Uzi kwa tuliowahi kutapeliwa au kuibiwa.ebu tuje hapa tukumbuke.mimi nakumbuka kko niliuziwa matambala

Uzi kwa tuliowahi kutapeliwa au kuibiwa.ebu tuje hapa tukumbuke.mimi nakumbuka kko niliuziwa matambala

ommytk

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2015
Posts
520
Reaction score
1,143
Matapeli au wezi ni watu wenye akili sana kwenye kazi yao mimi nakumbuka kwenye miaka 90 hivi nilienda kko kununua nguo sikukuu basi nikakuta suruali nzuri ya kitambaa jamaa kaishika anauza nikaipenda akanipa bei basi natoa hela akawa anafunga kwenye mfuko karatasi zamani ilikuwa mifuko karatasi kama bahasha za kaki basi nikaondoka kufika nyumbani matambala yaani nikabaki kucheka tu.ebu nawe njoo na kisa chako
 
Mimi nikiwa mdogo darasa la pili nilitumwa mafuta ya taa sheli. Sasa sheli niliyo agizwa sikujua naipataje kwa ule mda. Nikakutana na jamaa flani alikua na umri wa kuguess kama 20's ivi nikamuuliza sheli ikowapi?
Akaniuliza "unataka ukafanyaje?"
Nikamjibu kama nilivyo agizwa akaniambia nimfwate tukatembea kidogo
Akaniambia iyo sheli huwa huwahudumii watoto
Kwaio nimpe hela akaniletee
Nikampatia dumu la mafuta na pesa 10k.
Chaku sikitisha sasA. Mpaka leo ajarudigi sijui alienda sheli za Mars!
 
Miaka hio,kuna jamaa alienda wanapouza mkaa kwenye magunia,yale makubwa kipindi hicho. Akambebesha lile gunia akamwambia twende pesa ipo nyumbani, wametembea wakafika sehemu kuna hardware, jamaa akamwambia muuza mkaa kama una pesa hapo nipe ninunue cement walete home, hela ya mkaa na hii nakupa home,jamaa akatoa mauzo yote, safari ikaendelea.

Sasa sisi asub hio niko bro na Mzee, tunakuta mtu mmoja anatua mkaa njee,mwingine kaingia,akaanza uliza kuna vyumba vya kupanga hapa,tukamjibu hatupangishi ila kuna jirani hapa kaangalie,tunatoka tunamwonesha hio nyumba, yule wa mkaa kakalia tu gunia. Yule jamaa akaenda akaongea kidogo na yule wa mkaa akawa anaondoka.

Kama lisaa mbele tunakuta wa Mkaa anagonga getini anauliza mbona kaka yenu harudi na mkaa amwingizi ndani. Kumbe jamaa alimwambia pale ni kwao na Muda ule tumetoka tunamwelekeza nyumba ya jirani, ndio ule Muda akamfuata jamaa akamwambia baba ananituma nyumba ile,maana wakatianamwelekeza alikua anainyoshea kidole
 
Mimi nikiwa mdogo darasa la pili nilitumwa mafuta ya taa sheli. Sasa sheli niliyo agizwa sikujua naipataje kwa ule mda. Nikakutana na jamaa flani alikua na umri wa kuguess kama 20's ivi nikamuuliza sheli ikowapi?
Akaniuliza "unataka ukafanyaje?"
Nikamjibu kama nilivyo agizwa akaniambia nimfwate tukatembea kidogo
Akaniambia iyo sheli huwa huwahudumii watoto
Kwaio nimpe hela akaniletee
Nikampatia dumu la mafuta na pesa 10k.
Chaku sikitisha sasA. Mpaka leo ajarudigi sijui alienda sheli za Mars!
Aisee ulirudije home mkuu? Hujachezea kichapo kwa bi mkubwa😂
 
Miaka hio,kuna jamaa alienda wanapouza mkaa kwenye magunia,yale makubwa kipindi hicho. Akambebesha lile gunia akamwambia twende pesa ipo nyumbani, wametembea wakafika sehemu kuna hardware, jamaa akamwambia muuza mkaa kama una pesa hapo nipe ninunue cement walete home, hela ya mkaa na hii nakupa home,jamaa akatoa mauzo yote, safari ikaendelea.

Sasa sisi asub hio niko bro na Mzee, tunakuta mtu mmoja anatua mkaa njee,mwingine kaingia,akaanza uliza kuna vyumba vya kupanga hapa,tukamjibu hatupangishi ila kuna jirani hapa kaangalie,tunatoka tunamwonesha hio nyumba, yule wa mkaa kakalia tu gunia. Yule jamaa akaenda akaongea kidogo na yule wa mkaa akawa anaondoka.

Kama lisaa mbele tunakuta wa Mkaa anagonga getini anauliza mbona kaka yenu harudi na mkaa amwingizi ndani. Kumbe jamaa alimwambia pale ni kwao na Muda ule tumetoka tunamwelekeza nyumba ya jirani, ndio ule Muda akamfuata jamaa akamwambia baba ananituma nyumba ile,maana wakatianamwelekeza alikua anainyoshea kidole

Mkuu nimesoma kwa utulivu wa hali ya juu hata sijaelewa
 
Back
Top Bottom