UWT kumuenzi Bibi Titi Mohamed

UWT kumuenzi Bibi Titi Mohamed

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA (UWT) KUMUENZI BI TITI MOHAMED (1926 - 2000)

Leo nimetembelewa na Waandishi Maalum waliokuja nyumbani kwangu tufanye kipindi kuhusu maisha ya Bi. Titi Mohamed ambae taifa limeamua kumuenzi kama tangazo linavyoonyesha hapo chini.

Nimejitahidi kumueleza Bi. Titi kadri nilivyoweza.

Katika moja lililowashangaza wageni wangu ni pale nilipowaambia kuwa Bi. Titi Mohamed alihutubia mikutano ya TANU miwili akihanikisha wananchi wajiunge na TANU kudai uhuru mwaka wa 1955 hata haijui sura ya Julius Kambarage Nyerere inafananaje.

Naamini wengi wetu hatujui kuwa Bi. Titi Mohamed aliingizwa TANU na Schneider Abdillah Plantan, ili aunde Idara ya Wanawake katika chama ushauri aliopewa na John Hatch wa Labour Party ya Uingereza.

Hatch alikuja kumtembelea Tanganyika akiwa mgeni wa TANU.

Naamini wengi wetu hatujui kuwa Bi. Titi Mohamed aliingizwa TANU na Schneider Abdillah Plantan, ili aunde Idara ya Wanawake katika chama.

Bi. Titi alifanya kazi hii kwa ufanisi mkubwa sana.

Bi. Titi alisimama na Julius Nyerere bega kwa bega ndani ya TANU katika kupigania uhuru wa Tanganyika akihutubia mikutano katika viwanja vikubwa vya mapambano vya Tanganyika kama Mnazi Mmoja na Jangwani Dar es Salaam, Tangamano, Tanga na Uwanja wa Majengo Moshi kwa kuvitaja vichache.

Bi. Titi alivuka bahari na kuingia Zanzibar alikotoa msaada mkubwa kwa Afro Shirazi Party (ASP).

Bi. Titi hakuishia visiwani, aliingia Kenya kuisaidia KANU ili Jomo Kenyatta atolewe kifungoni akihutubia mikutano iliyofurika watu Mombasa na Nairobi.

Si hili peke yake Bi. Titi aliwahamasisha wanawake wa Kenya kutoka jikoni waingie uwanjani katika mapambano ya kuipigania nchi yao.

Wakati huo Bi. Titi akifanya haya yote alikuwa msichana mdogo hajafika miaka 30.

Waandishi hawa maalum katika mazungumzo yetu baada ya kufahamu kuwa nimeandika vitabu kadhaa katika historia ya Tanganyika walitaka kujua kwa nini hadi leo sijaandika maisha ya Bi. Titi.

Jibu langu kwao lilikuwa ninao mswada wa maisha ya Bi. Titi kwa miaka mingi lakini sijathubutu kuuchapa kuwa kitabu.

Sijaweza kuwa na ujasiri huo.

Niliwaeleza kuwa mimi si wa kuandika maisha ya Bi. Titi kwani Bi. Titi ameacha ''mwanae,'' shoga yake na mzungumzaji wake katika waandishi wanawake mahiri Tanzania.

Mwanamama huyu alikuwa karibu na Bi. Titi kwa miaka mingi hadi umauti ulipomfikia.

Huyu kasomeshwa na Bi. Titi alif kwa kijiti historia ya mapambano ya uhuru wa Tanganyika na askari mwenyewe aliyekuwa mstari wa mbele katika vita vile.

Bi. Titi kamweleza na kamsomesha shogs yake somo la ustahamilivu katika dhahma na fitna za siasa, utumishi wa jamii, kusamehe na kusonga mbele na mwenyewe Bi. Titi Mohamed.

Mwanamama huyu Bi. Titi alimfungulia kitabu cha maisha yake akamsomesha kuanzia ukurasa wa kwanza wa dibaji hadi ukurasa wa mwisho wa kufunga kitabu na kuweka kalamu chini.

Mwanafunzi huyu yeye kwa mapenzi hadi leo anamwita Bi. Titi ''bibi'' na haishi kumrehemu.

Huyu niliwaeleza Waandishi Maalum kapokea mengi katika historia ya maisha ya Bi. Titi kwani katembea na Bi. Titi mwenyewe katika safari yote ya maisha yake toka akiwa msichana mdogo.

Bi. Titi kwa mapenzi makubwa akimfungulia bint huyu masanduku yake ya nguo akimvisha shoga yake huyu kijana wa kileo muhitimu wa fani ya uandishi kutoka Uingereza khanga zake za miaka ya 1950 alizokuwa akivaa wakati wa TANU avae ajipambe achezee ngoma kila taasisi yao ilipokuwa na shughuli.

Huyu bint ndiye aliyemshika mkono bibi yake huyu akamfungulia mlango Bi. Titi atoke nje aliangalie jua upya.

Bi. Titi alitoka na akakubali kuwa Mlezi wa watoto hawa wa kike.

Bi. Titi katika shughuli hizi na vijana hawa kila walipomwalika shughuli yao na akiwa miongoni mwao walikuwa wakimkumbusha safari yake ya maisha na wenzake aliopigania nao uhuru wa Tanganyika wengi wao wakiwa wametangulia mbele ya haki.

Watoto hawa wa kike wasomi walikuwa matunda ya uhuru.

Kila alipowatazama walimkumbusha Bi. Titi, marehemu wanaharakati wenzake - Chiku bint Said Kisusa, Hawa bint Maftah, Tatu bint Mzee, Nyange bint Chande, Halima Selengia, Amina Kinabo, Mwema bint Sultan, Sharifa bint Mzee, Lucy Lameck, Fatma Matola kwa kuwataja wachache.

Nani leo anawakumbuka mashujaa hawa?

Ukurasa mmoja tu niliosoma aloniandikia mwandani huyu wa Bi. Titi umeniliza.

Nimelia kwa kuwa sikuwa nayajua niliyoandikiwa na nina hakika wachache sana wanayajua.

Nimelia kwa kuwa nilikuwa namuomboleza Bi. Titi baada ya kifo chake kupita miaka 21.

Wenzangu walikuwa wamelia na kufuta machozi.

Mwanafunzi huyu wa Bi. Titi ndiye wa kunyanyua kalamu kumwandika Bi. Titi si mimi mchezea pembeni.

Kama maandishi ya khanga yalivyozungumza, ''Tutamuenzi Bi. Titi Daima.''

Screenshot_20211021-011128_Facebook.jpg
 
UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA (UWT) KUMUENZI BI TITI MOHAMED (1926 - 2000)

Leo nimetembelewa na Waandishi Maalum waliokuja nyumbani kwangu tufanye kipindi kuhusu maisha ya Bi. Titi Mohamed ambae taifa limeamua kumuenzi kama tangazo linavyoonyesha hapo chini.

Nimejitahidi kumueleza Bi. Titi kadri nilivyoweza.
Kwahiyo ndio hao tu wasiojulikana, ambao walipigania uhuru?
 
UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA (UWT) KUMUENZI BI TITI MOHAMED (1926 - 2000)

Leo nimetembelewa na Waandishi Maalum waliokuja nyumbani kwangu tufanye kipindi kuhusu maisha ya Bi. Titi Mohamed ambae taifa limeamua kumuenzi kama tangazo linavyoonyesha hapo chini.
Wanamuenzi mhaini aliyetaka kupindua nchi? Ajabu. Wamuenzi na Komando Mohammed Tamimu.
 
Ugomvi ulianza 1966 lilipoanza vugu vugu la Azimio la Arusha kupora Mali za watu, Bibi Titi alipinga Amri ya Nyerere kupora Nyumba zote za Watu Nchi nzima zilizokuwa na thamani ya Tz.laki moja kwenda juu bila ya kujali namna mtu alivyopata mali hizo

Nyerere akashikilia msimamo wake akapora Mali za watu kwa kisingizio cha Azimio la Arusha na Bibi Titi akaporwa Nyumba zake mbili moja iliyopo Upanga Opposite na Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi JWTZ na Nyingine iliyopo Temeke Wailes Nyumba ambazo alipata kwa biashara zake ndogo ndogo kabla hajajiunga na Siasa

Kwny Kilele cha Mkutano wa Azimio walipambana kwa hoja sana akipokea Vitisho vya wapambe wa Kambarage hadi aliposimama na kusisitiza Hamuogopi yeyote aliepo ndani au nje ya Ukumbi haijalishi atapata Madhara gabi kwa kauli yake

Kauli ile ikachukuliwa kuwa ni Choko choko dhidi ya Jamhuri na akapelekwa Mahakaman kwa jaribio la Uhaini pamoja na kina Mzee John Lifa Chipaka wakahukumiwa Kifungo cha Maisha

1972 Mahakama ya EA ilitengua hukumu hiyo

1999 akihojiwa na Gazeti la Majira Bibi Titi alisema Ugomvi wake na Nyerere ulikuwa kwny Jambo moja la msingi 'haamini kama angeweza kukosea na kukosolewa'
Ilikuwaje akataka kuipindua Serikali ya Baba wa Taifa?
 
Ugomvi ulianza 1966 lilipoanza vugu vugu la Azimio la Arusha kupora Mali za watu, Bibi Titi alipinga Amri ya Nyerere kupora Nyumba zote za Watu Nchi nzima zilizokuwa na thamani ya Tz.laki moja kwenda juu bila ya kujali namna mtu alivyopata mali hizo

Thanks mkuu. Tungekuwa na uhuru wa habari biography kamili za viongozi na watu wakuu (mashujaa) zingeandikwa bila uoga kwa mabaya na mazuri yao, tungeelewa jinsi nchi yetu ilivyokuja kuwa ilivyo. Hatuna historia ya taifa letu kabisa. Tuna vipande vya propaganda za kimkakati.

Kuna watu wanarahisisha mambo kwa kufikiri Magufuli ndiye aliyeleta balaa. Wengine wanadhani ni Kikwete, wengine Mkapa na wengine Mwinyi. Kumbe mambo yalianza asubuhi na mapema. Nyerere alipotoa kitabu cha “Tujisahihishe” akielekea kung’atuka ilikuwa ni aina ya “kutubu” na kujaribu kurejesha utu.
 
Kwahiyo ndio hao tu wasiojulikana, ambao walipigania uhuru?
Rogo...
Paragraph za mwisho za kitabu cha Abdul Sykes niliandika kueleza kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika nyingi ilo katika mikono ya watu kwa hiyo ifanywe bidii ya kuiandika.

Maana yangu ni kuwa mimi nimeandika michango ya wale ambao niliweza kuwafikia lakini bado kuna wazalendo wengi ambao bado hawajatambuliwa.

Hii ina maana kuwa mlango bado uko wazi kwa utafiti zaidi.
 
Ugomvi ulianza 1966 lilipoanza vugu vugu la Azimio la Arusha kupora Mali za watu, Bibi Titi alipinga Amri ya Nyerere kupora Nyumba zote za Watu Nchi nzima zilizokuwa na thamani ya Tz.laki moja kwenda juu bila ya kujali namna mtu alivyopata mali hizo

Nyerere akashikilia msimamo wake akapora Mali za watu kwa kisingizio cha Azimio la Arusha na Bibi Titi akaporwa Nyumba zake mbili moja iliyopo Upanga Opposite na Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi JWTZ na Nyingine iliyopo Temeke Wailes Nyumba ambazo alipata kwa biashara zake ndogo ndogo kabla hajajiunga na Siasa

Kwny Kilele cha Mkutano wa Azimio walipambana kwa hoja sana akipokea Vitisho vya wapambe wa Kambarage hadi aliposimama na kusisitiza Hamuogopi yeyote aliepo ndani au nje ya Ukumbi haijalishi atapata Madhara gabi kwa kauli yake

Kauli ile ikachukuliwa kuwa ni Choko choko dhidi ya Jamhuri na akapelekwa Mahakaman kwa jaribio la Uhaini pamoja na kina Mzee John Lifa Chipaka wakahukumiwa Kifungo cha Maisha

1972 Mahakama ya EA ilitengua hukumu hiyo

1999 akihojiwa na Gazeti la Majira Bibi Titi alisema Ugomvi wake na Nyerere ulikuwa kwny Jambo moja la msingi 'haamini kama angeweza kukosea na kukosolewa'
Huko Mkuranga na Rufiji pia alikuwa na nyumba.
 
Bado historia inatolewa vipande vipande na wanaoitoa, wanaitoa kwa tahadhari kubwa
Y awezekana kuna jambo kubwa nyuma ya pazia linalomuhusu huyu bibi, waandishi wetu wanatakiwa kwenda mbali zaidi kuihakiki na kuielezea kwa uhakika historia halisi ya maisha yake mpaka umauti unamkuta. Tuwe wakweli ili tuifahamu historia yetu.
 
Huko Mkuranga na Rufiji pia alikuwa na nyumba.
Hivi Bibi Titi aliwahi kuolewa?
Na Nani,maishaa yake ya NDOA yakikuwaje!
Kutokana na simukizi za watu hapa,alipata umaarufu mkubwa akiwa chini ya Umri was miaka 30.
Alitoka familia ya aina gani!
 
Ashaenziwa huyu barabara imepewa mpaka jina lake!
Nyumba ndugu wanaishi upanga
Wajuku wako mabbroad huko
Anataka nini tena,serikali haikumtupa

Ova
 
Hatuna historia ya taifa letu kabisa. Tuna vipande vya propaganda za kimkakati.
Hapana, Usituchanganye kwa ajili ya kutokuelewa kwako!! hapo nakupinga mpaka kesho!! Historia ya Taifa letu tunayo sana tu!! kwenye vitabu vya kiada na ziada, usitake kutupotosha inawezekana wewe ulikimbia umande ndo matokeo yake haya!

Hukuudhuria, .....zamani zile somo la Historia unaanza kusoma rasmi drs la tatu!! tukawa na kitabu kilicho itwa Historia ya Tanzania, jamani chifu kwawa tulimjuaje, majimaji, MangisinaNK, la nne Historia ya Africa ivoivo mpaka ya Dunia!! hata Geografia ivo, ivo

wewe mzee muongo sana!! unaonekana ulikuwa mtoro hasa unasubiri kiporo cha bibi tu! hujui hata aa! asa kihiyo nae anachangia mjadala acha wenye akili zao waseme bana usituchanganye!
 
Huyu bibi alistahili kuwekwa ndani kwa sababu, kutaifisha nyumba zile kuwa mali ya Umma ambao wengi mmeupa jina baya eti kupora!! ulikuwa ni uamuzi wa Baraza lote la Azimio la Arusha!! walikubaliana na kutia sahihi!! km viongozi Nyerere alikuwa msimamizi tu!

Ila sasa wengi walikuwa vigeugeu! na walafi wa pesa!! walitumiwa tu! sababu baadaye walihongwa mapesa Mengi na mabepari uchwara ili kukwamisha na kupinga zoezi la utaifishaji na Malengo ya Azimio la Arusha!! akiwemo Kambona kitu ambacho ni kosa km kiongozi!!

Bibi titi na gegnge lake hawakuwa na msimamo!! kitu ambacho ni hatari kwetu km taifa!! alitumiwa na adui kirahisi mnoooo!! alikuwa hafai kuwa kwenye safu ya viongozi imara!! wa kusimamia sera za utekelezaji wa sera za sirikali bila kuyumba.

mtu pekee aliyekuwa na msimamo bila kuyumba ni kawawa na sokoine baaasi!! wengine woooote walikuwa ni hatare!! huenda tusingefika hapa tulipo km taifa tungekuwa zaidi ya somalia au DRC,

Julius Nyerere hakufanya kosa kusimamia maamuzi ya utekelezaji wa serikali yake, kwa sababu ndo ilikuwa kazi na wajibu wake km Mkuu wa nchi aliye pendwa na kuteuliwa na Mungu na wananchi wake miaka yote ya uhai wake! mpaka leo!! kwani nani anamuenzi bibi titi?

Haya kuyaelewa siyo mpaka uende kusoma UDSM hapana! ni uelewa wa asilia tu! wanafiki maishani ni wengi mpaka leo na kesho! dawa yao ni km hii hapa sasa!! tena mchonga alikuwa mstaaarabu sana.......

jiwe yeye alinyonga faster bin kudumbukizwa baharini kwenye viroba ufe polepole au risasi chagua weye mnyongwa!!!! ... kabisaaaa si utani!.... alikuwa hakucheleweshi! na huyo bibi ashukuru sana mchonga kwa usaliti wake ule!!!

Angekuwa Mlevibin kichaa Magufuli heee!! Bibi titi angepigwa risasi hadharani mchana kweupe! peee!! bila kupepesa macho km nanliu......halafu anakupa hela na passport ukaugulie kenya!! na dawa anakupa! haijalishi weye unajua sheria au hujui!

Halafu akisha kunaniliu anakusindikiza na hotuba ya usaliti!! ..... ''wasaiti nyie wanajeshi mnajua cha kuwafanya!! huwezi kumuacha msaliti ana survive! survive tu! km ivi!!''
 
Back
Top Bottom