Uzuri wa kitu kwa nje si usalama wa ndani

Uzuri wa kitu kwa nje si usalama wa ndani

Anyisile Obheli

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2009
Posts
3,400
Reaction score
320
Papai jama papai, lanipendeza machoni,
Kwa yake rangi papai, halinitoki usoni,
Hata nikifunga tai, nalisogeza mdomoni.
Nikilikata papai, kumbe lishaaoza ndani

Ukiliona ni zuri, machoni linavutia,
Ni kwa yake rangi nzuri, mikononi ukilitia,
Njano na kijani nzuri, na umbole vyavutia,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani

Yapo mapapai mengi, kwa zake rangi tofauti,
Na mitaani kwa wingi, na hayahitaji suti,
Pia sokoni ni mengi, tena hayana masharti,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani.

Ni mazuri sana kwa nje, shida yake kule ndani,
Ukiyaona yalivyo nje, huna swali na ndani,
Yanavutia sana nje, yanachefua kwa ndani,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani
 
Papai la Afrika, vitamini limesheneni,
Ukilikosa hakika, unyafuzi ndani mwilini,
Kiswahili kimepunguka, peni naweka kabatini,
Uozo tukiukwepa, unyafuzi utatuua.
 
Papai la Afrika, vitamini limesheneni,
Ukilikosa hakika, unyafuzi ndani mwilini,
Kiswahili kimepunguka, peni naweka kabatini,
Uozo tukiukwepa, unyafuzi utatuua.
pole sana ndugu pole, upendaye vya kuoza,
tumbo kupiga kelele, kitandani lakulaza,
na njaa isikukele, hata kula vya kuoza,
kweli ongeza bidii, unyafuzi kuukwepa.
 
anyisile wa obheli, mbona kwikwi kulikoni?
umeipata asali, kuila waitamani
sasa mbona wakejeli, kisa imeoza ndani
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

vile vinavyopendeza, wenzako wavisifia
kwafujo wanavikuza, ndo mana vina mikia
sasa wewe wavibeza, kisa vimejivundia
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

hata noti za thamani, bidhaa twanunulia
zimepita pande gani, nawewe kukufikia
hauziachi kwanini, bidhaa kujipatia
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

papai ni tunda tamu, lenye ladha maridhawa
wenzako hatwishi hamu, tulilapo twapagawa
twala hatujilaumu, hatuhitaji kunawa
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

kuna njia nyingi mno, za kutafuna papai
hata ushike kiuno, utaona haifai
kula utoe miguno, papai hutakinai
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

kula umechuchumaa, papai litaingia
au kula umekaa, kitako kujikalia
papai tunda balaa, utamu wa asilia
ukimchunguza bata, huwezi kumla ndugu

papai kama nanasi, twayala kila wakati
kula kwataka nafasi, na kupanga mikakati
vinginevyo hutapasi, utaja pigwa kibuti
papai tunda adhimu, ukisusa sisi twala.
 
Ni ya kweli bwana Mundu, usichunguze ya bata,
Hata kule kishumundu, wanajivunia bata,
Wala hana ya utundu, kama ya mbuzi matata,
Wa muhimu umakini, ili kuboresha afya.

Mundu uwe na makini, papai na lake umbo.
Usijesema maskini, na yamenikuta mambo,
Likioza jalalani, usiliweke kwa tumbo,
Wa muhimu umakini, ili kuboresha afya.

Halifanani na bata, lenyewe mwili halina,
Uchafu akila hata, matatizo ni hakuna,
Ni halali kumla bata, papai kutofanana,
Wa muhimu umakini ili kuboresha afya.

Papai likishaoza, halifai kwa chakula,
Ni heri kulichunguza, hata kabla hujalila,
Maamuzi kugeuza, uozo usije kula,
Wa muhimu umakini, ili kuboresha afya.

Mimi bado naosia, uzuri wa kitu si nje,
Tusipende kukisia, tena wala tusionje
Na bomba twavisifia, tukishaviona kwa nje
Wa muhimu umakini, ili kuboresha afya.
 
mi hapo sina changu,papai kulichambua,
nililipata kitangu,mbolea iliumua,
pozi papa lipo kwangu,wambea huwaumbua,
kama lako bovu papa,i njoo uone langu,

kwa nje linachanua,usukumani patia,
kwa ndani pia ubua,kufunzwa ndiko papai,
mkuu hili tambua,asili mia patia,
kama lako bovu papa,i njoo uone langu,
 
Back
Top Bottom