Uwezo ninao, tatizo lipo wapi na mimi nifanikiwe?

Smith Rowe

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2018
Posts
4,319
Reaction score
9,003
Nina pesa nyingi sana kwenye makaratasi. Nina akili vizuri sana ila sina hela mkononi. Darasani nimekimbiza watu sana. Mawazo ninayo mengi na mazuri Sina vitendea kazi

Mawazo yamegeuka msongo wa mawazo. Kesho yangu sijui itakuwaje. Mtaji umekuwa kikwazo. Kipaji changu hadi Leo sijakijua. Sioni future kwenye elimu kabisa

Wakubwa zangu nyie mmetumia njia hipi. Mmefanikiwa kupitia nini? Mbona sioni taa ya kijani miaka 3 mbele? Mbona kwangu mtaji ni tatizo sana? Au tatizo sio mtaji?

Hivi kufanikiwa kunaanzaje?

Tusaidieni wanazengo kwa mawazo ya kutufungua kiakili ili na sisi tutoboe

Tupeni elimu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu, tuliambiwa tungojee tanzania ya viwanda inakuja uku na sisi tuakianzisha viwanda vidogo vya kukamua miwa
 
Bro una mtu aliyefanikiwa (tajiri) ambaye una ukaribu nae. Ili uwe na fedha nyingi ulimwenguni wekeza kwenye biashara.

Humu utapewa pole🙄tu

Tunajuana sie.
 
Una pesa nying kwenye makaratasi kivipi? Halafu una akili nying na umekimbiza watu darasani...!? How...!?

Mkuu hapo ndo kuna tatizo. Hivi kukimbiza watu darasani na maisha ya mtaani ni wapi na wapi? Tatizo lipo kwenye kukariri... Ishi kwa uhalisia mkuu, ishi vile mazingira yalivyo.

Isahau jana yako, (yakumbuke tu makosa yako ya jana ili uiimarishe leo yako), iishi leo yako, itafakari kesho yako.

Yote kwa yote pole sana mkuu.
 
Nashukuru sana mkuu
Kwa ushauri mujarabu
Lakini sijamlalamikia mtu mkuu haya niliyoandika tunapitia vijana wengi tuu huku mtaani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tupe cv yako imekaaje yaani namaanisha elimu yako ipoje na umesomea fani gani?

Hali uliyonayo hata mimi ilinikuta kwa miaka mingi sana hadi hivi karibuni angalau nimeanza kupata nuru.

Maelezo yako nimeyaelewa vizuri sana kwa sababu ni vitu nilipitia yaani unakuta kichwa muda wote kinajaa michanganuo mbalimbali hadi utajiri unauona umekaribia kabisa lakini mfukoni hamna kitu.

yaani kichwa kinafocus mambo mengi hadi mwili unakonda
Nashukuru sana mkuu
Kwa ushauri mujarabu
Lakini sijamlalamikia mtu mkuu haya niliyoandika tunapitia vijana wengi tuu huku mtaani

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu usichanganyikiwe kitu cha kwanza jua unachotaka katika maisha yako, pili jua namna gan ya kupata.

Usitake kufanya kila jambo chagua vitu vichache vya kukomaaa navyo, hapa duniani yapo mambo mengi huwezi kufanya kila jambo



Sent using Jamii Forums mobile app
 
...Vizur sana mkuu,hiyo hali vijana wengi huwa tunapitia.

Kwanza kabisa,embu jitambue kwamaana jifahamu ww mwenyew...
- nini unataka\ unataka kuwa nani.

Pili,jijenge katka hali ya positive thoughts usiwe unafikiria mambo hasi ktk maisha yako hasa ktk mafanikio.
( If u hold negative thoughts about yrself at subconscious level,u will tend to experience negative realities in yr life and vice versa)

Tatu,jijengee utaratibu wa kujiongezea maarifa ktk kichwa chako,soma sana vitabu hasa vile ambavyo vinazungumzia mambo ya mafanikio mfno: Rich Dad poor Dad

Nne,tafuta fursa swala la mtaji sio matter sana,wapo watu wanapeana lakin hawana mawazo ya kutengeneza fursa so unaweza ukatafuta fursa then ukatafuta mtu mwenye pesa mkajoin mambo yakaenda,au andaa ata business plan zako vzur naamin wapo watu ambao utawapata waweze kuwekeza pesa zao kupitia business zako.

Tano,jitaidi kutafuta connection zaidi, achana na watu ambao hawakupi mchango wwote ktk maisha yako zaid ya kukudumaza tu kimawazo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…