Uwanja wa Taifa Dar: Yanga1-0 St Louis, Ligi ya mabingwa Afrika

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253

Dk 1, mechi ndiyo imeanza na Yanga wanaanza kujipanga wakitaka bao la mapema

Dk 2 krosi safi ya Buswita, walinzi St Louis wanazembea na Raphael Daud anachelewa

Dk 2 Tshishimbi anaachia mkwaju safi hapa lakini ni goal kick

Dk 3 Martin naye anageuka naye vizuri, mkwaju mkali kabisa kutoka mguu wake wa kushoto, kipa yuko makini, anadaka

Dk 5, Yanga wanapata kona, inachongwa lakini ni dhaifu, inaokolewa

Dk 7, shambulizi kali la kwanza la St Louis, krosi nzuri lakini Tshishimbi anafanya kazi nzuri kabisa na kuokoa

Dk 10 sasa, bado Yanga hawajafanya shambulizi kubwa na hali ilivyo, St Louis wanaonekana kukaa nyuma zaidi wakifanya mashambulizi ya kushitukiza

Dk 11, shambulizi jingine la St Louis, Tahid anaachia mkwaju mkali hapa lakini Kabwili yuko
vizuri, anakamata

Dk 15 sasa, ndani ya dakika tatu hakuna shambulizi hata moja la Yanga ndani ya lango la St Louis. Yanga wanatakiwa kujitahidi kupata bao mapema na mfumo wa krosi wanaoutumia unaonekana umekataa, hivyo lazima wabadili ili kupata mabao ya mapema kwa kuwa wao ndiyo wako nyumbani

Dk 16, Yanga wanapata kona, inachongwa na Ajibu, nafasi nzuri kwa Buswita baada ya kipa kujichanganya lakini anachelewa

Dk 17, nafasi nyingine kwa Yanga, Chirwa anaingia vizuri lakini Yanga hakuna mtu

Dk 17, Yanga wanaonekana kuchangamka, Buswita anaachia mkwaju mkali lakini unatoka nje
kidogo

Dk 17, St Louis inabidi pia wawe makini maana wanacheza faulo hovyo, Yanga wanatakiwa kuendelea kuwapa presha zaidi ili wazidi kucheza faulo

Dk 19, Martin anaachia mkwaju mkali kabisa lakini hakulenga lango hata kidogo...

KADI Dk 22, Herve analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Kessy
PENAAAAAAAT Dk 22, Kessy anaangushwa ndani ya eneo la penalti box na mwamuzi anasema ni penaaat

Dk 27, chirwa anaangushwa nje kidogo ya boksi mwamuzi anasema faulo
ANAKOSAAAA Dk 24, Chirwa anapiga na mpira unapita nje. Iko haja ya Yanga kumbadili sasa Chirwa katika upigaji penalti

Dk 27, Ajibu anapiga faulo hiyo lakini inatoka nje sentimeta chache juu ya lango la St Louis

Dk 30, yanga wanagongeana vizuri na Patrick Kelvin Yondani anajaribu mkwaju maridadi kabisa, goal kick

Dk 31, beki wa St Louis anaunawa mpira nje kidogo ya boksi yao, mwamuzi anasema ni faulo

Dk 32 Gadiel anaichonga ile faulo la anapiga hovyo kabisa

Dk 33, Yanga wanasukuma shambulizi jingine na kupata kona, inachongwa kona dhaiifuuu kabisa, hawa Yanga vipi?

Dk 34, nafasi nyingine ya Yanga, Ajibu akatika nafasi nzuri anapiga kasimama kama msumari, goal kick

Dk 35, mpira safi wa Ajibu, Buswita anapiga kichwa nyanya, goal kick

Dk 37, Yanga wanapata kona nyingine, inachongwa na Ajibu, inaokolewa na kuwa kona ya tano

Dk 37, Gadiel anachonga kona ya tano ya Yanga, ni kona dhaifu na inadakwa kwa ulaini

Dk 39, Gadiel anaingia vizuri anapiga krosi, inaokolewa na kuwa kona

Dk 40, inachongwa kona, mpira unamkuta Yondani anaachia mkwaju mwingine matata lakini hakulenga lango

Dk 41 mwamuzi anasimamishwa mpira kwa muda, wachezaji waweze kupoza makoo yao

Dk 43, Tshishimbi anaachia mkwaju mkali kwelikweli, bahati mbaya unatoka nje sentimeta chache kwenye lango la St Louis

Dk 44 St Louis wanagongeana vizuri kwa lakini mwisho wanapiga shuti kuuubwa la kutungua minazi

DAKIKA 1 YA NYONGEZA

MAPUMZIKO

Dk 45 Mechi imeanza kila upande ukionekana umepanga kufanya vizuri

Dk 47 Yanga wanapata kona ya kwanza kipindi cha pili, inachongwa, Buswita anapiga tik tak, kipa anadaka

Dk 48 St Louis inapata kona, inachongwa lakini ni dhaifu kabisa

Dk 50 sasa bado hakuna bao, Yanga wanapata kona lakini ni butu

Dk 52, St Louis wanafanya shambulizi kali, Yanga wanajichanganya hapa

Dk 56 Bado Yanga hawana ile hali ya kutaka kupata bao la mapema

Dk 60 St Louis wanafanya mabadiliko

Dk 60 Ajibu anapoteza nafasi nyingine muhimu kabisa, yeye na nyavu, hii hatari kabisa

Dk 64, Yanga inapata kona nyingine lakini ni dhaifu

SUB Dk 66 Juma Mahadhi anaingia kuchukua nafasi Ajibu na Martin anakwenda nje pia anaingia Godfrey Mwashiuya

GOOOOOOOOOOO Dk 67, Yanga inapata bao la kwanza kupitia Mahadhi

Dk 68, St Louis wanaonekana wamepania kurejesha bao, wanafanya shambulizi lakini Yanga wako makini

Dk 70, Yondani anaachia mkwaju mkali hapa, mara nyingine kipa yuko makini

Dk 72, Yanga wanapoteza nafasi nyingine nzuri hapa baada ya krosi nzuri ya Mwashiuya, kumfikia Chirwa ambaye anapiga shuti kuuuuuuubwaaaaaa

Dk 73, St Louis wanafanya shambulizi kali, mshambuliaji wao alibaki yeye na kipa Kabwili, mpira wa kichwa, akashindwa kumalizia

Dk 75 pasi nyingine nzuri, Mahadhi anaiwahi lakini beki anatoa na kuwa kona

Dk 75, MWashiuya anachonga kona lakini safai hii kipa Todo, anadaka kwa ulaini kabisa

Dk 77 kwa kuwaangalia, hawa St Louis wanaonekana wamechika sana lakini wanajitutumua. Yanga wanapaswa kuzidisha mashambulizi ili kupata bao la pili

Dk 81, Mwashiuya anaachia mkwaju mkali kabisa, goal kic
KADi Dk 80 Herve wa St Louis analambwa kadi ya njano kwa kumvuta Mwashiuya

Dk 82, Mahadhi anaingia kwa kasi tena lakini inaokolewa na kuwa kona, inachongwa na Mwashiuya, inaondoshwa

Dk 85 krosi nzuri ya Chirwa, Buswita anaruka vizuri lakini St Loius wanaokoa

SUB Dk 86 Yanga wanamtoa Buswita, anaingia Yusuf Muhilu kuchukua nafasi yake

Dk 88 St Louis nao wanafanya mabadiliko wanamtoa Herve na kumuingiza Lane

Dk 90 sasa, wachezaji wote wa St Louis wamerudi nyuma na mpira unakuwa mgumu kwa Yanga wanaotaka bao la pili huku wageni wao wakionekana hawataki kufungwa zaidi

DAKIKA 3 ZA NYONGEZA

MPIRA UMEKWISHA
 
Uko nyumbani unapata kagoli kamoja!
 
yanga hii raund ya kwanza wanapita kimbembe kipo raund ya pili ns el merreikh cjui watatokea wapi?
 
Sasa mnaifunga time dhaifu km Ole bao moja kweli yanga imekwisha. Katibu imezoea ligi tu kubebwa na kuhonga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…