UZINDUZI: Juzuu la ‘Rai ya Jenerali’ - Agosti 6, 2021

UZINDUZI: Juzuu la ‘Rai ya Jenerali’ - Agosti 6, 2021

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
B4F41326-0209-4877-873F-4956340A0ABE.jpeg


Juzuu hii ina makala moto na ngumu zinazohusu mambo makubwa yaliyowahi kufanyika nchini na ambayo hakuna Mwandishi yeyote aliyewahi kuthubutu kuyasimulia.

Ni shuhuda za mwandishi wa habari mahiri katika bara la Afrika anayeheshimika duniani pote akisimulia mambo makubwa yaliyofanyika katika awamu zote tangu Uhuru wa Nchi hii na pengine hayajawahi kusimuliwa na mwandishi yeyote, yakiwemo vuguvugu la Katiba Mpya la mwaka 2011 na kuundwa kwa G55.

Je, ni wakina nani waliounda kundi hilo?
Je, ni kweli hilo kundi lilikuwa na watu 55?

Kitabu hicho kimesheheni hazina ya taarifa za uchunguzi zinazohusu mambo makubwa ya siasa za Tanzania yakisimuliwa na kuandikwa na mwanaharakati wa miongo minne asiyeyumba wala kuyumbishwa, Jenerali Twaha Ulimwengu!

Pata nakala ya Juzuu la “Rai ya Jenerali” uwajue mashujaa waliosimama kidete kutaka Katiba Mpya na hatma yao.

Juzuu hilo lenye kurasa 234 na makala 37 tayari liko Mtaani kwa bei ya Tsh. 30,000/- tu. Zinatolewa nafasi kwa vijana wenye mtaji wa vitabu kuanzia vitano wanaotaka kujiajiri mahali popote Tanzania kuwasiliana na wasambazaji.

Kuhusu Uzinduzi

Uzinduzi wa Juzuu la “Rai ya Jenerali” utafanyika Agosti 6, 2021. Mgeni Rasmi ni Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba, Mwenyekiti wa Tume ya mchakato wa Katiba Mpya 2011, Waziri Mkuu Wa Tanzania 1985 -1990 na Jaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki.

Juzuu au kitabu kimewekewa sahihi za heshima na Profesa Mark Mwandosya, Dkt. Martha Qorro, Dkt. Azaveli Lwaitama na wengineo.
 
General ulimwengu zao bora kabisa LA chama chamapinduzi

Ile kanuni ilimkaa yakutokuongea uongo daima

Ccm yenye uwezo wakuhoji na kujibu hoja iliishia pale kwa uvccm ya nape nauye
Hata ikishindwa kujibu kikamilifu ilikua na mbinu moja Kali sana kuonyesha imejibu hoja

Hii yasasa sijui inahali mbaya
 
Nchi za kiafrika tuna laana!!yaani MIDUDE kama hii, inawekwa pembeni na mifumo kutokana na misimamo yao ya kutokuwa minafiki!!jamaa alishawahi kukataa uhamisho wa u DC, nadhani kutoka wilaya ya hai kuja ilala!!na akaachana nao!!
 
mwendazake kuandika hakuweza, aliamuru wizara imuandikie mapambio na nyimbo za majisifu aliyoyaita historia mpya ya Tanzania
Tumuache Mwendazake. Mtu kama yule ni nadra sana kutokea duniani. Dunia ina watu wachache wa aina ile. Tusimchukulie poa.
Jamaa alitufanya wote tuwe kama mazombie. Tumeufyata. Tumeanza kuongea baada ya yeye kufa
 
Tumuache Mwendazake. Mtu kama yule ni nadra sana kutokea duniani. Dunia ina watu wachache wa aina ile. Tusimchukulie poa.
Jamaa alitufanya wote tuwe kama mazombie. Tumeufyata. Tumeanza kuongea baada ya yeye kufa
Walikuwepo zaidi ya yeye ndugu. He was a typical tyrant na Wana tabia zinafanana.

Angalia akina Hitler, Pinochet Duterte and the like, Wana tabia ya kutooenda kukosolewa na wanaaminisha wananchi wao kwamba ni wao tu ndio wanaweza kuwaletea wananchi maendeleo na wanaaminisha kwamba ili muendelee mnapasws kutokuwa na mawazo mbadala wa kiongozi huyo.

The guy was non than a tyrant, hakutaka mtu awe maarufu zaidi yake na alitaka mawazo yake ndio yatawale vichwani mwa watanzania. Hakutaka kabisa mtu ajitokeze kuleta policies na theories mpya tofauti na zake.

It's normal kwa tyrants kuweka alama fulani kwenye taifa wanaoongoza ili kuwaaminisha wananchi kwamba kiongozi huyo ndio anafaa, mathalani wanahakikisha wanajesga alama fulani kama shule,kilimo au hospital au matibabu wanaweka bure na elimu bure ili muone kwamba bila wao maisha yatakuwa magumu. Hii yote wanafanya kuwahadaa ili waendelee kuwatawala unakutanhakuna mawazo mbadala, hakuna Uhuru wa Mambo kibao na anaua wapinzania wake.

So kwangu mimi naona he was just another tyrant.
 
Kwa hakika maandiko ya Generali yamesheheni ubobevu na umakini mkubwa, si cha kukosa kitabu hiki.
 
Walikuwepo zaidi ya yeye ndugu. He was a typical tyrant na Wana tabia zinafanana.

Angalia akina Hitler, Pinochet Duterte and the like, Wana tabia ya kutooenda kukosolewa na wanaaminisha wananchi wao kwamba ni wao tu ndio wanaweza kuwaletea wananchi maendeleo na wanaaminisha kwamba ili muendelee mnapasws kutokuwa na mawazo mbadala wa kiongozi huyo.

The guy was non than a tyrant, hakutaka mtu awe maarufu zaidi yake na alitaka mawazo yake ndio yatawale vichwani mwa watanzania. Hakutaka kabisa mtu ajitokeze kuleta policies na theories mpya tofauti na zake.

It's normal kwa tyrants kuweka alama fulani kwenye taifa wanaoongoza ili kuwaaminisha wananchi kwamba kiongozi huyo ndio anafaa, mathalani wanahakikisha wanajesga alama fulani kama shule,kilimo au hospital au matibabu wanaweka bure na elimu bure ili muone kwamba bila wao maisha yatakuwa magumu. Hii yote wanafanya kuwahadaa ili waendelee kuwatawala unakutanhakuna mawazo mbadala, hakuna Uhuru wa Mambo kibao na anaua wapinzania wake.

So kwangu mimi naona he was just another tyrant.
And yet, wameacha kumbukumbu ambazo wachache sana wanaacha. Mwendazake ameenda. Tugange yaliyopo na yajayo
 
Back
Top Bottom