Uzi maalumu kwa Vituko vyako vya utotoni mpaka la STD 7!

Kuna kipindi cha nyuma tulikuwa darasa la nne shule yetu ilikuwa na shamba la machungwa. Tukazama manunda watatu katikati ya shamba kuiba machungwa sasa ile tumevuna kama machungwa kumi tukamwona dada mmoja anajisaidia haja kubwa sasa kwa akili yetu ya utoto tukamfuata na kuanza kumkimbiza as if ni kibaka baadae yule dada akasimama akatuomba tumsamehe baadae tukajiuliza kati ya yeye na sisi nani amefanya kosa ikabidi tumwachie aende zake. Yule dada sasa hivi ni mhenga mwenzangu tukikutana inabidi niangalie chini ingawa imepita miaka mingi sana
 
Kukojoa kitandani..ilinitesa sana hii..nilichekwa na nilichapwa sana na nilijitahidi kuacha ila nikashindwa..mpk leo mtt akikojoa kitandani simpigi cuz naelewa wanapitia nilikopitiaga na ipo siku wataacha...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaman mm nlikuwa mshari. Kwanza nlikuwa mdogo kuliko wote shule. Then nlikuwa mtundu kuliko shule nzima, nlikuwa napigana na watu wakubwa ie la saba wkt nikiwa la 3, nlikuwa bingwa wa kupigana na kundi la watu wengi mf. Darasa zima. Nikibeba panga nikinyanyua linashuka nanbega sikuwa natania. Hivyo nlikuwa tishio. Mfukoni nlikuwa na seti nzima ya topaz yaan huku tano na huku tano. Halafu nlikuwa natembea na visu kwa ajili ya kupigania. Nikiwa A level nlipigana na mabweni 2 nikashinda na zaidi ya wanafunzi 17 walilazwa na kushonwa nyuzi za kutosha tu sababu nlikuwa na square pipe niloivunja kutoka kwenye dawati na mbele ilikuwa imechmwa misumari. Hivyo nlikuwa napiga na kuivuta inachana kama ni kichwa ama tumbo mi sio kazi yangu. In short nliogopeka from thet day

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uwiiiiiiii babu sasa huko ulipo sipo naomba urudi nyumbani lasivo kesho nitakuja hapo nikupeleke muhimbili........sio bure
Basi sawa... ngoja basi nipokee simu then narudi fasta..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…