Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Leo Julai 26, 2019 Mhe. Rais Magufuli atakuwa mgeni rasmi kwenye uwekaji jiwe la msingi la mradi wa kuzalisha umeme katika mto Rufiji
Rais Magufuli aliwasili Rufiji akitokea Dar es Salaam akitumia treni ya reli ya TAZARA kwa kupitia Fuga na Kisaki
UPDATE:
Waziri wa Nishati, Medard Kalemani;
Rais ulipotuita Ikulu kutueleza ndoto yako kuhusu mradi huu, wengi hatukuelewa lakini sasa tumeanza kukuelewa. Mradi huu utatekelezwa kwa miezi 42 na mpaka sasa umeshatekelezwa kwa miezi 6
Dkt. Kalemani: Mradi huu utakapokamilika utazalisha Megawati 2,115 ambazo zitatumika kuendesha treni ya umeme. Umeme huu pia utasafirishwa hadi Chalinze na baadaye Dar es Salaam na Dodoma. Tunatazamia utasaidia sana kuendesha viwanda hapo baadaye
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Kampuni hizi zinazojenga mradi huu zimefanya maajabu makubwa kule nchini Misri. Pacha wako Rais wa Misri, Fattah al-Sisi amejenga Mfereji wa Suez mwingine ndani ya kipindi kifupi. Nyie Marais nyieeee
Rais Magufuli:
Napenda nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kuwa hai siku ya leo. Napenda kumshukuru Waziri wa Nishati kwa kunialika, nawashukuru pia Mabalozi na wageni wetu kutoka Misri. Hiki ni kielelezo cha urafiki
Hapa kwetu umeme unauzwa zaidi ya senti 11, gharama za umeme zinafanya kupanda kwa bei ya bidhaa na mwisho haziwezi kushindana kwenye soko. Nchi yetu imeudhihirishia ulimwengu kuwa ni Taifa huru, mradi huu umepata upinzani kutoka nje na ndani
Nchi yetu ni huru na wala sio masikini, tuliamua kujenga kwa fedha zetu za ndani kupitia kodi zinazokusanywa kutoka kwa Wananchi. Fedha hizi watalipwa Waafrika wenzetu, hii ni ishara kuwa Waafrika tukiamua tunaweza
Huku kuna sehemu chumba kimoja mtu analala kwa dola 3,000. Watu wanakuja na kuondoka huku. Sijui kama Mawaziri mnajua hizo fedha tunapata asilimia ngapi, wala sijui kama vyombo vya usalama vinajua mali kiasi gani inasafirishwa kutoka hapa
Kiasi cha umeme kitakachozalishwa hapa hakijawahi kuzalishwa katika historia ya nchi yetu. Kwa sasa nchi yetu inazalisha umeme Megawati 1,601. Natarajia umeme utakaozalishwa hapa utasaidia kushusha gharama za umeme
Tanzania inaongoza kwa utunzaji wa mazingira. Maeneo tuliyoyatenga ni makubwa mno. Mradi huu utaongeza fursa katika sekta ya kilimo. Kule Mtera na Nyumba ya Mungu shughuli za uvuvi zilishamiri baada ya ujenzi wa mabwawa
Kwenye hii Selous kuna maeneo ya kuwindia (Hunting Block) 47 watu wanakuwa wanaua Simba wanaondoka na gharama kwa mwezi ni Dola 5,000. Ukilipa hiyo unaruhusiwa kuwinda hata ukiua Nyati 10. Ukweli uwindaji haulipi kwenye hii mbuga
Naomba kuanzia leo hili eneo la uwindaji likatwe, tulifanye kuwa National Park. Mataifa mengine hayafanyi sana hizi shughuli. Waziri uende ukakae kwenye Wizara mkapunguze eneo la uwindaji, hilo limesemwa sana lakini utekelezaji umechelewa
Hapa kuna 'Hunting Block' za uwindaji sijasema zifutwe. Na kwa sababu ziko eneo la chini basi eneo la juu ligeuzwe kuwa National Park na iitwe Nyerere National Park. Bwawa liitwe Bwawa la Nyerere ili vizazi vijavyo vikumbuke mambo mazuri ya Nyerere
Juzi zimerudishwa Dhahabu kutoka Kenya ambazo thamani yake ni zaidi ya bilioni 5, hizo Fedha zianze kujenga barabara kutoka Fuga kuja hapa. Tuanze kutengeneza pole pole hizi Kilomita 60. Leo watu wanaweza wasielewe
Serikali imeendelea kutekeleza miradi mingine na tunatekeleza miradi mikubwa ya kusafirisha umeme. Naipongeza Wizara ya Nishati na TANESCO kwa miradi hii ambayo imepunguza mgao wa umeme. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni
Kutokana na TANESCO kupunguza kuagiza vifaa kama nguzo na 'transformer' kutoka nje, Viwanda 15 vimeanzishwa na kuzalisha ajira zaidi ya 3,000. Niwasisitize Wakandarasi kutekeleza mradi huu ndani ya wakati na unatarajiwa kutimia Juni 2022
Kumekuwa na mabishano kati ya NIC(Wanaotoa Bima), TANESCO na Makampuni yanayojenga hapa. Bima lazima itolewe na Serikali, ole wenu akasaini Bima na mtu mwingine. Vibali vya Wafanyakazi vitolewe mapema lakini isiwe utolewaji holela
Wananchi wa eneo hili ndio wakapewe kipaumbele cha ajira kwa sababu wao ndio wamelilinda pori hili tangu kuumbwa kwa dunia. Vyombo vya ulinzi na usalama, viuchukue mradi huu kama mboni ya nchi. Nitashangaa kama JKT hawatahusika kufanya kazi hapa
Natoa wito kwa Wizara kuanza kutekeleza kuzalisha umeme kwa njia nyingine kama jua, joto na upepo. Wananchi kama Pwagu wa kule Njombe wanaojitokeza kuzalisha umeme waungwe mkono kwani wanaweza kuzalisha umeme katika vijiji vyao
Ndugu zangu Wananchi namalizia na maneno haya, 'Ukiona umeenda kwenye pori na nyuki ni wakali sana ujue kuna asali'. Hapa kuna asali ndio maana watu walipiga kelele. Ukiamua kufanya mradi wako fanya usisubiri watu wakushauri
Huku kuna hoteli kubwa kuliko hoteli za Dar es Salaam. Chumba kimoja dola 3,000 na ina vyumba 15. Sijui kama Serikali inapata mapato. Muda wa kuchangamka ni sasa. Wizara ya Maliasili kagueni hiyo hoteli mjue Serikali inaingiza kiasi gani.
PIA SOMA
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
HISTORIA
Rais Magufuli aliwasili Rufiji akitokea Dar es Salaam akitumia treni ya reli ya TAZARA kwa kupitia Fuga na Kisaki
UPDATE:
Waziri wa Nishati, Medard Kalemani;
Rais ulipotuita Ikulu kutueleza ndoto yako kuhusu mradi huu, wengi hatukuelewa lakini sasa tumeanza kukuelewa. Mradi huu utatekelezwa kwa miezi 42 na mpaka sasa umeshatekelezwa kwa miezi 6
Dkt. Kalemani: Mradi huu utakapokamilika utazalisha Megawati 2,115 ambazo zitatumika kuendesha treni ya umeme. Umeme huu pia utasafirishwa hadi Chalinze na baadaye Dar es Salaam na Dodoma. Tunatazamia utasaidia sana kuendesha viwanda hapo baadaye
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Kampuni hizi zinazojenga mradi huu zimefanya maajabu makubwa kule nchini Misri. Pacha wako Rais wa Misri, Fattah al-Sisi amejenga Mfereji wa Suez mwingine ndani ya kipindi kifupi. Nyie Marais nyieeee
Rais Magufuli:
Napenda nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kuwa hai siku ya leo. Napenda kumshukuru Waziri wa Nishati kwa kunialika, nawashukuru pia Mabalozi na wageni wetu kutoka Misri. Hiki ni kielelezo cha urafiki
Hapa kwetu umeme unauzwa zaidi ya senti 11, gharama za umeme zinafanya kupanda kwa bei ya bidhaa na mwisho haziwezi kushindana kwenye soko. Nchi yetu imeudhihirishia ulimwengu kuwa ni Taifa huru, mradi huu umepata upinzani kutoka nje na ndani
Nchi yetu ni huru na wala sio masikini, tuliamua kujenga kwa fedha zetu za ndani kupitia kodi zinazokusanywa kutoka kwa Wananchi. Fedha hizi watalipwa Waafrika wenzetu, hii ni ishara kuwa Waafrika tukiamua tunaweza
Huku kuna sehemu chumba kimoja mtu analala kwa dola 3,000. Watu wanakuja na kuondoka huku. Sijui kama Mawaziri mnajua hizo fedha tunapata asilimia ngapi, wala sijui kama vyombo vya usalama vinajua mali kiasi gani inasafirishwa kutoka hapa
Kiasi cha umeme kitakachozalishwa hapa hakijawahi kuzalishwa katika historia ya nchi yetu. Kwa sasa nchi yetu inazalisha umeme Megawati 1,601. Natarajia umeme utakaozalishwa hapa utasaidia kushusha gharama za umeme
Tanzania inaongoza kwa utunzaji wa mazingira. Maeneo tuliyoyatenga ni makubwa mno. Mradi huu utaongeza fursa katika sekta ya kilimo. Kule Mtera na Nyumba ya Mungu shughuli za uvuvi zilishamiri baada ya ujenzi wa mabwawa
Kwenye hii Selous kuna maeneo ya kuwindia (Hunting Block) 47 watu wanakuwa wanaua Simba wanaondoka na gharama kwa mwezi ni Dola 5,000. Ukilipa hiyo unaruhusiwa kuwinda hata ukiua Nyati 10. Ukweli uwindaji haulipi kwenye hii mbuga
Naomba kuanzia leo hili eneo la uwindaji likatwe, tulifanye kuwa National Park. Mataifa mengine hayafanyi sana hizi shughuli. Waziri uende ukakae kwenye Wizara mkapunguze eneo la uwindaji, hilo limesemwa sana lakini utekelezaji umechelewa
Hapa kuna 'Hunting Block' za uwindaji sijasema zifutwe. Na kwa sababu ziko eneo la chini basi eneo la juu ligeuzwe kuwa National Park na iitwe Nyerere National Park. Bwawa liitwe Bwawa la Nyerere ili vizazi vijavyo vikumbuke mambo mazuri ya Nyerere
Juzi zimerudishwa Dhahabu kutoka Kenya ambazo thamani yake ni zaidi ya bilioni 5, hizo Fedha zianze kujenga barabara kutoka Fuga kuja hapa. Tuanze kutengeneza pole pole hizi Kilomita 60. Leo watu wanaweza wasielewe
Serikali imeendelea kutekeleza miradi mingine na tunatekeleza miradi mikubwa ya kusafirisha umeme. Naipongeza Wizara ya Nishati na TANESCO kwa miradi hii ambayo imepunguza mgao wa umeme. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni
Kutokana na TANESCO kupunguza kuagiza vifaa kama nguzo na 'transformer' kutoka nje, Viwanda 15 vimeanzishwa na kuzalisha ajira zaidi ya 3,000. Niwasisitize Wakandarasi kutekeleza mradi huu ndani ya wakati na unatarajiwa kutimia Juni 2022
Kumekuwa na mabishano kati ya NIC(Wanaotoa Bima), TANESCO na Makampuni yanayojenga hapa. Bima lazima itolewe na Serikali, ole wenu akasaini Bima na mtu mwingine. Vibali vya Wafanyakazi vitolewe mapema lakini isiwe utolewaji holela
Wananchi wa eneo hili ndio wakapewe kipaumbele cha ajira kwa sababu wao ndio wamelilinda pori hili tangu kuumbwa kwa dunia. Vyombo vya ulinzi na usalama, viuchukue mradi huu kama mboni ya nchi. Nitashangaa kama JKT hawatahusika kufanya kazi hapa
Natoa wito kwa Wizara kuanza kutekeleza kuzalisha umeme kwa njia nyingine kama jua, joto na upepo. Wananchi kama Pwagu wa kule Njombe wanaojitokeza kuzalisha umeme waungwe mkono kwani wanaweza kuzalisha umeme katika vijiji vyao
Ndugu zangu Wananchi namalizia na maneno haya, 'Ukiona umeenda kwenye pori na nyuki ni wakali sana ujue kuna asali'. Hapa kuna asali ndio maana watu walipiga kelele. Ukiamua kufanya mradi wako fanya usisubiri watu wakushauri
Huku kuna hoteli kubwa kuliko hoteli za Dar es Salaam. Chumba kimoja dola 3,000 na ina vyumba 15. Sijui kama Serikali inapata mapato. Muda wa kuchangamka ni sasa. Wizara ya Maliasili kagueni hiyo hoteli mjue Serikali inaingiza kiasi gani.
PIA SOMA
- Arab Contractors na Elsewedy Electric Kukabidhiwa Rasmi Eneo la Rufiji (PHPP) Kesho
- Arab Contractors wakabidhiwa Billion 688.6 kama malipo ya awali mradi wa umeme wa maporomoko ya mto Rufiji
- Serikali Yakabidhi Eneo La Mradi Wa Umeme Wa Maji Mto Rufiji Kwa Mkandarasi Tayari Kwa Kazi Kuanza
- Rais Magufuli kuzindua mradi wa umeme Mto Rufiji Julai 26, 2019
- SADC yamuunga mkono Rais Dkt Magufuli ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme Rufiji
- Uzinduzi Mradi wa Umeme, mto Rufiji: Rais Magufuli aagiza sehemu ya Selous kuwa Hifadhi ya Taifa
- Mbunge Sospiere Mukweli ameniogopesha kwa kauli yake kuhusu ujenzi wa bwawa la Rufiji; je, kuna haja ya wabunge wote kupimwa akili?
- Mradi wa Kufua Umeme Rufiji (MW 2115) uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika
- Kampuni ya ElSewedy Electric Co inayotengeneza bwawa la umeme Rufiji imewekewa vikwazo, haitaweza kukopesheka nje
- Waziri Makamba: Msitegemee wala kutarajia bwawa la mto Rufiji kujazwa maji mwezi Machi
- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asema Serikali itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya mradi wa umeme wa mto Rufiji
- Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere Hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda
- Waziri Makamba: Ujenzi wa tuta kwenye bwawa la mwl Nyerere umekamilika
- Maji katika bwawa la Nyerere kuanza kujazwa 15/11/2021 na 13/04/2022 litakuwa limejaa tayari kwa majaribio
- PM Majaliwa: Bwawa la umeme kukamilika Juni 2022
- Tanesco:- Bwawa la Nyerere litakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme Megawati 2115 hata kama mvua haijanyesha kwa miaka 2
- Waziri Kalemani: Bwawa la Nyerere kujazwa Maji Novemba 15, 2021. Umeme wa maji ni nafuu kuliko wa vyanzo vingine
- Kutokukamilika kwa Mradi wa Umeme Rufiji mwaka 2022 kama ilivyotakiwa na sasa Kukamilika 2024 ni Kumtukana na Kumdhalilisha Hayati Dkt. Magufuli
- Rais Samia kuzindua zoezi la ujazaji maji katika Bwawa la Julius Nyerere, Disemba 22
- Makamba: Ujenzi wa Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere umefikia asilimia 67
- Makamba: Sisi tumeamua kuwa wakweli, bwawa la Nyerere linaisha Juni 2024. Adai tarehe ya mwanzo isingewezekana kwa namna yoyote
- Makamba: Itachukua misimu miwili ya mvua kujaza Bwawa la Nyerere
- Maji yatakayojazwa Bwawa la Nyerere (JNHPP) yanaweza kuzalisha Umeme kwa mwaka mmoja bila kutegemea mvua
- Rais Samia akishiriki shughuli ya kuanza kujaza maji Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), 22/12/2022
- TANESCO: Bwawa la Nyerere halitapunguza bei ya umeme
- Serikali: Mashine ya kwanza ya Kufua Umeme Bwawa la Nyerere itawashwa Mwezi Februari 2024
- Rais Samia: Uzalishaji Umeme Bwawa la Nyerere kuanza Januari 2024
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Kamati ya Bunge: Bwawa la Nyerere litakamilika Juni 2024, Tsh. Trilioni 5.85 zimelipwa tayari
- Biteko: Shida ya umeme sasa basi, megawati 235 zimeingia Grid ya Taifa
- Rais Samia: Suluhu ya Umeme itapatikana Aprili 2024 baada ya kuanza uzalishaji wa Megawatt 470-500 katika Bwawa la Mwalimu Nyerere!
- Dotto Biteko: Tumezima mtambo wa bwawa la Mwl Nyerere
- TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma
- Profesa Tibaijuka: Mafuriko ya Rufiji hayajasababishwa na Ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ila limeshindwa kuregulate mafuriko!
- Mtambo wa pili bwawa la Nyerere kuwashwa, kumaliza kabisa mgao wa umeme nchini
TUHUMA ZA UFISADI NA HUJUMA
- Mtaalam: Watanzania mnadanganywa Stiglers Gorge haiwezekani kwani Kina cha Maji Mto Rufiji kinapungua mno
- Hatma ya mradi Stiegler’s Gorge: Hatakama hatukubaliana kiitikadi, tukubaliane katika Ushauri wa kitaalam
- Hotuba ya bajeti Nishati; Miradi ya Rufiji na gesi itaumiza nchi: Mnyika aonya
- Tuambiwe ukweli: Stiglers Gorge inaweza kuwa maafa makubwa kwa taifa badala ya furaha
- Lissu: Serikali na benki hazina uwezo wa kujenga bwawa la Umeme Rufiji
- CAG: Bwawa la Nyerere liliharakiswa
- Polepole: Bwawa la Nyerere ni mradi wa kufa na kupona hatutakubali wahuni wauchezee, Winchi ni kitu kidogo sana!
- Inaumiza sana kuona mradi wa bwawa la Nyerere unahujumiwa wazi wazi
- Unakataje miti milioni 4 ili kujenga la umeme (JNHPP)
- Makamba: Mradi wa JNHPP upo nyuma kwa siku 477 (yaani mwaka na zaidi ya siku 100)
- UFISADI: Mpina aibua tuhuma za upigaji wa Sh. Trilioni 1.5 Bwawa la Nyerere
HISTORIA
- Mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere katika maporomoko ya mto rufiji unaotekelezwa na Serikali uliasisiwa na Baba wa Taifa mwaka 1975
- CAG: Mradi wa Umeme wa Bwawa la Nyerere unatumia upembuzi wa mwaka 1970
- Mhandisi Mkazi, Upembuzi yakinifu wa 1980 unatumika bwawa la JNHPP
- Mwalimu Nyerere aliomba fedha Mradi wa Bwawa la Umeme Rufiji