Kuna siku niliandika mahali, 'mila na tamaduni' ni ubombo aka bone marrow, elimu ni vinyweleo.
Mtu aliyekulia kwenye mfumo dume (ikijumuisha, kupanga uzazi ni mambo ya wanawake), hata asome vipi hiyo kitu haiwezi kumtoka ndani ya siku 2.
Inahitaji uzoefu wa jambo baya ama kujamiiana na tamaduni zingine kwa kipindi kirefu kujua hili ni suala la pamoja kati ya mke na mme. Kuna wanaume, piga ua haruhusu mkewe kutumia njia za uzazi wa mpango wa kisasa, lakini unaweza kukuta mke alishapata kuharibikiwa mimba ndio akagundua hilo.
Kwa hiyo, kuamka tu over a night na kumwambia mwanamme huku kwetu afanye aidha utaambiwa unatafuta 'shingira-ingredients za kichawi' ana umepatwa na mapepo. Ni jambo la kujadiliana, ikibidi kuhudhuria vipindi vya ushauri nasaha vya uzazi pamoja.
Pamoja na hayo, vasectomy nayo ina madhara kwa akina baba, kama kansa kama haikufanyika vizuri, msongo wa mawazo au mzio wa muda mrefu. Na pia isipofanyika vizuri inaweza isiwe effective, mbegu za mahindi zikazaliwa na uchavushaji ukafanyika kama kawaida.
Hili jambo la mmoja kujitolea kuchukua jukumu hili sio rahisi kivile, lazima apitie kashkash, ndo maana ni bora kugawana wote 2, kila mmoja acheze sehemu yake, safe days au ndomu.
Very safe lakini hebu jaribu kusuggest vasectomy kwa mtu, hata wale wasomi wenye uelewa mkubwa wa kupambanua mambo hawakubali kabisa.