Uwanja wa Ndege wa Bujumbura wafunguliwa Burundi

Uwanja wa Ndege wa Bujumbura wafunguliwa Burundi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Uwanja wa ndege wa Bujumbura


Kuanzia siku ya Jumapili, Uwanja wa ndege wa Bujumbura umefunguliwa kwa ajili ya ndege zinazofanya safari kimataifa baada ya kufungwa kwa miezi saba kutokana na janga la virusi vya corona.

Burundi imekuwa nchi ya mwisho ya Afrika mashariki kufungua anga yake baada ya Tanzania mwezi May, Sudani Kusini mwezi Julai, Kenya na Rwanda mwezi Agosti na Uganda mwezi Septemba.

Mamlaka ya anga imesema, abiria watakaoingia watahitajika kuwasilisha cheti kinachoonesha majibu ya vipimo vilivyofanywa saa 72 zilizopita yanayoonesha kutokuwa na maambukizi ya virusi, kufanyiwa vipimo na kukaa karantini kwa saa 72, kwa gharama zao.

Melance Ndayisenga, mkazi wa jiji la Bujumbura, amefurahishwa na kufunguliwa kwa uwanja wa ndege lakini amesema sekta ya utalii imeporomoka kutokana na kufungwa kwa uwanja huo wa ndege.

Burundi mpaka sasa imerekodi maambukizi kwa watu 421 na kifo cha mtu mmoja.
 
Back
Top Bottom