Naomba msaada wenu ndugu zangu,ni muda mrefu sana nimekuwa nikisumbuliwa na muwasho usoni,shingoni hadi kifuani na imepelekea ngozi kuwa na mabaka meusi na meupe. Tiba pekee ambayo hunisaidia kwa muda ni prednisolone tabs,wiki moja baada ya kumaliza doz tatizo hujirudia tena. Nilipima allege na nikaambiwa nisikae maeneo yenye vumbi,pia nilalie godoro lenye plastic cover,nimetekeleza lakini hali iko vile vile. Kwa mwenye uwezo au ushauri wa tiba naomba anisaidie.