Uzuzu wa kisiasa,kidemokrasia na kikatiba Tanzania nini kifanyike?

Uzuzu wa kisiasa,kidemokrasia na kikatiba Tanzania nini kifanyike?

Kichwamoto

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2019
Posts
3,403
Reaction score
4,692
Habari za kutwa miamba na majabali ya jukwaa mujarabu.

Rejeeni kichwa cha maada, nimetafakari nyakati nyingi na kwa marudio kwanini nchi hii ina ombwe kisiasa,kidemokrasia na kikatiba.

Kwanini uhuru katika nyanja hizo si kipaumbele kwa Taifa hili?

Mara nyingi maswali yangu hujikita kitaaluma, sera mfanano za kidunia katika nyanja mbalimbali, mfano Bunge la muundo wa jumuiya ya madola, katiba kufuata muundo wa uingereza, kuwa na mfumo wa siasa za vyama vingi na miongozo yake.

Uhuru wa vyombo vya habari, uhuru binafsi wa mmoja mmoja wa kimawazo, maoni, ushauri na ukosoaji.

Katika nyanja zingine tunajinasibu kufanana na wengine mfano nchi majirani na ng'ambo, kwanini inapokuja kwenye mambo msingi na chocheo kimaendeleo na ukombozi wa kifikra katika taifa hasa siasa, demokrasia na kikatiba sio kipaumbele?

Je, mnufaika ni nani?ili iweje?na dira yake anaenda wapi?

Wanaotutaka tuwe mazuzu kwenye kila kitu, je, dira yao ni nini?

Tanzania ya Mazuzu haikubaliki.

Tupige vita uzuzu wa kulazimishwa.
 
Mnufaika ndio huyo aliyeko madarakani, nae hutumia njia kuu mbili;

1. Kuwanunua wapinzani wasiojitambua, na kuwadanganya wale wapinzani wenye viherehere walafi wa madaraka.

Mfano wapo wapinzani wanaojua kabisa uchaguzi nchi hii hauwezi kuwa free and fair, lakini kwa tamaa zao tu na kujipendekeza, na wakati wengine wakigoma kushiriki; bado wao hushiriki chaguzi zinazofuata wakitegema mambo kuwa sawa, lakini huishia kupigwa tu.

2. Ujinga wa wananchi kwa ujumla wao wengi hawajitambui, wengi hudhani Katiba Mpya ni ya wanasiasa, hawajui hata maisha yao yanategemea uwepo wa sheria nzuri zitakazowalinda wao na mali zao, na zaidi kuwasaidia pale watakapodai haki zao.

Huu ujinga wa wananchi nao uliochangiwa na uwepo wa CCM madarakani kwa muda mrefu, unaendelea kuinufaisha CCM kwa kuwa maeneo mengi penye elimu ndogo na umasikini mkubwa nchi hii, ndio CCM angalau hupata kura huko, lakini mijini hali yao ni mbaya.

3. Uoga wa watanzania, japo wengi mitaani hulalamika juu ya hali ya kisiasa inayoendelea nchini, lakini hakuna anayethubutu kuonesha kwa vitendo kukerwa na hali hiyo na kuwa tayari kuibadilisha.

Mfano maandamano, japo yapo kisheria na ni haki ya wananchi, lakini akijitokeza kamanda wa polisi wa mkoa akayapiga marufuku hakuna yeyote anayeamua kushinikiza upatikanaji wa haki hiyo zaidi ya viongozi wachache wa vyama vya siasa.
 
Habari za kutwa miamba na majabali ya jukwaa mujarabu.

Rejeeni kichwa cha maada, nimetafakari nyakati nyingi na kwa marudio kwanini nchi hii ina ombwe kisiasa,kidemokrasia na kikatiba.

Kwanini uhuru katika nyanja hizo si kipaumbele kwa Taifa hili?

Mara nyingi maswali yangu hujikita kitaaluma, sera mfanano za kidunia katika nyanja mbalimbali, mfano Bunge la muundo wa jumuiya ya madola, katiba kufuata muundo wa uingereza, kuwa na mfumo wa siasa za vyama vingi na miongozo yake.

Uhuru wa vyombo vya habari, uhuru binafsi wa mmoja mmoja wa kimawazo, maoni, ushauri na ukosoaji.

Katika nyanja zingine tunajinasibu kufanana na wengine mfano nchi majirani na ng'ambo, kwanini inapokuja kwenye mambo msingi na chocheo kimaendeleo na ukombozi wa kifikra katika taifa hasa siasa, demokrasia na kikatiba sio kipaumbele?

Je, mnufaika ni nani?ili iweje?na dira yake anaenda wapi?

Wanaotutaka tuwe mazuzu kwenye kila kitu, je, dira yao ni nini?

Tanzania ya Mazuzu haikubaliki.

Tupige vita uzuzu wa kulazimishwa.
Wakabdhibiwe nchi hawa MaGENIUS ili nchi iwe kama DUBAI.

Popoooooossssss

IMG_20211103_093523.jpg
 
Ukistaajabu ya siasa ya Tanzakiza utashangaa ya ACT wazalendo kutaka tume huru ya uchaguzi huku wakiacha msingi wa sheria mama katiba
 
bila kubadili katiba tukawaondoa ccm madarakani tutaendelea kuwa mazuzu wa kulazimishwa coz katiba iliyopo inawafavour na kuwalinda.
 
Back
Top Bottom