View: https://m.youtube.com/watch?v=Qc7M0ljsAXI&pp=ygUYZmF1bGF0YSBqdXdhdGEgamF6eiBiYW5k
[FAULATA - Juwata Jazz Band]
(Kibao kimeimbwa naye mwenyewe Joseph Lusungu , Moshi William, Suleiman Mbwembwe, Joseph Maina,
Juma Akida Hamisi Kitambi na Tino Masenge, solo chini yake Mabera, rythim na Pishuu, bass na Issa Ramadhani,
drums kucharazwa na Saidi Mohamed, Mohamed Haroub kwenye tumba, Julius Betto na Zitto Mbunda kwenye trumpets,
Mnenge, Abdi Mketema na Hagai Kauzeni kwenye midomo ya bata (sax) )
(Mwanzo)
Ilikuwa siku ya jumanne asubuhi
nataka kwenda kazini
ndipo ulipotamka neno kuwa umechokaa
kuishi na mimi
kosa gani eh
ewe Faulata
sikupata jibu jengine ila sikutaki eh
sikutaki tuuu
kuchunguza kuchunguza kumbeeeeee
umempata awezae kumiliki maisha yako
kunishinda mimi
[wote] Kibwagizo
ama kweli oh maradhi yote ugua
lakini kuchacha usiombee
[Lusungu]
naomba unisikile kwa makini
haya ninayokuambia
kuibuka na kuchacha mola ndiye mpangaji wa yotee
[wote] kibwagizo
[Lusungu]
umekuwa kama mzigo wa moto ..... lo salale
haubebeki wala haushiki
nakuruhusu wendee ....... nenda
utaiona dunia eh
[wote] kibwagizo