Uwanja wa Sheikh Amri Abeid | Vodacom Premier League VPL, Coastal Union Vs Simba SC

Uwanja wa Sheikh Amri Abeid | Vodacom Premier League VPL, Coastal Union Vs Simba SC

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League (VPL), kuendelea kuvurumishwa leo November 21, 2020 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, ambapo Wagosi wa Kaya, Coastal Union, wanapambana na Mnyama Mkali, Simba SC.

Ni mechi kali na ya kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 za mchezo huku kila timu ikihitaji alama tatu muhimu VPL.

Kocha wa Coastal Union Juma Mgunda amesema wao wapo tayari kabisa kwenye mchezo huu, huku akisisitiza kwa wachezaji wake kuwa makini wawapo uwanjani.

Na upande wake Kocha wa Simba SC Sven Vanderbroeck amesema wanatarajia kukutana na ushindani kwani mechi haitakuwa rahisi, lakini tupo tayari kwa mapambano.

Kumbuka mtanange huu wa VPL ni kuanzia saa 10: 00 jioni.. Usikose Ukaambiwa.

Kulipewa Mwana.. Kulitaka Mwana

Update,

Timu ya Simba SC wakiwa ugenini wameitandika bila huruma Coastal Union mabao 7-0 kwenye Ligi Kuu Tanzania VPL' mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Mabao ya Simba yamefungwa na John Bocco amefunga mabao 3 Hat-Tick, Cloutius Chama mabao 2 huku Dilunga na Morrison wakifunga bao 2 kwa mmoja.



Screenshot_20201121-152226.jpg
 
Naendelea kusapoti chama langu Msimbazi, lkn kocha Kishingo bado simuelewi, mnisamehe kwa hilo na sijui kwanin hampendi KAHATA.
POINT 3 leo muhimu
 
Timu ziko uwanjani zikifanya ukaguzi pamoja na kupiga picha za kumbukumbu.

Wakati wowote mpira utaanza
 
Naaam mpira umeanza Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha

Ni mapambano wa VPL
 
06' Dilungaaaa anakwendaa
Goooooal Goooooooooooooooaal

Hassan Dilunga anahesabu bao la kwanza upande wa Simba SC, kazi bomba ya John Bocco

Coastal Union 0-1 Simba SC
 
Naona leo Nyoni anacheza sita ( kiraka)
 
10' Ni free kick kuelekea Simba SC, anakwendaa kupiga mchezaji wa Coastal anapigaaaa njeeeeee
 
13' anakwendaa Mohamed Hussein anawekwa chini, anapiga lakini ni faulo tena

Anapiga Chamaaaa, mpira unagongwa mwamba, laaaaa ilikuwa hatari sana lango la Coastal
 
17' Coastal walipata Kona ambayo hazikuzaa bao, baada ya mpira uliopigwa kutoka njee na kuwa goal kick
 
24' Gooooooooooooal John Bocco anaandika bao la pili baada ya kupokea pasi safi kwa Dilunga

Coastal Union 0-2 Simba SC
 
06' Dilungaaaa anakwendaa
Goooooal Goooooooooooooooaal

Hassan Dilunga anahesabu bao la kwanza upande wa Simba SC, kazi bomba ya John Bocco

Coastal Union 0-1 Simba SC
Mpira wa Simba umekuwa laini mnooooo, yaani utazan wachezaji hawana mazoezi ya Viungo. Dilunga ndio kawa mwepeeeeesi hadi anakera. Timu haipigi mashuti langonk mwa adui halafu tunataka Kombe la CAF
 
28' Bocooooo......Goooooal goooooal

John Bocco anaandika bao la tatu baada ya kazi bomba ya Morisson
 
Mpira wa Simba umekuwa laini mnooooo, yaani utazan wachezaji hawana mazoezi ya Viungo. Dilunga ndio kawa mwepeeeeesi hadi anakera. Timu haipigi mashuti langonk mwa adui halafu tunataka Kombe la CAF
Kweli team bado haina makali sana
 
Back
Top Bottom