Uwanja wa Ndege wa Mwanza utabeba Abiria wa Kigeni 200

For total operations ingekuwa 800 kwa mpigo maana ya departure na arrival
 
Sasa kwa nini wajenge uwanja wa abiria 200?
Mkuu uliwahi kusoma Kitabu cha kusadikika?

Ile Nchi iliyozungumziwa ni Bongoland

Sioni umuhimu wa kujenga uwanja wa kupokea abiria 200 wakati ndege Moja ya Airbus inabeba zaidi ya abiria hao.

Na kusema kweli ndege ya kwenda Mwanza huwa inajaza siti zote labda mambo yabadirike hivi karibuni
 
Abiria 200 au 2000 jamani, abiria 200 ni kidogo mnoooooooo, jengo la abiria 200 ni dogo sana sana for International Airport
 
Ule wa Chato (ambao sasa lami yake imeshageuzwa na wananchi kuwa ni jiwe kubwa la kukaushia mpunga na mahindi) laiti kama fedha zake zingetumika kuupanua huu wa Mwanza, hakika Mwanza sasa ingeshakuwa nyingine kabisa..

Lakini kwa ujinga na upumbavu wa viongozi wa serikali ya CCM waliokuwa wakiongozwa na yule babalao Hayati Rais John P. Magufuli wakafanyaga maamuzi ya kijinga na kipumbavu (sawa na ujinga na upumbavu wao) ya kwenda kuzika mabilioni ya fedha huko Chato - Geita badala ya kuiimarisha hadhi ya huu wa Mwanza..

Sasa hivi Mwanza Airport ungeshakuwa na hadhi ya kimataifa muda mrefu sawasawa na ule wa Mwl Julius Kambarage Nyerere International Airport - Dar es Salaam..

Sasa hivi wanahaha lakini pamoja na hayo uwekezaji huu ni mdogo sana na hautainua hadhi ya uwanja huu katika kiwango cha kimatifa kinachotakiwa. Ni bora fedha iongezwe mara nne kufikia 200bn tupate uwanja wa tatu mkubwa wenye hadhi kwelikweli ya kimataifa ili kanda ya ziwa ifunguke kimataifa zaidi..
 
Kanda ya ziwa ikifunguka kuna kanda itapotea maana Serengeti iko kanda ya ziwa
 
Waende na mtizamo wa Mb Tabasamu watafakari upya Rais aongeze pesa hata bn 5 tu wafanye variation au waweke addedum kwenye mkataba kuongeza ujazo,pamoja na ubora unaosemwa kimataifa izingatie pia ujazo uendane na hadhi ya jiji la Mwanza. Wabunge acheni kushangilia uwanja wa aina hii.
 
Mizengwe mingi kuhusu ujenzi wa uwanja huo toka zamani ni ishara kwamba kuna watu wanaoweka ngumu hapo kwa sababu zao wanazozijuwa wenyewe.

Hili la sasa kama ilivyo kawaida, ni ghersha tu, toka kwa watu waliojaa hadaa na udanganyifu mwingi, kuwapofusha akili watu ili wapate wanalotaka (kura) wakati wa uchaguzi. Hawa hawana nia yoyote ya kufanikisha ubora wa uwanja huo.
 
Mwanza kutua ndege ya watu 300 si leo, wageni weengi Mwanza kutafuta Nini? hayo majengo mengine yatajengwa baadae kwasasa hilo linawafaa.
Waskuma msipende makuu yasiyo na tija
Siyo "wasukuma" pekee wanaoishi huko; na siyo "wasukuma" pekee hupanda ndege.
Mawazo yako ni ya kitoto sana kama huelewi mifumo ya usafiri wa anga.
 

Bila shaka hujawahi kupanda ndege hata mara moja ndiyo maana una ushamba mwingi na ujinga sana
 
Miezi 10 siyo mingi tutaona kama itakuwa international airport de jure. Maana huko nyuma ulipokaribia uchaguzi waziri mmoja wa miundo mbinu awamu ya 5 wakati wa Mongela aliwahi kuhadaa na kutangaza UMMA kuwa umekuwa international baada ya kuileta air Rwanda kubeba minofu na kisha ET sijui declaration hiyo ilipotelea wapi. uwanja huu inatumika kisiasa zaidi. wacha tuone this time.
 
Bila shaka hujawahi kupanda ndege hata mara moja ndiyo maana una ushamba mwingi na ujinga sana
Mada inayojadiliwa ni uwanja wa ndege wa Mwanza..

Hatujadili nani amewahi kupanda ndege na nani hajawahi..

Hata nikukuambia kuwa huwa nasafiri kwa ndege mara kwa mara ndani na nje ya nchi, unadhani wewe itakuongezea nini kichwani mwako?

Nyie vijana wa UVCCM ni wajinga sana aisee...

Wengi ni wazito na wagumu kuelewa mambo...

Ndio maana kwenye majadiliano mnapigwa sana..

Na huwa mkizidiwa kwa hoja, mnajigeuza mapolisi kanzu na wengine UWT feki na kuomba bunduki kuwaua wapinzani wenu huku mkilindwa na mabwana zenu..!
 
Sasa unataka nani akusapoti eti pesa nibora zingeboresha mwanza airpor. Na sindio nyinyi mnaanzishaga thread mnanza kusema mwanza na Arusha wapi bora![emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji4] unataka uwanja wakimataifa uwanze kulingishia mikoa jirani?[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji847][emoji847][emoji847] baba pesa ya silikali aipangiwi... Na sisi wanjombe tunataka uwanja[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] wakimataifa.... (Inshot acha wivu na nyinyi ndo mlio uuwa uwacha wa chato, mbona kipindi Magu ajaaga ndege zilikua zinatua! Uja jiuliza?).
 
Siyo "wasukuma" pekee wanaoishi huko; na siyo "wasukuma" pekee hupanda ndege.
Mawazo yako ni ya kitoto sana kama huelewi mifumo ya usafiri wa anga.
Viongozi wenyewe kils siku wanapanda ndege kwenda Mwanza je wanafurahia kutua kwenye uwanja chakavu kama huu!
 
Viongozi wenyewe kils siku wanapanda ndege kwenda Mwanza je wanafurahia kutua kwenye uwanja chakavu kama huu!
Mimi hata sielewi huo uwanja una tatizo gani; maana haikuanza leo. Huu uwanja ni miaka na miaka umekuwa ukipigwa danadana. Ni kama kuna watu wanayo maslahi fulani na uwanja huu!

Magufuli mwenyewe hakufanya bidii ya kuujenga ipasavyo; badala yake kaweka nguvu zaidi kwa ule wa Chato!

Kuna jambo lisiloelezeka juu yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…