Uzembe na uswahili kwenye ofisi za umma ngazi ya elimu umerudi. Inasikitisha sana

Uzembe na uswahili kwenye ofisi za umma ngazi ya elimu umerudi. Inasikitisha sana

MR KUO

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2016
Posts
2,678
Reaction score
3,818
Kipindi cha awamu ya chuma,jiwe tulishuhudia huduma bomba sana kwa watumishi wa umma ngazi zote, kuanzia chini hadi juu, ila baada ya kuondoka inaonekana kaondoka na vyote mapanya buku yametawala baada ya paka kusepa.

Majuzi hapa nilienda shule x kuomba nafasi ya uhamisho kwa kijana wangu wa kidato cha kwanza, nikaonana na mkuu wa shule nikajieleza shida yangu vema, yeye akaniambia hapa nafasi hakuna kabisa jaribu shule ya jilani hapo na alirudia zaidi ya mara 5 kunielekeza kwenye hiyo shule huku akiisifia hadi nikapata mashaka, ila kwa sababu mimi nilikuwa nimeona panapomfaa kijana ni pale pale nikaomba anifanyie vyovyote kijana ahamie, akanitazama kwanza kisha akaniambia sawa nitakusaidia ukitaka aje lipia hela ya dawati, nikauliza sh ngapi akaniandikia kwenye karatasi kiasi cha 120,000/=, nilishtuka ila nikaficha mshituko ikabidi nijifanye naomba huruma akaniambia haiwezekani vinginevyo fanya nilivyokwambia,nikasema kiasi hicho sina kwa sasa,akaniambia kama vipi nije kesho yake ili nionane na fundi wake tuone tunafanyaje ikiwezekana nilipie kwa awamu, kumbe kesho yake yenyewe hatakuwa ofisini kutwa nzima, nilikuja kugundua maana hata mimi nilipata dharula nikaitwa ofisi ya mkurugezi manispaa kwa shughuli zangu,

Ile namaliza naondoka tukakutana nikamsalimia vema tukatoka mazingira ya ofisi nikakumbushia jambo langu na yeye akakomalia kiasi hicho, sasa sijui ikawaje wakati tunaondoka kwa mguu nikapigiwa simu nirudi ofisini, ikabidi nimuage narudi, nikarudi nikamalizana nao ile naondoka pia nikakumbuka si kuna maafisa elimu hapa ngoja niwachek, nikamchek afisa elimu sekondar nikamweleza namna nilivyokwama kutokana na ghalama ya kununua dawati.

Akauliza maswali nikamtajia vyote akashtuka kisha akampigia simu mkuu wa shule, wakaongea kama dakika 20 nikaona hapa huenda nimelipua liziki za watu nikawa na hofu fulani aisee.ile anamaliza kuongea akaniambia amemalizana na mkuu wa shule kesho nirudi shuleni tuelewane anionyeshe dawati ambalo ni bovu nitengeneze mtoto ahamie, kesho yake nikaenda kweli cha ajabu mkuu wa shule akaruka vyote akadai hawajaongea hivyo.dah nilichoka nikajisemea hawa tayari tushapishana kimawasiliano haina haja ya kurudi tena hapa nikaaga na kuondoka.

Napanga kumtafutia shule nyingine ila nimechukia na kusikitika sana.

How come mtu ana shida ya kiofisi na wewe unamwambia njoo kesho siku ambayo unajua hautakuwepo ofisini hivi unafikiria ghalama anazoingia katika muda wake, pesa zake n.k??

Nimechukia sio kidogo.
 
Kipindi cha awamu ya chuma,jiwe tulishuhudia huduma bomba sana kwa watumishi wa umma ngazi zote, kuanzia chini hadi juu, ila baada ya kuondoka inaonekana kaondoka na vyote mapanya buku yametawala baada ya paka kusepa.

katika muda wake, pesa zake n.k??

Nimechukia sio kidogo.
Wewe ni umasikini ndo unao kusumbua watu tunalipia mpaka 700k kuhamisha mtoto shule unao ona atafaulu wewe unalilia 120k mkuu hi ni Tanzania watumishi na viongozi ni wale wale siku zote,........toa pesa mwanao asome kama ni wakwako kweli.
 
Kama unaona Elimu ni gharama jaribu ujinga.

Unampeleka mtoto shule akakae kwenye meza na kiti cha nani?.
 
Kwa sasa kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake....pesa sabuni ya roho
 
Nyie mnadharau hao walimu Wana mishahara midogo kuliko nyie, Sasa nyie wenye mishahara mikubwa mmeombwa 120 tu ya dawati mnafungua adi nyuzi.
 
Nyie mnadharau hao walimu Wana mishahara midogo kuliko nyie, Sasa nyie wenye mishahara mikubwa mmeombwa 120 tu ya dawati mnafungua adi nyuzi.
Nadhani hujasoma andiko langu kwa jicho la tatu, mwalimu tangu mwanzo kaonyesha hata nikizilipa haliwezi kutengenezwa hilo dawati, kingine sasa mpango wa elimu bure kwa shule za serikal una maana gani??.

Hiyo hela ni ndogo sana sema mazingira ya kuidai ndo yamenitia mashaka.

Any ways mishahara yao kuwa midogo sio kosa la yoyote kila mtu anakula anakopeleka mboga.
 
Kama unaona Elimu ni gharama jaribu ujinga.

Unampeleka mtoto shule akakae kwenye meza na kiti cha nani?.
Wewe ulilipia vyote? Au nyie ndo wale hamuwezi kuhoji lolote lile kila kitu ni sawa sawa kama mawatu yanayopewa kofia na khanga za lile lichama?
 
Wewe ni umasikini ndo unao kusumbua watu tunalipia mpaka 700k kuhamisha mtoto shule unao ona atafaulu wewe unalilia 120k mkuu hi ni Tanzania watumishi na viongozi ni wale wale siku zote,........toa pesa mwanao asome kama ni wakwako kweli.
Sasa si inategemea? Huenda wewe unamtoa shule za binafis kwenda binafis, mkoa kwenda mkoa.

Mimi ni kata kwa kata mjini hapa.
 
Kipindi cha awamu ya chuma,jiwe tulishuhudia huduma bomba sana kwa watumishi wa umma ngazi zote, kuanzia chini hadi juu, ila baada ya kuondoka inaonekana kaondoka na vyote mapanya buku yametawala baada ya paka kusepa.

Majuzi hapa nilienda shule x kuomba nafasi ya uhamisho kwa kijana wangu wa kidato cha kwanza, nikaonana na mkuu wa shule nikajieleza shida yangu vema, yeye akaniambia hapa nafasi hakuna kabisa jaribu shule ya jilani hapo na alirudia zaidi ya mara 5 kunielekeza kwenye hiyo shule huku akiisifia hadi nikapata mashaka, ila kwa sababu mimi nilikuwa nimeona panapomfaa kijana ni pale pale nikaomba anifanyie vyovyote kijana ahamie, akanitazama kwanza kisha akaniambia sawa nitakusaidia ukitaka aje lipia hela ya dawati, nikauliza sh ngapi akaniandikia kwenye karatasi kiasi cha 120,000/=, nilishtuka ila nikaficha mshituko ikabidi nijifanye naomba huruma akaniambia haiwezekani vinginevyo fanya nilivyokwambia,nikasema kiasi hicho sina kwa sasa,akaniambia kama vipi nije kesho yake ili nionane na fundi wake tuone tunafanyaje ikiwezekana nilipie kwa awamu, kumbe kesho yake yenyewe hatakuwa ofisini kutwa nzima, nilikuja kugundua maana hata mimi nilipata dharula nikaitwa ofisi ya mkurugezi manispaa kwa shughuli zangu,

Ile namaliza naondoka tukakutana nikamsalimia vema tukatoka mazingira ya ofisi nikakumbushia jambo langu na yeye akakomalia kiasi hicho, sasa sijui ikawaje wakati tunaondoka kwa mguu nikapigiwa simu nirudi ofisini, ikabidi nimuage narudi, nikarudi nikamalizana nao ile naondoka pia nikakumbuka si kuna maafisa elimu hapa ngoja niwachek, nikamchek afisa elimu sekondar nikamweleza namna nilivyokwama kutokana na ghalama ya kununua dawati.

Akauliza maswali nikamtajia vyote akashtuka kisha akampigia simu mkuu wa shule, wakaongea kama dakika 20 nikaona hapa huenda nimelipua liziki za watu nikawa na hofu fulani aisee.ile anamaliza kuongea akaniambia amemalizana na mkuu wa shule kesho nirudi shuleni tuelewane anionyeshe dawati ambalo ni bovu nitengeneze mtoto ahamie, kesho yake nikaenda kweli cha ajabu mkuu wa shule akaruka vyote akadai hawajaongea hivyo.dah nilichoka nikajisemea hawa tayari tushapishana kimawasiliano haina haja ya kurudi tena hapa nikaaga na kuondoka.

Napanga kumtafutia shule nyingine ila nimechukia na kusikitika sana.

How come mtu ana shida ya kiofisi na wewe unamwambia njoo kesho siku ambayo unajua hautakuwepo ofisini hivi unafikiria ghalama anazoingia katika muda wake, pesa zake n.k??

Nimechukia sio kidogo.
Wahenga wanasema ofisi haihami....yupo kaimu
 
Umefanya busara sana kutokumpeleka mwanao hapo ht baada ya mambo kukaa vzr, mana ungesikia mwanao kavunjwa mgongo kisa kuchapwa na mwalimu kisa kosa fulani.
 
Umefanya busara sana kutokumpeleka mwanao hapo ht baada ya mambo kukaa vzr, mana ungesikia mwanao kavunjwa mgongo kisa kuchapwa na mwalimu kisa kosa fulani.
Yaani,niliona kulazimisha kumpeleka ni kununua matatizo mengine yasiyo ya msingi maisha haya amani ni bora kuliko ushindi.
 
Nyie mnadharau hao walimu Wana mishahara midogo kuliko nyie, Sasa nyie wenye mishahara mikubwa mmeombwa 120 tu ya dawati mnafungua adi nyuzi.
Kila mtu anakula kadiri ya urefu wake, unaleta mastori ya zama za mawe.
Na una madili mpaka na Mkurugenzi!
Ingejuwa TRA angetoa, kwa kuwa ni ticha analalama.
Anakimbilia kwa Afisa Elimu bila kujua maafisa wanategemea toka kwa wakuu wa shule, walizokusanya kwa wazazi kama yeye ili 'waaishi kifahari' town.
Hapo mkuu wa shule amekomaa kuisuka staff na watoto wanafaulu wewe unataka vya bure, mkuu alikushauri vyema ..... shule zipo nyingi
 
Kila mtu anakula kadiri ya urefu wake, unaleta mastori ya zama za mawe.
Na una madili mpaka na Mkurugenzi!
Ingejuwa TRA angetoa, kwa kuwa ni ticha analalama.
Anakimbilia kwa Afisa Elimu bila kujua maafisa wanategemea toka kwa wakuu wa shule, walizokusanya kwa wazazi kama yeye ili 'waaishi kifahari' town.
Hapo mkuu wa shule amekomaa kuisuka staff na watoto wanafaulu wewe unataka vya bure, mkuu alikushauri vyema ..... shule zipo nyingi
Sasa yote hayo ndo matakwa ya kazi zake???.

Na kusema shule zipo nyingi hiyo ya kwake??

Na uhakika wa madawati ndo uhakika wa ufaulu??

Ukute wewe ndo huyo mkuu wa shule njaa zitawaua nyie aisee ndo maana kazi ya ualimu inadharauliwa kutokana na watu wazembe kama nyie.

Kila shule si inapokea fungu la bajeti kutoka serikalini zinaenda wapi??

Ni bora hata angeniambia kwa njia ya kirafiki ningemuelewa sio kwa mazingira hayo.

Okay ushasema sasa kuna muunganiko wa kiulaji kati ya maafisa elimu na wakuu wa shule...... umenifungua mwanga hapa asante sana.
 
Back
Top Bottom