Uwazi wa Mikataba ya Serikali huchochea Maendeleo jumuishi

Uwazi wa Mikataba ya Serikali huchochea Maendeleo jumuishi

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
0001-18419382945_20210317_094436_0000.png


Uwazi, Uingiaji, Usimamizi na Upatikanaji wa Mikataba na Taarifa katika Sekta ya Madini, Mafuta na Gesi umebaki kuwa ni changamoto.

Hali hii inazuia wananchi kupata taarifa sahihi, na kwa wakati, hili linapunguza hali ya kujiona kuwa ni wamiliki wa rasilimali zao na kupunguza shauku ya kushiriki kikamilifu katika majadiliano na maamuzi kuhusu usimamiaji wa rasilimali za umma.

Uwazi wa Mikataba ni uwekaji na upatikanaji rahisi wa mikataba inayohusu rasilimali za umma iliyoingiwa kati ya serikali na makampuni.

Mchakato wote wa utayarishaji wa mikataba unatakiwa kuwa wazi, wa haki, na wenye ufanisi tokea hatua za upangaji, utoaji wa zabuni, ugawaji, na utoaji wa mikataba hadi utekelezaji.
 
Upvote 1
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom