Uwiano wa umri wangu na uzito ni tofauti sana mpaka naogopa

Uwiano wa umri wangu na uzito ni tofauti sana mpaka naogopa

Wamajanga

Senior Member
Joined
Jun 24, 2014
Posts
133
Reaction score
47
Ni hivi nina umri wa miaka 23 lakini uzito wangu ni kilogram 86 uwiano wake ni mkubwa kupita na naogopa usije kuniletea madhara

Na nilikuwa nakuombeni mnitajie vyakula vya kuacha ili nipungue mwili mana mazoezi nashindwa kwa sababu nipo bize sana


Msaada wenu jamani unatakiwa
 
Wewe bado unakua kwahiyo ni muhimu kula vyakula vya aina zote yaani vyenye protein na carbohydrate pia ila zingatia kupunguza junk food yaani chipsi, snacks nk ambavyo haviongezi kitu mwilini mwako

Mazoezi ni muhimu sio lazima kwenda gym hata kutembea ni zoezi zuri kwako

Sijajua unapendelea vyakula gani hasa ila kwa mji huu watu walio busy chakula chao kikuu ni chipsi

Mimi sio mtaalamu nimejaribu tu kusema kulingana na uelewa wangu wa kati

NB: Achana na 'junk food' hasa chipsi na vitu vingine kwenye hilo kjndi
 
Umri tu siyo shida sana, TAJA NA UREFU WAKO. HALAFU UNASEMA HUNA MUDA WA KUFANYA MAZOEZI MBONA UNASHANGAZA SANA, NA JE NI JINSIA GANI WEWE?
 
Mimi nina 185cm nina miaka 23 nina 70kg hapo vipi kuhusu uzito wangu unafaa au niongeze?samahani kwa kuingilia
 
Uzito sahihi unaotakiwa kuwa nao ni kwa fomula hii chukua urefu wako ktk sentimeta utoe na 100 kinachobakia ndio uzito unaotakiwa kuwa nao kiafya...mfano una urefu wa sentimeta 172 toa kwa 100 unatakiwa uwe na kg 72
 
chart hii hapa kila mmoja aangalie mwenyewe

BMI_chart.gif
 
Body mass index (BMI) = BMI = Weigh (kg)/(Height in meter)2

BMI 25 – 29.9 = Overweight; BMI > 30 Obesity
 
Mimi yangu ni 21 BMI niko kwenye normal
Formula
BMI = WEIGHT/(HEIGHT^2 in mt)
 
Uzito sahihi unaotakiwa kuwa nao ni kwa fomula hii chukua urefu wako ktk sentimeta utoe na 100 kinachobakia ndio uzito unaotakiwa kuwa nao kiafya...mfano una urefu wa sentimeta 172 toa kwa 100 unatakiwa uwe na kg 72

uuwiiii mimi nina urefu wa 165 cm na nna uzito wa 43 kg so natakiwa niongeze kula eeh?
 
Uzito sahihi unaotakiwa kuwa nao ni kwa fomula hii chukua urefu wako ktk sentimeta utoe na 100 kinachobakia ndio uzito unaotakiwa kuwa nao kiafya...mfano una urefu wa sentimeta 172 toa kwa 100 unatakiwa uwe na kg 72

Formula yoyote lazima iwe na conditions, sasa yako haina conditions kwa lugha nyepesi your formula is invalid.

Your formula is invalid for height less than or equal to 100.

Mtu akiwa na urefu wa cm 100, kwa mujibu wa formula yako atakuwa na uzito wa zero. Akiwa na urefu wa chini ya cm 100, basi atakuwa na uzito wa negative number.
 
Back
Top Bottom