Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,400
- 320
Papai jama papai, lanipendeza machoni,
Kwa yake rangi papai, halinitoki usoni,
Hata nikifunga tai, nalisogeza mdomoni.
Nikilikata papai, kumbe lishaaoza ndani
Ukiliona ni zuri, machoni linavutia,
Ni kwa yake rangi nzuri, mikononi ukilitia,
Njano na kijani nzuri, na umbole vyavutia,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani
Yapo mapapai mengi, kwa zake rangi tofauti,
Na mitaani kwa wingi, na hayahitaji suti,
Pia sokoni ni mengi, tena hayana masharti,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani.
Ni mazuri sana kwa nje, shida yake kule ndani,
Ukiyaona yalivyo nje, huna swali na ndani,
Yanavutia sana nje, yanachefua kwa ndani,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani
Kwa yake rangi papai, halinitoki usoni,
Hata nikifunga tai, nalisogeza mdomoni.
Nikilikata papai, kumbe lishaaoza ndani
Ukiliona ni zuri, machoni linavutia,
Ni kwa yake rangi nzuri, mikononi ukilitia,
Njano na kijani nzuri, na umbole vyavutia,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani
Yapo mapapai mengi, kwa zake rangi tofauti,
Na mitaani kwa wingi, na hayahitaji suti,
Pia sokoni ni mengi, tena hayana masharti,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani.
Ni mazuri sana kwa nje, shida yake kule ndani,
Ukiyaona yalivyo nje, huna swali na ndani,
Yanavutia sana nje, yanachefua kwa ndani,
Nikilikata papai, kumbe lishaoza ndani