Uzi Maalulm wa Makocha wa Soka

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,170
Reaction score
7,665
Kwa wapenzi wa Mchezo wa mpira wa miguu huu ni uzi special kwa ajili ya Waalimu wa mpira wa miguu maarufu kama Coach

Kupitia Uzi huu utapata kujua Habari mbalimbali za makocha Duniani katika timu za mataifa mbalimbali,vilabu mbalimbali duniani

Pia tutajadiri mifumo wanayotumia katika ufundishaji wao ,madhara ya mfumo wake katika timu husika na uzuri wa mfumo wake katika timu aliopo! Mbinu mbalimbali za makocha na aina yao ya utengenezaji na uundaji wa timu husika

Pia tutapata kujua taarifa mbali mbali za makocha ikiwamo na sababu zinazomfanya kuitwa na timu fulani,kufukuzwa na timu fulani pamoja na mapendekezo kwa timu husika ni kocha gani angee Faa!

Hatuwezi ongelea kocha yeyote duniani lakini Wale wenye kufanya vizuri na wenye mafanikio watajadiriwa sana!

Kifupi ni uzi utakao husu taarifa mbalimbali za Makocha hapa duniani!

Karibu wachambuzi na wapenzi wa soka!
 
Mnawajadili makocha wa Ulaya kwa faida ya nani kwa mfano?
Humu mnaitwa GreatThinkers, mnachokijadili walau kiwe na faida basi, sio kujifurahisha tu...
 
Mnawajadili makocha wa Ulaya kwa faida ya nani kwa mfano?
Humu mnaitwa GreatThinkers, mnachokijadili walau kiwe na faida basi, sio kujifurahisha tu...
Hata makocha wa bongo pia watajadiliwa haijabagua
 
nami pia nijadiliwe ni kocha wa timu ya kijiji.
 
Hata wewe unaedhani ni great thinker hakuna kitu hapo; mtoa mada kasema makocha duniani we umeshadakia ulaya. Kwani ulaya ndo duniani? Try to think big before yelling shit.
Sikumjibu mtoa mada, nimewajibu wachangiaji walioanza kuchambua akina Morinyo... Unataka tutukanane?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…