Mbahili
JF-Expert Member
- Nov 28, 2016
- 281
- 525
Nikiwa naendelea subiri mzigo wangu Kariakoo, ngoja niwape nondo moja.
Je, upo tayari kupigania nchi yako kwa jasho na damu endapo kuna adui kaingia?
Je, unahani una sababu yeyote ya kupigania nchi hii?
Kama unasoma nakala hii na kujibu "ndio," naona kabisa akili inasaliti moyo. Moyo unasema hapana, akili hapana, ila mkono ndio. Ukichunguza kwa umakini, unahofia huenda ukisema hapana utafukuzwa kazi na ukoo mzima unakutegemea. Huenda utapoteza marafiki waliokubali kukana mioyo yao.
Lakini jibu halisi ni "hapana."
Kabla ya kuandika uzi huu, nilifanya utafiti. Nilichukua wanafunzi kumi wa darasa la saba na kuwaambia waniandikie wimbo wa taifa. Alipata mmoja tu, na si kuwa alipatia sana.
Tukumbuke darasa la saba ndio darasa la mwisho katika elimu yetu ya msingi.
Ni Watanzania wachache sana wanaojua historia ya nchi yao. Yaani, zaidi ya 95% watakwambia mwasisi wa TANU ni Nyerere.
Waasisi wengi na wapigania uhuru wengi, majina yao yamefichwa kwa makusudi maalum, na sio nyingine ila uchu wa madaraka.
Nisiandike mengi sana ila kiuhalisia ni kwamba hauwezi kuwa mzalendo kwa kitu usichokijua. Pia huwezi jua pasi na kujulishwa.
Ningeshauri wizara iangalie upya historia ya nchi yetu, wakombozi wapewe heshima yao, ijenge hamasa ya mtu kuwa tayari kwa ajili ya nchi yao.
Mfano mzuri, sikiliza wimbo wa taifa la Marekani. Huinua hisia ya kulipambania (hata kama ulizama kiaina).
Tanzania, somo la uraia litenezwe kiasi kwamba mwanafunzi tangu mtoto anajua na kuthamini ardhi yao, rangi yao, mila zao, na kila kitu chao.
Nikiwa nimesimama hapa juani, acha niwaache na hili.
Nikireport kutoka hapa karibu na madereva bodaboda, mimi ni Astrum27 wa JF.
Je, upo tayari kupigania nchi yako kwa jasho na damu endapo kuna adui kaingia?
Je, unahani una sababu yeyote ya kupigania nchi hii?
Kama unasoma nakala hii na kujibu "ndio," naona kabisa akili inasaliti moyo. Moyo unasema hapana, akili hapana, ila mkono ndio. Ukichunguza kwa umakini, unahofia huenda ukisema hapana utafukuzwa kazi na ukoo mzima unakutegemea. Huenda utapoteza marafiki waliokubali kukana mioyo yao.
Lakini jibu halisi ni "hapana."
Kabla ya kuandika uzi huu, nilifanya utafiti. Nilichukua wanafunzi kumi wa darasa la saba na kuwaambia waniandikie wimbo wa taifa. Alipata mmoja tu, na si kuwa alipatia sana.
Tukumbuke darasa la saba ndio darasa la mwisho katika elimu yetu ya msingi.
Ni Watanzania wachache sana wanaojua historia ya nchi yao. Yaani, zaidi ya 95% watakwambia mwasisi wa TANU ni Nyerere.
Waasisi wengi na wapigania uhuru wengi, majina yao yamefichwa kwa makusudi maalum, na sio nyingine ila uchu wa madaraka.
Nisiandike mengi sana ila kiuhalisia ni kwamba hauwezi kuwa mzalendo kwa kitu usichokijua. Pia huwezi jua pasi na kujulishwa.
Ningeshauri wizara iangalie upya historia ya nchi yetu, wakombozi wapewe heshima yao, ijenge hamasa ya mtu kuwa tayari kwa ajili ya nchi yao.
Mfano mzuri, sikiliza wimbo wa taifa la Marekani. Huinua hisia ya kulipambania (hata kama ulizama kiaina).
Tanzania, somo la uraia litenezwe kiasi kwamba mwanafunzi tangu mtoto anajua na kuthamini ardhi yao, rangi yao, mila zao, na kila kitu chao.
Nikiwa nimesimama hapa juani, acha niwaache na hili.
Nikireport kutoka hapa karibu na madereva bodaboda, mimi ni Astrum27 wa JF.