Mtapata tabu sana msimu huu! Eti pasi tano!!!?? Sasa hivi sio mechi za mikoani tena! Na badoMkuu kwani we huoni timi hata kupiga pasi 5 zifike hawawezi ni butua butua tu
Raha ya marathon kumalizianasikia rahaaa utamuuuu jamani yanga rahaa utamu
oyoooooooooo....!
mikia fc utawasikia ligi bado mbichi...jitieni tu mioyo sisi ndio haooo...! yani akili yenu na maombi yenu kusema hivi kwamba yanga atapoteza michezo ya mbeleni teh teh teh hilo msahau coz kama sisi tutapoteza na mikia fc watapoteza tu...ila dalili ya mvua ni mawingu
leo wamecheza Tanzania prison lakini kuugua na kuombeleza wameombeleza mashabiki wa simba na prison.....yanga wamechakaza wote wawili
Papii sijui Nani Nani ndo alikuwa anabeba power bank ya SimbaHuyo mchezaji super-tall wa Msimbazi alikuwa anaitwa nani?
Hahahahaaa naona unajitekenya na kisha unacheka mwenyeweKwani ligi imeisha? Ndo Kwanza 14 Kati ya 38 kwa yanga hi pumzi itakata muda si mrefu
Labda hufatilii mpira jombii zaidi ya hii ligi ya bongo, juzi kati Marcus rashford alipogwa redcard vs Burnley kwa kosa kama hilo la ngasa, kwenye mpira haya yanatokea sana na yataendelea kutokea banana binadamu siyo wote wanaoweza kuzuia temper, akishajaa anajikuta anafanya kitendo cha ajabu ambalo hadi yeye mwenywe anakuja kulijutia.Kama TFF ikimuongezea adhabu itakuwa ni jambo la busara zaidi, alichofanya sio kitendo cha kiungwana kabisa, tangu nimeanza kufuatilia huyu bwana mdogo kwenye 2006 sijawahi kushuhudia hiki alichokifanya leo, alikotupeleka leo tulishatoka huko, sasa hivi kuna kamera kibao uwanjani, Ngasa anasahau kuwa hakuna anachoweza kukifanya kikakwepa kamera zote zilizopo uwanjani, poor him.
mbinu moja wapo ya kumshinda mpinzani wako katika marathon ni kumtangulia mpinzani wako kwa maana utakuwa unamchosha na kumfanya akate tamaa kwa maana kila akichirimika akukute we unakuwa mbali zaidi na ndivyo ushindi utapataRaha ya marathon kumalizia
Tutaheshimiana tuLeo mida ya saa kumi jioni kwa saa za Afrika Mashariki utapigwa mtanange wa kukata nashoka kati ya maafande wa magereza Tanzania dhidi ya Yanga afrika, yanga ambayo haijapoteza mchezo ata mmoja ikiwa inaongoza ligi kuu, itavaana na maafande wa magereza Tanzania ambao wako katika nafasi ya 19,swali ni je Yanga itaendeleza ubabe katika TPL kwa kujinyakulia alama zote tatu au Prison watafanya maajabu leo ili kutoka mkiani walikosalia?
Tukutane hapa kupeana yale yatakayokuwa yanajiri huko uwanja wa Sokoine Mbeya.
Updates
Dakika 45 za kipindi cha kwanza ndio zimeanza hapa ccm Sokoine Mbeya.
Updates
19' yanga wanapata mpira wa adhabu senti mita chache kabisa kutoka 18, anaenda kupiga Ajib.....anakosa.
Updates
35' Maka Edward anapewa kadi ya njano, na prison wanapata nafasi ya kupiga mpira wa adhabu kuelekea lango la yanga, prison wanapoteza nafasi hii ya mpira wa adhabu.
Updates
43' prison wanapata penalty
Ajibu, Juma Abdul, Chikupe wanapewa kadi ya njano hapa.
45' prison wa naandika goli la kwanza kupitia kwa Jumanne Nikaze Elfadhili.
Updates
Vurugu zinatokea hapa uwanjani, mchezaji wa prison yupo chini,mrisho Ngasa kampiga kichwa Hassan Kapalata, hiki ndicho chanzo cha vurugu.
Updates
Umeme unatolewa kwa Ngasa na Laurian Mpalile, kadi nyekundi.
Mpira ni half time.
Updates
45' za kipindi zinaweza kuanza muda wowote kuanzia sasa, wakati huo huo Mateo Anthony anaingia kuchukua nafasi ya Maka Edward, mpira umeanza hapa.
Updates
51'Jumanne Elfadhili anapewa kadi ya njano kwa kumchezea mchezo usiokuwa wa kiungwana Feisal Salum.
Updates
Maji mazito kwa Feisal, anakwenda bench na nafasi yake inachukuliwa na Thaban kamusoko
Updates
74' yanga wanapata penalty.
76' Ajibu gooooooooo prison 1 yanga 1.
Updates
80' Prison 1 Yanga 1.
Updates
84' Amiss Tambwe anaiandikia yanga goli la pili hapa.
Updates
+3 za nyongeza hapa uwanja wa mbeya
90+ gooooooooooo Amiss Tambwe anaiandikia yanga goli la tatu hapa.
Updates
FT Prison 1 yanga 3, mpira umekwisha hapa.
Ligi itaisha mtabaki kusema hivyohivyo huku Yanga ikibeba ubingwa....Kabisa mkuu, hawa wametangulia na baiskeli ya barafu, jua la February na March halitawaacha salama, kila mmoja atakuwa kwenye nafasi yake kipindi hicho.
Yanga baskeli ya barafu alafu tunakaribia saa 6 mchanambinu moja wapo ya kumshinda mpinzani wako katika marathon ni kumtangulia mpinzani wako kwa maana utakuwa unamchosha na kumfanya akate tamaa kwa maana kila akichirimika akukute we unakuwa mbali zaidi na ndivyo ushindi utapata
Upepo unaisha huku ubingwa tushabeba tayari kama ilivyokua simba msimu ulioisha kwa kagera.Hapana, huu upepo utafikia mwisho tu.
Amini nakuambia, kuna timu za aina mbili tu, zinazoongoza kwa ushindi na zinazoongoza kwa ballpositionHuu ndio ukweli ambao mashabiki wengi wa yanga hawataki kabisa kuukubali, kikosi kibovu kama hiki cha yanga kikichukua ubingwa itakuwa ni fedheha kubwa kabisa katika ligi kuu Tanzania Bara.
Yanga hawezi pata alama tatu mbele ya simba na azam, hapo lazima afungwe breki, hasa akikutana na Simba ata waweke magolikipa kumi mbele acheze mtu mmoja game ya raundi ya pili kichapo kiko pale pale.
Hahahaaa, umesahau ya boko kumpiga mwenzie ngumi?Mkuu kyata kwa upumbavu aliofanya Ngasa wa kumpiga mchezaji wa prison kichwa akifungiwa atakuwa kaonewa? Let us be objective on this matter even once, Ngasa anatakiwa kufungiwa ili iwe fundisho kwake nakwa wachezaji wengine wasiokuwa na uungwana wawapo uwanjani, timu yenu haina nidhamu ata kidogo, chikupe nae ni mtu wa vurumai, kiukweli fundisheni timu yenu nidhamu kwani wakitanguliwa kufungiwa wote wanapaniki.
Hivi hadi ifike march si itakua tumeshawaacha pointi zaidi ya 20 huko?Mkuu hawa wametangulia na baiskeli ya barafu jua la Feb na March halitawaacha salama abadan asilan.
Sakanma tu mzee familia yako haijambo?Hali yako vipi mkuu?
Siku 12 mechi 4 ...tatu mikoani..points 12... mababu wa mikia wanaweza????Kikosi hiki Cha Sasa hakina ubora was kuchukua ubingwa ukilinganisha na Azam na Simba kwa Sasa ni upepo mzuri unapepea jangwani ukiambatana na bahati
Tofauti ya Simba na Yanga ni moja..Simba kufungwa na Mbao hakubadilishi maana na uhalisia kwamba Yanga wanna timu mbovu Quality ya wachezaji wa Yanga inaonekana japo matokea yapo upande wao kwa sasa
Manara ndio kasema hivyo..teh teh tehNi aibu mkuu Yanga kuongoza ligi timi mbovu sana
umeanza kutazama mpira lini??? Yanga bingwa mara 27... ukiona Yanga anachukua points mikoani ujue anachukua ndoo....mara ya mwisho Yanga kufungwa Dar es salaam na timu za mikoani ilikuwa 2009....Bahati na upepo ndio vinavyowabeba ila si kitambo kidogo mtaanza kutafutana, amin amin nakuambia.