hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo, kati ya hekta zote ni takribani hekta milioni 10.8 tu sawa na asilimia 24 ndizo zinazolimwa kwa mwaka(wizara ya kilimo,2017).

Serikali ingeongeza hekta zingine kwa ajili ya kuwapa vijana fursa maana imekua ni kilio kikubwa kwa vijana kukosa ajira huku wakiitwa wavivu kua mali ipo shambani hivyo wakajiajiri, mashamba ambayo wengi hawajui wanaanzia wapi kuyapata. Serikali ingefungua milango kwa kuwekeza katika kufungua mashamba mapya ili kuongeza wigo wa soko la ajira na uzalishaji kwa vijana. VIJANA TUKIWEZESHWA TUNAWEZA, TUFUNGULIENI MASHAMBA TUCHAPE KAZI.

View attachment 2346488
View attachment 2346489 picha za mtandao

HITIMISHO
Kutokana na takwimu za shirika la chakula na kilimo duaniani(FAO) mwaka 2018 inaonyesha kufikia mwaka 2030 biashara ya chakula itakua juu zaidi kufikia dola za kimarekani trilioni 1. Kwa upande mmoja ni taarifa nzuri sana , kwa upande mwingine ni onyo, taarifa hii inaweza kua nzuri ama onyo kwa taifa husika kutokana na hatua itakazoamua kuchukua katika uzalishaji na usimamizi wa mazao kuelekea 2030.

Kilimo pekee hakiwezi kupunguza umaskini na kukabiliana na mfumuko wa bei ila kinaweza kutumika kama nyenzo kuu ya kuunganisha sekta zingine ili kuleta uchumi thabiti. Natoa wito kwa wataalamu na wadau wote kutoka idara za sera na mipango, wizara ya kilimo, viongozi wa serikali kuu na watunga sheria wa nchi kufumbua macho kutizama mbali zaidi ili kufanya uaamuzi bora leo na kutoa mwongozo mzuri kwa ajili ya kesho ili ifikapo 2030 tuwe na utoshelevu unaoonekana wa mazao kwa chakula pamoja na biashara.
Mfumuko wa bei za bidhaa za kilimo unashusha sana Hali ya uchumi tupambane na hili swala tutafika salama
 
Back
Top Bottom