Uzito wa Vicoba vyako uzingatie mzani wa uchumi wako

Uzito wa Vicoba vyako uzingatie mzani wa uchumi wako

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
💼 MHADHARA WA 11:

Hakikisha uzito wa VICOBA/au MICHEZO YA KUPEANA HELA unayocheza usizidi Mzani wa MFUKO (UCHUMI) wako. Kwa mfano upo kwenye uanachama wa VIKUNDI VYA MICHEZO YA KUPEANA HELA au VICOBA zaidi ya kimoja, halafu kila ifikapo muda wa marejesho ya madeni uliyokopa au muda wa kuweka hisa unapatwa na KICHAA CHA SAA 24, yaani huna raha ndani kwako - hiyo ni mbaya sana.

Kama utafanya biashara ambayo itakuwa inalipa madeni makubwa nje kuliko faida inayoingia ndani, ni lazima utafunga hiyo biashara - yaani hata ndoa yako utahisi inakupa kichefu chefu.

Kwa hiyo kama uzito wa VICOBA/au MICHEZO YA KUPEANA HELA itazidi Mzani wa MFUKO (UCHUMI) wako, au VICOBA unavyocheza hadhi yake iko juu haiendani na hali yako wala uchumi wako; ndugu yangu tegemea kutumbukia kwenye shimo la:

1. Msongo wa mawazo.
2. Kudanga - Ili kupata hela ya marejesho.
3. Kuuza assets zako muhimu kwa bei ya hasara (Mfano nyumba, Kiwanja, gari, duka, vitu vya ndani, n.k).
4. Kuikimbia nyumba yako - kutwa kushinda Bar au maskani ili kuwakwepa wahasibu wa Vicoba.
5. Ugomvi wa mara kwa mara kwenye ndoa yako, au kutengana kwenye ndoa.
6. Kumchukia mumeo/mkeo/mpenzi wako bila sababu ya msingi huku ukichukizwa na hali yake ya maisha.

By: RIGHT MARKER-TZ
Mbezi Louis, Dar es Salaam,
Sept 20, 2024.

PIA SOMA
- Marejesho ya mikopo bubu na VICOBA yazidisha wimbi la wizi mjini na vijini
 
💼 MHADHARA WA 11:

Hakikisha uzito wa VICOBA/au MICHEZO YA KUPEANA HELA unayocheza usizidi Mzani wa MFUKO (UCHUMI) wako. Kwa mfano upo kwenye uanachama wa VIKUNDI VYA MICHEZO YA KUPEANA HELA au VICOBA zaidi ya kimoja, halafu kila ifikapo muda wa marejesho ya madeni uliyokopa au muda wa kuweka hisa unapatwa na KICHAA CHA SAA 24, yaani huna raha ndani kwako - hiyo ni mbaya sana.

Kama utafanya biashara ambayo itakuwa inalipa madeni makubwa nje kuliko faida inayoingia ndani, ni lazima utafunga hiyo biashara - yaani hata ndoa yako utahisi inakupa kichefu chefu.

Kwa hiyo kama uzito wa VICOBA/au MICHEZO YA KUPEANA HELA itazidi Mzani wa MFUKO (UCHUMI) wako, au VICOBA unavyocheza hadhi yake iko juu haiendani na hali yako wala uchumi wako; ndugu yangu tegemea kutumbukia kwenye shimo la:

1. Msongo wa mawazo.
2. Kudanga - Ili kupata hela ya marejesho.
3. Kuuza assets zako muhimu kwa bei ya hasara (Mfano nyumba, Kiwanja, gari, duka, vitu vya ndani, n.k).
4. Kuikimbia nyumba yako - kutwa kushinda Bar au maskani ili kuwakwepa wahasibu wa Vicoba.
5. Ugomvi wa mara kwa mara kwenye ndoa yako, au kutengana kwenye ndoa.
6. Kumchukia mumeo/mkeo/mpenzi wako bila sababu ya msingi huku ukichukizwa na hali yake ya maisha.

By: RIGHT MARKER-TZ
Mbezi Louis, Dar es Salaam,
Sept 20, 2024.

PIA SOMA
- Marejesho ya mikopo bubu na VICOBA yazidisha wimbi la wizi mjini na vijini
HAKIKA. Ni kuishi kwa akili tu. Mfano mdogo unakuta inahitajika kuchangia vikundi zaidi ya vi4, Tena wamependekeza elf 20 au 15 kwa Mwezi (mfano). Tena siku hizi Whatsapp groups ndio balaa e.g Group la std VII, form 4, form 6, Chuo kwa maana mliosoma kozi moja, kazini, mtaani, familia n.k unakuta inahitajika kuchangia si chini ya laki na 50 kwa Mwezi. Ukijuondoa kwa baadhi ya group kwa kuwapa sababu zenye mashiko wanahisi hutaki umoja na wao. Au unajisikia
 
Back
Top Bottom