Uzee wako unataka uweje?

Uzee wako unataka uweje?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Natamani nikifikisha miaka 60 kama Mungu atajalia, nisiwe natumia nguvu nyingi sana za kupata ugali kwa siku. Kama itawezekana, uwe ni umri wa kucheza na wajukuu pamoja na kwenda kuwinda au kushangaa kobe porini.

Siku ya ibada kwa sababu mimi ni mkiristu, nisiwe nasali katika kanisa moja, bali kila jumapili niwe naenda kusali kanisa jingine.

Niwe nakula vyakula vya asili na kwa upande wa nyama niwe nakula nyama pori kama za sungura, ndege, swala, samaki n.k

Nitapenda niwe na dreva wa kike ambaye atakuwa smati na mcha Mungu, ambaye tutakuwa tunaenda naye tripu mbalimbali; nimechagua wakike kwa sababu ili safari zisiwe zinanichosha.

Nitapenda muda mwingi niishi porini ili niweze kupata hewa safi ambayo haijachakachuliwa na uharibifu wa mazingira.

We uzee wako unataka uweje?
 
Nimevuka huo umri mda sasa ila bado napenda kazi na bata
Kwa mwaka naweza kusafiri hata mara nne nje ya nchi na holiday zenyewe sio zaidi ya mwezi na wakati mwingine siku tatu kama Costa del Sol Spain nauli haizidi £150

Kustaafu bado kidogo ila kazi ni muhimu kuliko kukaa nyumbani na kukatakata garden
Hii siwezi kabisa kufanya nataka kuwa na uwezo wa kukimbia hata nikifika 80 Mungu akinipa umri
 
Nimevuka huo umri mda sasa ila bado napenda kazi na bata
Kwa mwaka naweza kusafiri hata mara nne nje ya nchi na holiday zenyewe ni sio zaidi ya mwezi na wakati mwingine ni siku tatu kama Costa del Sol Spain nauli haizidi £150

Kustaafu bado kidogo ila kazi ni muhimu kuliko kukaa nyumbani na kukatakata garden
Hii siwezi kabisa kufanya nataka kuwa na uwezo wa kukimbia hata nikifika 80 Mungu akinipa umri
Yote yanawezekana kama mikakati itakuwepo na afya ikiwa njema. Inasemekana pia, mwili usipoushughulisha kwa kazi, uzee unaweza kuja haraka pamoja na kutangulia mbele za haki? Kuna ukweli wowote hapa?
 
Nimevuka huo umri mda sasa ila bado napenda kazi na bata
Kwa mwaka naweza kusafiri hata mara nne nje ya nchi na holiday zenyewe ni sio zaidi ya mwezi na wakati mwingine ni siku tatu kama Costa del Sol Spain nauli haizidi £150

Kustaafu bado kidogo ila kazi ni muhimu kuliko kukaa nyumbani na kukatakata garden
Hii siwezi kabisa kufanya nataka kuwa na uwezo wa kukimbia hata nikifika 80 Mungu akinipa umri
Kwa nick name ya avatar sijui kama una umri huo labda inawezekana
 
Yote yanawezekana kama mikakati itakuwepo na afya ikiwa njema. Inasemekana pia, mwili usipoushughulisha kwa kazi, uzee unaweza kuja haraka pamoja na kutangulia mbele za haki? Kuna ukweli wowote hapa?

Mkuu kifo kipo pale pale
Ila fikiria mtu anaelala tu kwa mfano mgonjwa kitandani asietembea kwa siku nyingi
Hii inasababisha hata haja asiende vizuri kwa sababu mwili haufanyi harakati zozote

Hata kama ukiwa huna maradhi ila umekaa tu kula kulala ni kujitakia maradhi na hata msongo wa mawazo

Naamini kifo kwa kila aina ya viumbe uwe na afya au mgonjwa
Ila kuwa fit pia ni muhimu sana
 
Nimevuka huo umri mda sasa ila bado napenda kazi na bata
Kwa mwaka naweza kusafiri hata mara nne nje ya nchi na holiday zenyewe ni sio zaidi ya mwezi na wakati mwingine ni siku tatu kama Costa del Sol Spain nauli haizidi £150

Kustaafu bado kidogo ila kazi ni muhimu kuliko kukaa nyumbani na kukatakata garden
Hii siwezi kabisa kufanya nataka kuwa na uwezo wa kukimbia hata nikifika 80 Mungu akinipa umri
Mkuu, ni kipindi gani(umri) kwenye maisha yako kilikuwa bora sana kwa wakati wote uliyoishi paka sasa?
 
Mkuu, ni kipindi gani(umri) kwenye maisha yako kilikuwa bora sana kwa wakati wote uliyoishi paka sasa?

Hakuna kipindi kizuri na kumbukumbu nzuri kama wakati mpo wadogo na kukua mkiwa nyumbani na ndugu zako
Hii ni furaha na majonzi pia nikikumbuka maisha yale

Ila baada ya hapo niliondoka na kuanza maisha yangu nikiwa na 20
Maisha hayo yalikuwa mazuri sana pia kwani nilijitegemea kwa kila kitu na kuweza kuiona dunia sana

Nimesafiri na kuziona nchi 32
Kwa kweli siyajutii maisha na sasa bado naishi vizuri tu sijawahi kupata dhiki namshukuru Mungu

Ingawa changamoto za hapa na pale
 
Hakuna kipindi kizuri na kumbukumbu nzuri kama wakati mpo wadogo na kukua mkiwa nyumbani na ndugu zako
Hii ni furaha na majonzi pia nikikumbuka maisha yale

Ila baada ya hapo niliondoka na kuanza maisha yangu nikiwa na 20
Maisha hayo yalikuwa mazuri sana pia kwani nilijitegemea kwa kila kitu na kuweza kuiona dunia sana

Nimesafiri na kuziona nchi 32
Kwa kweli siyajutii maisha na sasa bado naishi vizuri tu sijawahi kupata dhiki namshukuru Mungu

Ingawa changamoto za hapa na pale
Vyema sana kiongozi na mungu azidi kukuweka
 
Nataka nizeeke vizuri Yani, Yani jibibi shangingi Kama Da Kasie 😂 At that age nitakuwa nimestaafu, naota kwenda Hija Mecca na mpenzi wangu sana Insha'Allah.....
Napenda kusafiri, natamani huo uwe muda wa kufanya utalii wa ndani....kutunza bustani, navyopenda kupika itakuwa ni Muda wangu wa kupika vyakula mbalimbali....Namuomba Mungu anipe umri.
 
Back
Top Bottom