Uzi Maalum wa Jinsi ya Kutoa Huduma ya Kwanza kwa matatizo mbalimbali kabla ya kufika hospitali

Uzi Maalum wa Jinsi ya Kutoa Huduma ya Kwanza kwa matatizo mbalimbali kabla ya kufika hospitali

Jaluo_Nyeupe

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2010
Posts
2,824
Reaction score
2,264
Habari zenu wana JF,

Ni wazi kwamba watu wengi hatuna elimu ya kutosha jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa wapendwa wetu pindi wanapopata matatizo mbali mbali ya kiafya kabla ya kuwapeleka hospitali. Wakati mwingine mtu anaweza kupata tatizo litakalomfanya aweze kudumu kwa dakika chache tu bila kupata huduma ya kwanza.

Hali hiyo imepelekea watu kupoteza maisha wakiwa njiani kupelekwa hospitali au kupata ulemavu wa kudumu pengine kutokana na namna ya ubebaji au ukaaji akiwa njiani kupelekwa hospitali.

Hivyo basi nawakaribisha watu (wataalamu) mbali mbali wanaojua jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa matatizo mbali mbali kama:-
  1. Kuzimia.
  2. kuanguka ghafla kutokana na maradhi mbalimbali mf. presha, kisukari nk.
  3. kuumwa na nyoka
  4. kupigwa shoti ya umeme
  5. kupata jeraha linalota damu nyingi
  6. kuungua moto
  7. kushindwa kupumua
  8. kupata ajali
  9. kupaliwa/kwikwi mfululizo
  10. kukwamwa na kitu katika njia ya hewa au chakula (mf. mtoto kumeze sarafu au kisoda)
  11. kunywa sumu au chochote kisichofaa (mf. mtoto kunywa dawa kimakosa au mafuta ya taa)
  12. kuingiwa na sumu au chochote kisichofaa machoni.
  13. kuzama kwenye maji ya kina kirefu na kunywa maji mengi.
  14. kuchomwa na kitu chenye ncha kali kisipokuwa/kikiwa bado ndani ya mwili wako
  15. Shambulio la moyo
  16. Kutapika/kuharisha mfululizo
  17. .....
  18. ......
  19. ......
  20. .......
Mimi nitaanza na namba nne, KUPIGWA SHOTI YA UMEME.
Endapo mtu kapigwa shoti ya umeme unachotakiwa kufanya cha kwanza ni kuzima chanzo cha umeme kama kipo karibu na kinafikika kwa urahisi, hapa nazungumzia main switch. Kama chanzo kipo mbali au hakifikiki kwa urahisi unachotakiwa kufanya ni kumtoa muhanga kwenye eneo tukio ili asiendelee kupata madhara kwa kutumia kitu kikavu kisichopitisha umeme kwa mfano mti mkavu. Kamwe usimshike kwa mikono (bare hands) kwani na wewe kuna uwezekano ukapigwa shoti kupitia mwili wake. Mcheki kama anapumua kawaida na kama anashindwa msaidie kwa kumlaza chali huku wewe ukiwa umepiga magoti na kumkandamiza na kuachia (kama mtu anavyohema) kifuani kwa viganja vyako (tizama kiambatanisho). Kama bado hawezi kupumua, njia nyingine ambayo si salama sana kiafya hasa kipindi hiki cha UVIKO19 ni hii. Mpanue mdomo huku ukimziba pua, weka mdomo wako kwenye mdomo wake na kumpulizia pumzi (mouth to mouth inhalation). Kisha endelea kumgandamiza kifua na kuachia mpaka pale atakapoanza kupumua. Baada ya hapo mpeleke hospitali kwa matibabu zaidi.

Karibuni.


CPR.png
 
Habari zenu wana JF,

Ni wazi kwamba watu wengi hatuna elimu ya kutosha jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa wapendwa wetu pindi wanapopata matatizo mbali mbali ya kiafya kabla ya kuwapeleka hospitali. Wakati mwingine mtu anaweza kupata tatizo litakalomfanya aweze kudumu kwa dakika chache tu bila kupata huduma ya kwanza.

Hali hiyo imepelekea watu kupoteza maisha wakiwa njiani kupelekwa hospitali au kupata ulemavu wa kudumu pengine kutokana na namna ya ubebaji au ukaaji akiwa njiani kupelekwa hospitali.

Hivyo basi nawakaribisha watu (wataalamu) mbali mbali wanaojua jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa matatizo mbali mbali kama:-
  1. Kuzimia.
  2. kuanguka ghafla kutokana na maradhi mbalimbali mf. presha, kisukari nk.
  3. kuumwa na nyoka
  4. kupigwa shoti ya umeme
  5. kupata jeraha linalota damu nyingi
  6. kuungua moto
  7. kushindwa kupumua
  8. kupata ajali
  9. kupaliwa/kwikwi mfululizo
  10. kukwamwa na kitu katika njia ya hewa au chakula (mf. mtoto kumeze sarafu au kisoda)
  11. kunywa sumu au chochote kisichofaa (mf. mtoto kunywa dawa kimakosa au mafuta ya taa)
  12. kuingiwa na sumu au chochote kisichofaa machoni.
  13. kuzama kwenye maji ya kina kirefu na kunywa maji mengi.
  14. kuchomwa na kitu chenye ncha kali kisipokuwa/kikiwa bado ndani ya mwili wako
  15. Shambulio la moyo
  16. Kutapika/kuharisha mfululizo
  17. .....
  18. ......
  19. ......
  20. .......
Mimi nitaanza na namba nne, KUPIGWA SHOTI YA UMEME.
Endapo mtu kapigwa shoti ya umeme unachotakiwa kufanya cha kwanza ni kuzima chanzo cha umeme kama kipo karibu na kinafikika kwa urahisi, hapa nazungumzia main switch. Kama chanzo kipo mbali au hakifikiki kwa urahisi unachotakiwa kufanya ni kumtoa muhanga kwenye eneo tukio ili asiendelee kupata madhara kwa kutumia kitu kikavu kisichopitisha umeme kwa mfano mti mkavu. Kamwe usimshike kwa mikono (bare hands) kwani na wewe kuna uwezekano ukapigwa shoti kupitia mwili wake. Mcheki kama anapumua kawaida na kama anashindwa msaidie kwa kumlaza chali huku wewe ukiwa umepiga magoti na kumkandamiza na kuachia (kama mtu anavyohema) kifuani kwa viganja vyako (tizama kiambatanisho). Kama bado hawezi kupumua, njia nyingine ambayo si salama sana kiafya hasa kipindi hiki cha UVIKO19 ni hii. Mpanue mdomo huku ukimziba pua, weka mdomo wako kwenye mdomo wake na kumpulizia pumzi (mouth to mouth inhalation). Kisha endelea kumgandamiza kifua na kuachia mpaka pale atakapoanza kupumua. Baada ya hapo mpeleke hospitali kwa matibabu zaidi.

Karibuni.


Namba 1 aliyezimia
Huduma ya kwanza

Mlaze chali mgonjwa.
Legeza nguo zake zote, shingoni, kifuani na kiunoni.
Mpatie mgonjwa hewa nyingi safi na zuia watu kusonga.
Mpepee ili kumpatia hewa nyingi zaidi.
Mnawishe uso wake kwa maji safi kama yanapatikana.
Baada ya muda wa dakika 30 kupita bila matokeo, mpeleke mgonjwa zahanati.
Hizi ni bahazi ila zinamanufaha kumpatia mgonjwa

Namba 4 Kuunguwa kwa moto mpake asali.

Namba 16 Dawa ya kuzuia kutapika kunywa chai ya Tangawizi Dawa ya kuzuia kuharisha koroga kijiko 1 cha unga wangano unywe.
 
Back
Top Bottom